Mzimu wa Lissu ndio tatizo kubwa kwa sasa kuliko mtu yeyote hapa Tanzania

leonaldo

JF-Expert Member
Oct 26, 2014
2,585
3,179
Kwa hali ya kisiasa ilivyo hapa Tanzania kwa sasa Tundu Lisu ni tatizo kubwa kwa CCM kuliko ilivyo kuwa kwa Lowasa kwenye uchaguzi wa mwaka 2015,lakini kuung'amua na kuukubari ukweli huu inahitaji jicho la tatu.
Wapo wengi wanajiuliza kwa nini CCM inaonekana kuwa na wasiwasi mwingi mwaka huu wa uchaguzi licha ya kuwa inajivunia kutekeleza ilani yake ya uchaguzi pengine kwa kiasi kikubwa kuliko wakati wowote.
zipo sababu kadhaa ninazoziona Mimi kama;
  1. Katika kipindi hiki cha miaka miaka Minne CCM imejiweka mbali na wananchi Kuliko wakati wowote ule,hasa baada ya kuteua makada WA chama kushika nyadhifa za kiserikali, mbwembwe za makada hawa na unyanyasaji wa raia huku wakijinasibisha na chama,ulikiondoa chama kuwa cha kisiasa kwa ushawishi na kuwa chama dola cha kimabavu hivyo kuogopewa na kupendwa kinafiki.
  2. Kuzuia mikutano ya kisisa kwa muda mrefu na kubana Uhuru wa habari kumewafanya wananchi kuwa na kiu ya kujua upande wa pili,hii itafanya mikutano ya wapinzani kuwa na mafuriko ya aina yake na watakacholishwa hapo kitakuwa kipya na CCM hawatakuwa na muda WA kutosha kupangua hoja za wapinzani.
  3. Kugombea kwa Lisu katika nafasi ya urais na hasa Kama atakuja Kati ya Mwezi April mwishoni au Mei, Watanzania kwa asili yao ni watu wanaomsubiri masihi wao wasie mjua kumbukumbu zipo,Mrema 1995, Lowassa 2015, Then who's next? Bila Shaka ni Lisu na CCM wanalijua hili. Na sababu kubwa ya wananchi ni kuhitaji mtu mtenda haki, shupavu na jasiri. Kuumizwa kwa Lisu na kuwepo kwake nje ya nchi kwa mda mrefu atakuwa mtu mpya kwa wakati sahihi na kila mtu atataka kumsikiliza na ninaamini atavuta watu wengi kuliko Lowassa 2015
  4. Uwezo wa Lisu kujieleza ni mzuri hili halina ubishi, ninachokiona kwa uwazi agenda ya uchaguzi mwakani huu itakuwa ni haki za binadamu. Kutupwa kwa katiba mpya,makosa yaliyofanywa na viongozi wa chini kuhusiana na haki za watu yataifanya CCM kujitetea kwa mda mwingi kuliko kuelezea sera zao.
Mzimu wa Lisu ndio tatizo kubwa kwa sasa kuliko mtu yeyote hapa Tanzania
kete ya mwisho na ya msingi ni kumzuia kugombea au la kuvigawa vyama vya upinzani visiungane na mamluki Kama Ben maembe wamwagwe upinzani.
 
Unamzungumzia Lisu huyu aliye kiri ku uandaa waraka wa Mafisadi na kuzunguka ku utangaza nchi nzima na baada ya yeye na DJ kupewa vipande vya fedha wakameza matapishi yao kwa kukataa na kupinga hadharani kuwa mamvi si fisadi. Yaani leo hii awe tishio wakati akuna mtanzania mwenye akili timamu aliye sahau ya 2015.
 
Unamzungumzia Lisu huyu aliye kiri ku uandaa waraka wa Mafisadi na kuzunguka ku utangaza nchi nzima na baada ya yeye na DJ kupewa vipande vya fedha wakameza matapishi yao kwa kukataa na kupinga hadharani kuwa mamvi si fisadi. Yaani leo hii awe tishio wakati akuna mtanzania mwenye akili timamu aliye sahau ya 2015.
Kati ya watu ambao hawakumeza matapishi yao ni pamoja na Lisu na Mnyika Kama una ushahidi weka hapa.
 
Utajuta milele kubadili gia angani
IMG_20200305_082705.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mleta mada una maono ya mbali sana!kwa utawala wa jpm ni rahisi mpinzani kufanya kampeni hata kama mpinzani hana uelewa wowote wa kisiasa!!Jpm ni rahisi sana kumpaka mavi kuliko hata shetani halisi!!KAMPENI KUU ITAKUWA HAKI ZA BINADAMU,MAUAJI YA KUTISHA AMBAYO MENGINE HATUJAFUMBULIWA MACHO BADO,SISI WATUMISHI TUMESAHAULIKA NA MAISHA KUWA MAGUMU SANA!!!!!!Kama kampeni zitakuwa huru jpm atadhalilika sana hata kura milion moja hatopata!!!
 
Unamzungumzia Lisu huyu aliye kiri ku uandaa waraka wa Mafisadi na kuzunguka ku utangaza nchi nzima na baada ya yeye na DJ kupewa vipande vya fedha wakameza matapishi yao kwa kukataa na kupinga hadharani kuwa mamvi si fisadi. Yaani leo hii awe tishio wakati akuna mtanzania mwenye akili timamu aliye sahau ya 2015.
Kati ya watu ambao hawakulamba matapishi yao kuhusu mafisadi ni pamoja na Lisu na Mnyika weka ushahidi hapa Kama unao
Utajuta milele kubadili gia anganiView attachment 1377605

Sent using Jamii Forums mobile app
Huu ni mfano wa mkakati dhaifu kabisa wa kuushinda upinzani,chini ya unezi wa Polepole CCM haijiwezi kabisa safari hii mtamkumbuka Nape.
 
Uwezo wa Lisu kujieleza ni mzuri hili halina ubishi, ninachokiona kwa uwazi agenda ya uchaguzi mwakani huu itakuwa ni haki za binadamu. Kutupwa kwa katiba mpya,makosa yaliyofanywa na viongozi wa chini kuhusiana na haki za watu yataifanya CCM kujitetea kwa mda mwingi kuliko kuelezea sera zao.
Lissu ni kiumbe aliyejaliwa kuwa na uwezo mkubwa wa kushawishi akikueleza jambo hata ulikatae vipi utakuwa umeamua tu kulikataa lakini ukweli utaukubali.

Tunahitaji Rais mtenda haki swala la maendeleo tutajiletea sisi wenyewe watanzania kwa nguvu zetu na kodi zetu.
 
Mleta mada una maono ya mbali sana!kwa utawala wa jpm ni rahisi mpinzani kufanya kampeni hata kama mpinzani hana uelewa wowote wa kisiasa!!Jpm ni rahisi sana kumpaka mavi kuliko hata shetani halisi!!KAMPENI KUU ITAKUWA HAKI ZA BINADAMU,MAUAJI YA KUTISHA AMBAYO MENGINE HATUJAFUMBULIWA MACHO BADO,SISI WATUMISHI TUMESAHAULIKA NA MAISHA KUWA MAGUMU SANA!!!!!!Kama kampeni zitakuwa huru jpm atadhalilika sana hata kura milion moja hatopata!!!
Na haya yote yako wazi machobi pa watanzania. Kama alikuwa anatafanya akijua 2020 iko mbali ameula wa chuya.
 
Kwa hali ya kisiasa ilivyo hapa Tanzania kwa sasa Tundu Lisu ni tatizo kubwa kwa CCM kuliko ilivyo kuwa kwa Lowasa kwenye uchaguzi wa mwaka 2015,l
Mzimu wa Lisu ndio tatizo kubwa kwa sasa kuliko mtu yeyote hapa Tanzania
Kuzungumzia mzimu wa mtu aliye hai, ni kutaka kumchuria!, mzimu ni wa mtu tuu aliyetangulia mbele ya haki!.
Please stop this!.
P
 
Lissu ni kiumbe aliyejaliwa kuwa na uwezo mkubwa wa kushawishi akikueleza jambo hata ulikatae vipi utakuwa umeamua tu kulikataa lakini ukweli utaukubali.

Tunahitaji Rais mtenda haki swala la maendeleo tutajiletea sisi wenyewe watanzania kwa nguvu zetu na kodi zetu.

..TL pia ni mtu mwenye UPENDO na MCHANGAMFU.

..Tofauti na Jpm ambaye ni KATILI na asiye na mwenye DHARAU.

..Wananchi wakipewa nafasi ya kuwalinganisha hao wawili kura zitaenda kwa TL.
 
Unamzungumzia Lisu huyu aliye kiri ku uandaa waraka wa Mafisadi na kuzunguka ku utangaza nchi nzima na baada ya yeye na DJ kupewa vipande vya fedha wakameza matapishi yao kwa kukataa na kupinga hadharani kuwa mamvi si fisadi. Yaani leo hii awe tishio wakati akuna mtanzania mwenye akili timamu aliye sahau ya 2015.
Jiulize kwanza nani waliomshambulia kwa risasi na ni kwa sababu gani??

Hilo wenzio walishaliona hilo mapema kuwa hawatamuweza Mh Lissu kwa hoja bali kwa mtutu wa bunduki pekee. Sasa aliyepanga na waliotekeleza unyama ule hawana amani. Wamejawa na hofu mno.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuzungumzia mzimu wa mtu aliye hai, ni kutaka kumchuria!, mzimu ni wa mtu tuu aliyetangulia mbele ya haki!.
Please stop this!.
P
Mzimu wa Lisu katika hili ni mambo yasiyo julikana kwa wanaoyajua na wasioyajua na ambayo wanayoyajua hawatataka wasio yajua wayajue he survived to tell the tale
 
Mkuu 'Leonaldo', ni uchambuzi wa kina.

Pengine mimi ningeupa jina la "Mzimu wa Magufuli versus Mzimu wa Lissu", hilo lingekuwa kamilifu zaidi kuwasilisha uliyoyaweka hapa.

Kwa maana, Magufuli kafanya mengi ambayo baadhi (pengine wengi) wangemuunga mkono kwayo kama haya machache na mazito zaidi (Mzimu) yasingekuwepo au angeweza kuyapoza kiustadi, ambao kwa hakika hana.

Kwa hiyo haya ya 'Kimzimu' yamejitokeza kuwa ni mzigo mkubwa kwake kama CHADEMA watajua na kuzitumia njia nzuri wanazoweza kuzitumia kuwakumbusha wananchi kabla hawajaenda kupiga kura.

Acha nisimchambue Lissu kwa sasa, mbali ya 'huruma' juu ya muujiza uliompata na kuwa sehemu ya muujiza kwa taifa letu.
 
kete ya mwisho na ya msingi ni kumzuia kugombea au la kuvigawa vyama vya upinzani visiungane na mamluki Kama Ben maembe wamwagwe upinzani
Kwa sasa hivi kete ni hiyo moja: ya "kumzuia"

Hiyo ya "vyama" itakuwa ni kuipunguzia nguvu CHADEMA na kuleta vurugu tu katika mipango yao.

Wanayo kila sababu ya kusimama kama chama pekee na kuweka wagombea kila sehemu inayohitaji kugombewa.
 
Kwa sasa hivi kete ni hiyo moja: ya "kumzuia"

Hiyo ya "vyama" itakuwa ni kuipunguzia nguvu CHADEMA na kuleta vurugu tu katika mipango yao.

Wanayo kila sababu ya kusimama kama chama pekee na kuweka wagombea kila sehemu inayohitaji kugombewa.

Mkuu nakuunga mkono kwa asilimia mia moja, cdm wasimame kama chama pekee na mgombea awe Tundu Lissu. Ni ukweli usioacha shaka kuwa Lissu ana mvuto na uwezo mkubwa wa kujenga hoja, huyu ndio mgombea pekee anayeweza kunifanya nipige kura, na ndiye mgombea anayeweza kurudisha hamasa ya siasa iliyouliwa na Magufuli kwakuwa hawezi siasa za ushindani. Huyu ndiye mgombea wa upinzani anayeweza kuamsha hamasa ya umma kudai tume huru ya uchaguzi na katiba mpya. Jambo pekee watakaloweza ccm ni kumfunga jela na sio zaidi ya hilo.
 
Mkuu nakuunga mkono kwa asilimia mia moja, cdm wasimame kama chama pekee na mgombea awe Tundu Lissu. Ni ukweli usioacha shaka kuwa Lissu ana mvuto na uwezo mkubwa wa kujenga hoja, huyu ndio mgombea pekee anayeweza kunifanya nipige kura, na ndiye mgombea anayeweza kurudisha hamasa ya siasa iliyouliwa na Magufuli kwakuwa hawezi siasa za ushindani. Huyu ndiye mgombea wa upinzani anayeweza kuamsha hamasa ya umma kudai tume huru ya uchaguzi na katiba mpya. Jambo pekee watakaloweza ccm ni kumfunga jela na sio zaidi ya hilo.

..kifungo kitawasaidia kama ni cha muda mrefu, miaka 15+.

..bahati mbaya kesi alizonazo TL ni za tuhuma ndogo-ndongo.

..sasa baada ya kujaribu kumuua na kushindwa, wakimfunga kwa hivi vikesi vyao visivyo na kichwa wala miguu, umaarufu wa TL utaongezeka.
 
Back
Top Bottom