sungwa.j
JF-Expert Member
- Jan 17, 2016
- 548
- 546
Kwanza kabisa stori yako ina kasoro nyingi sana,Mimi ni mkazi wa Lamadi hapa nikusahihishe Kamanda Kova hajawahi kuja hapa aliyekuja ni Kamanda Siro ni kweli alipiga mkwara wa nguvu sana na akasema kuwa ndani ya siku ya 10 jibu litapatikana,NI kweli hapa kwetu kulikuwa na hili suala la mauaji ya watoto wa kike na wanawake pia na walikuwa wakitolewa viungo vya siri hivyo ni kweli lakini ishu ya Nyageta umepotoshwa,Nyangeta ni dada fulani hivi kama chizi,kwao ni Kyabakali Musoma vijijini huko, Ni mtu hatari sana ana Mambo ya kishirikina kweli anaweza kuja dukani kwako akaomba umpe kitu ile unainama au kugeuka tu unapoteza network na kama Kuna pesa kwenye droo au sehemu yoyote ujue imeshaondoka hiyo,Sasa Kuna watu hapa walimchukua wakaenda nae sehemu mbalimbali hapa TZ wakapiga pesa huko wakaja hapa wakajenga nyumba wakafanya maendeleo pia,wakatokea wengine tena wakamtorosha wakapiga pesa tena wakajenga majumba na wananunua magari,Wengine tena wakamtorosha hivyo hivyo Sasa nafikiri kulitokea kutoelewana kati yao waliokuwa wakimchukua wakadhurumiana ndio Mambo yakatibuka wakasemana ikawa imejulikana wakakamatwa wakaachiwa tena,Sasa yalipojotokeza haya mauaji ya watoto na wamama ndio yakaibuka tena mambo ya Nyangeta wakawa wanahusisha haya Mambo na ishu ya Nyangeta stori ni ndefu nitawachosha naona niishie hapa ila huyo Nyangeta ni dada hatari ana dawa za hatari unaambiwa anaweza kuja kununua kitu dukani kwako akakupa elfu 10 ukiichanganya na pesa nyingine ndio hivyo tena imekula kwako yaani unaambiwa ana staili kibao sana za chuma ulete
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent using Jamii Forums mobile app