Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,399
Wilbur Smith ni mmoja wa waandishi maarufu duniani. Mpaka leo hii alikuwa ameandika vitabu 31 maarufu kama vile When the Lion Feeds, The River God na The Triumph of the Sun, ambacho kimetafsiriwa katika lugha 26.
Vitabu vyote hivi vina mandhari ya bara la Afrika na mzee huyu ambae alizaliwa Zambia miaka 33 iliopita anapenda kuandika kuhusu bara hilo kuzingatia kwamba amewahi kuwa mshauri wa masuala ya kodi katika serikali ya Zambia.
Leo jioni hii mzee Smith amezindua kitabu kipya pale Waterstones, duka maarufu la vitabu lililopo sehemu iitwayo Piccadilly mjini London.Mimi nikiwa mmoja wa wapenzi wa vitabu nilipata nafasi ya kwenda kuona kitabu ambacho kinaitwa Assegai.
Tafsiri sahihi ya assegai ni mkuki na kitabu hiki kinahusu enzi zile za ukoloni ambapo askari wa zamani Leon Courtney ambae amekuwa muwindaji anaingia urafiki na mfanyabiashara tajiri kutoka Ujerumani bwana Count Otto Von Meerbach ambae ana kiwanda cha kutengeneza magari na ndege.
Lakini baadae baba mkubwa wa Leon anaeitwa Penrod Ballantyne ambae ni kamanda wa jeshi la Afrika Mashariki anamshauri Leon kumpeleleza Count Otto Von Meerbach na kumpelekea habari.
Badala yake Leon anampenda mke wa Count Otto Von Meerbach aitwae Eva Von Wellberg. Kabla ya vita kuu ya kwanza ya dunia Leon anashauriwa na Count Von Meerbach kuandaa uasi dhidi ya jeshi la Uingereza la Afrika Mashariki kutoka kwa upande wa Ujerumani kwa kuwashirikisha wanajeshi wa zamani wa makaburu walioshiriki vita maarufu kama "Boer War" nchini Afrika Kusini.
Leon baadae anaachwa kwenye mataa na tena anamwona Eva Von Wellberg akirudi Afrika na mtu mwingine na Leon anatafuta kujua ukweli kuhusu bibie Eva Von Wellberg kwamba ni nani na amejificha nyuma na sanamu kwa minajili gani.
Sasa mzee Smith akanishanga kidogo kwa kauli yake kuhusu afrika pale alipokuwa akijibu baadhi ya maswali na moja ya maswali hayo lilikuwa swali kwamba je yeye ana imani na bara hili ambalo yeye amekua na kuishi humo?
Mzee huyu akajibu kwamba Ulaya Magharibi inavyolichukulia bara la Afrika si vile Waafrika wenyewe wanavyolichukulia bara lao kwa maana ya kuwa bara lenye neema na mambo yote mazuri na kwamba waafrika wanafaidi matunda ya kuwa na bara hilo.
Akaendelea kwa kusema kwamba, waafrika wataendela kulishughulikia bara lao kuelekea mwisho wake na kulirudisha bara hilo kule lilikotoka yaani kabla ya wazungu hawajatia mguu barani humo kwa maana kwamba kutakuwa na mifumo ya ukabila zaidi, udikteta zaidi kuliko mifumo ya kidemokrasia na akamalizia kwa kusema kwamba hio ndo hali ambayo waafrika wanaridhika nayo.
Ninasikitika sana, kwa sababu nikiangalia habari zote zihusuzo ufisadi, rushwa na midubwana mingine nikabakia natafuta majibu.
Kwa wale walioko Marekani na Canada kitabu hicho kitachapishwa tarehe 12 April, Norway tarehe 20 May,Denmark tarehe 25 June, na Netherlands tarehe30 July 2009.
Vitabu vyote hivi vina mandhari ya bara la Afrika na mzee huyu ambae alizaliwa Zambia miaka 33 iliopita anapenda kuandika kuhusu bara hilo kuzingatia kwamba amewahi kuwa mshauri wa masuala ya kodi katika serikali ya Zambia.
Leo jioni hii mzee Smith amezindua kitabu kipya pale Waterstones, duka maarufu la vitabu lililopo sehemu iitwayo Piccadilly mjini London.Mimi nikiwa mmoja wa wapenzi wa vitabu nilipata nafasi ya kwenda kuona kitabu ambacho kinaitwa Assegai.
Tafsiri sahihi ya assegai ni mkuki na kitabu hiki kinahusu enzi zile za ukoloni ambapo askari wa zamani Leon Courtney ambae amekuwa muwindaji anaingia urafiki na mfanyabiashara tajiri kutoka Ujerumani bwana Count Otto Von Meerbach ambae ana kiwanda cha kutengeneza magari na ndege.
Lakini baadae baba mkubwa wa Leon anaeitwa Penrod Ballantyne ambae ni kamanda wa jeshi la Afrika Mashariki anamshauri Leon kumpeleleza Count Otto Von Meerbach na kumpelekea habari.
Badala yake Leon anampenda mke wa Count Otto Von Meerbach aitwae Eva Von Wellberg. Kabla ya vita kuu ya kwanza ya dunia Leon anashauriwa na Count Von Meerbach kuandaa uasi dhidi ya jeshi la Uingereza la Afrika Mashariki kutoka kwa upande wa Ujerumani kwa kuwashirikisha wanajeshi wa zamani wa makaburu walioshiriki vita maarufu kama "Boer War" nchini Afrika Kusini.
Leon baadae anaachwa kwenye mataa na tena anamwona Eva Von Wellberg akirudi Afrika na mtu mwingine na Leon anatafuta kujua ukweli kuhusu bibie Eva Von Wellberg kwamba ni nani na amejificha nyuma na sanamu kwa minajili gani.
Sasa mzee Smith akanishanga kidogo kwa kauli yake kuhusu afrika pale alipokuwa akijibu baadhi ya maswali na moja ya maswali hayo lilikuwa swali kwamba je yeye ana imani na bara hili ambalo yeye amekua na kuishi humo?
Mzee huyu akajibu kwamba Ulaya Magharibi inavyolichukulia bara la Afrika si vile Waafrika wenyewe wanavyolichukulia bara lao kwa maana ya kuwa bara lenye neema na mambo yote mazuri na kwamba waafrika wanafaidi matunda ya kuwa na bara hilo.
Akaendelea kwa kusema kwamba, waafrika wataendela kulishughulikia bara lao kuelekea mwisho wake na kulirudisha bara hilo kule lilikotoka yaani kabla ya wazungu hawajatia mguu barani humo kwa maana kwamba kutakuwa na mifumo ya ukabila zaidi, udikteta zaidi kuliko mifumo ya kidemokrasia na akamalizia kwa kusema kwamba hio ndo hali ambayo waafrika wanaridhika nayo.
Ninasikitika sana, kwa sababu nikiangalia habari zote zihusuzo ufisadi, rushwa na midubwana mingine nikabakia natafuta majibu.
Kwa wale walioko Marekani na Canada kitabu hicho kitachapishwa tarehe 12 April, Norway tarehe 20 May,Denmark tarehe 25 June, na Netherlands tarehe30 July 2009.
Last edited: