Mzee wa Upako: Ningekuwa Waziri Mkuu ningemshauri Rais uchaguzi 2020 aufute waliopo madarakani waendelee na nafasi zao

“Ningekuwa Waziri Mkuu, ningemshauri Rais Uchaguzi huu aufute kwa sababu ni gharama. Waliopo madarakani waendelee na nafasi zao, uchaguzi ufutwe ili kutoisumbua nchi."

Mch. Lusekelo (Mzee wa upako, Transformer)
Kanisa la Maombezi GRC

Note: Hawa ndio Wachungaji pendwa katika serikali hii. Mara nyingi huwa najiuliza waumini katika haya makanisa ya namna hii huwa wanataka kutendewa muujiza gani?

Ni Lusekelo huyu huyu ambaye aliwahi kuonekana hadharani akiwa amelewa chakari, lakini cha kushangaza waumini katika Kanisa lake wakamtetea kwa nguvu zote kuwa Mchungaji wao ni msafi kama pamba. Haikupita muda mrefu Mchungaji Anthony Lusekelo akakiri kwa kinywa chake kuwa yeye hanywi pombe kali kama konyagi na gongo lakini anakunywa Wine tu. Waumini hao hao waliomtetea awali kuwa hanywi pombe wakashangilia.

Ni Lusekelo huyu huyu ambaye aliwaambia waumini wa Kanisa lake kuwa kufa masikini ni ufala. Aisee! Yani waumini walewale masikini wanaomtajirisha yeye kupitia umasikini wake hadi anapata pesa ya kutembelea Land Cruiser VX na kununua Wine za kifahari ni mafala. Kwa kustaajabisha waumini hao hao wakamshangilia.

Tuna tatizo kubwa sana katika mind set za waumini haswa hawa wa haya makanisa ya watu binafsi. Lakini kuna tatizo kubwa sana katika mamlaka ya ku regulate na kusimamia haya makanisa.

Waumini wengi wanaibiwa, wanaporwa mali zao kwa mgongo wa kuamini MIUJIZA ambayo kimsingi haipo au ni feki ya kutengenezwa "fabricated and pre determined miracles". Wachungaji wengi kusema UKWELI MCHUNGU wana take advantage ya shida na umasikini wa waumini hawa kuwaibia na kujitajirisha.

Ndio maana kila kona mahubiri katika makanisa haya ni habari ya kupanda mbegu, kulanyaga mafuta ya upako, kunywa fruto ya upako, kunywa maji ya upako, kununua vitambaa, shuhuda za mtu aliyepata kazi ya uhandisi bila hata ya kuwa na elimu ya VETA, kupata kazi bila hata kufanya interview, kuuza mchicha usiozidi mtaji wa shilingi 5000 kisha ukapata faida kubwa kimiujiza baada ya kupanda mbegu ya shilingi 50,000 ukajenga nyumba ya ghorofa tatu na ukanunua gari la shilingi milioni 100 n.k.

Ni makanisa haya tunaona MIUJIZA feki ya kufufua watu, watu kunyweshwa jiki, mafuta ya taa na hata kuamriwa kuvua nguo za ndani ili waombewe wapate watoto na wachumba.

Ni katika makanisa haya tunaona Wachungaji wakitembea juu ya migongo ya waumini wao. Yani migongo ya waumini ndio imegeuka kuwa majukwaa. Hawakanyagi chini.

Chakusitikisha haya makanisa yanajaa waumini ambao kila uchwao wanadumbukia kwenye lindi la umasikini huku Wachungaji wao wakitumia umasikini wa waumini hawa kuwa mabilionea. Nani hakumbuki ulaghai, wizi na ujambazi uliofanywa na Wachungaji hawa katika sakata la kupanda mbegu la DECI? Waumini walilizwa mchana kweupe na ni mabilioni hayo ambayo juzi tumesikia tena Serikali badala iwarudishie waumini masikini waliolizwa fedha zao badala yake serikali nayo imetumia wizi huo kupora fedha hizo na kuzitaifisha eti zitapangiwa miradi ya maendeleo!

Ipo haja ya kuyapiga msasa haya makanisa na Wachungaji wake. Yasiyokidhi vigezo yafutiliwe mbali na Wachungaji wake wafutiwe leseni.

Remmy Cameroon
Sauti ya wasio na sauti

View attachment 1130222
Ni Ushauri binafsi ila
Binafsi naona unapingana na katiba.
 
Kwahio mchungaji katiba haina maana?halafu tusipofanya uchaguzi ili iweje?ushauri wako haina mashiko Baki nao
Sasa braza anko kavunja katiba kanuni na sheria mara ngap we unaonea huruma hii moja ya kuahirisha uchaguz
 
“Ningekuwa Waziri Mkuu, ningemshauri Rais Uchaguzi huu aufute kwa sababu ni gharama. Waliopo madarakani waendelee na nafasi zao, uchaguzi ufutwe ili kutoisumbua nchi."

Mch. Lusekelo (Mzee wa upako, Transformer)
Kanisa la Maombezi GRC

Note: Hawa ndio Wachungaji pendwa katika serikali hii. Mara nyingi huwa najiuliza waumini katika haya makanisa ya namna hii huwa wanataka kutendewa muujiza gani?

Ni Lusekelo huyu huyu ambaye aliwahi kuonekana hadharani akiwa amelewa chakari, lakini cha kushangaza waumini katika Kanisa lake wakamtetea kwa nguvu zote kuwa Mchungaji wao ni msafi kama pamba. Haikupita muda mrefu Mchungaji Anthony Lusekelo akakiri kwa kinywa chake kuwa yeye hanywi pombe kali kama konyagi na gongo lakini anakunywa Wine tu. Waumini hao hao waliomtetea awali kuwa hanywi pombe wakashangilia.

Ni Lusekelo huyu huyu ambaye aliwaambia waumini wa Kanisa lake kuwa kufa masikini ni ufala. Aisee! Yani waumini walewale masikini wanaomtajirisha yeye kupitia umasikini wake hadi anapata pesa ya kutembelea Land Cruiser VX na kununua Wine za kifahari ni mafala. Kwa kustaajabisha waumini hao hao wakamshangilia.

Tuna tatizo kubwa sana katika mind set za waumini haswa hawa wa haya makanisa ya watu binafsi. Lakini kuna tatizo kubwa sana katika mamlaka ya ku regulate na kusimamia haya makanisa.

Waumini wengi wanaibiwa, wanaporwa mali zao kwa mgongo wa kuamini MIUJIZA ambayo kimsingi haipo au ni feki ya kutengenezwa "fabricated and pre determined miracles". Wachungaji wengi kusema UKWELI MCHUNGU wana take advantage ya shida na umasikini wa waumini hawa kuwaibia na kujitajirisha.

Ndio maana kila kona mahubiri katika makanisa haya ni habari ya kupanda mbegu, kulanyaga mafuta ya upako, kunywa fruto ya upako, kunywa maji ya upako, kununua vitambaa, shuhuda za mtu aliyepata kazi ya uhandisi bila hata ya kuwa na elimu ya VETA, kupata kazi bila hata kufanya interview, kuuza mchicha usiozidi mtaji wa shilingi 5000 kisha ukapata faida kubwa kimiujiza baada ya kupanda mbegu ya shilingi 50,000 ukajenga nyumba ya ghorofa tatu na ukanunua gari la shilingi milioni 100 n.k.

Ni makanisa haya tunaona MIUJIZA feki ya kufufua watu, watu kunyweshwa jiki, mafuta ya taa na hata kuamriwa kuvua nguo za ndani ili waombewe wapate watoto na wachumba.

Ni katika makanisa haya tunaona Wachungaji wakitembea juu ya migongo ya waumini wao. Yani migongo ya waumini ndio imegeuka kuwa majukwaa. Hawakanyagi chini.

Chakusitikisha haya makanisa yanajaa waumini ambao kila uchwao wanadumbukia kwenye lindi la umasikini huku Wachungaji wao wakitumia umasikini wa waumini hawa kuwa mabilionea. Nani hakumbuki ulaghai, wizi na ujambazi uliofanywa na Wachungaji hawa katika sakata la kupanda mbegu la DECI? Waumini walilizwa mchana kweupe na ni mabilioni hayo ambayo juzi tumesikia tena Serikali badala iwarudishie waumini masikini waliolizwa fedha zao badala yake serikali nayo imetumia wizi huo kupora fedha hizo na kuzitaifisha eti zitapangiwa miradi ya maendeleo!

Ipo haja ya kuyapiga msasa haya makanisa na Wachungaji wake. Yasiyokidhi vigezo yafutiliwe mbali na Wachungaji wake wafutiwe leseni.

Remmy Cameroon
Sauti ya wasio na sauti

View attachment 1130222
Apambane na Hali yake
 
huko ni kuvunja katiba ya Nchi au anafkiri wa2 wanakaa tu madrakani kama yye n kanisa lake ilo..
 
Unaposema haya makanisa yapigwe msasa na kufutiwa unazani hapo watakao athirika ni hao wenye makanisa makubwa? Au?
 
“Ningekuwa Waziri Mkuu, ningemshauri Rais Uchaguzi huu aufute kwa sababu ni gharama. Waliopo madarakani waendelee na nafasi zao, uchaguzi ufutwe ili kutoisumbua nchi."

Mch. Lusekelo (Mzee wa upako, Transformer)
Kanisa la Maombezi GRC

Note: Hawa ndio Wachungaji pendwa katika serikali hii. Mara nyingi huwa najiuliza waumini katika haya makanisa ya namna hii huwa wanataka kutendewa muujiza gani?

Ni Lusekelo huyu huyu ambaye aliwahi kuonekana hadharani akiwa amelewa chakari, lakini cha kushangaza waumini katika Kanisa lake wakamtetea kwa nguvu zote kuwa Mchungaji wao ni msafi kama pamba. Haikupita muda mrefu Mchungaji Anthony Lusekelo akakiri kwa kinywa chake kuwa yeye hanywi pombe kali kama konyagi na gongo lakini anakunywa Wine tu. Waumini hao hao waliomtetea awali kuwa hanywi pombe wakashangilia.

Ni Lusekelo huyu huyu ambaye aliwaambia waumini wa Kanisa lake kuwa kufa masikini ni ufala. Aisee! Yani waumini walewale masikini wanaomtajirisha yeye kupitia umasikini wake hadi anapata pesa ya kutembelea Land Cruiser VX na kununua Wine za kifahari ni mafala. Kwa kustaajabisha waumini hao hao wakamshangilia.

Tuna tatizo kubwa sana katika mind set za waumini haswa hawa wa haya makanisa ya watu binafsi. Lakini kuna tatizo kubwa sana katika mamlaka ya ku regulate na kusimamia haya makanisa.

Waumini wengi wanaibiwa, wanaporwa mali zao kwa mgongo wa kuamini MIUJIZA ambayo kimsingi haipo au ni feki ya kutengenezwa "fabricated and pre determined miracles". Wachungaji wengi kusema UKWELI MCHUNGU wana take advantage ya shida na umasikini wa waumini hawa kuwaibia na kujitajirisha.

Ndio maana kila kona mahubiri katika makanisa haya ni habari ya kupanda mbegu, kulanyaga mafuta ya upako, kunywa fruto ya upako, kunywa maji ya upako, kununua vitambaa, shuhuda za mtu aliyepata kazi ya uhandisi bila hata ya kuwa na elimu ya VETA, kupata kazi bila hata kufanya interview, kuuza mchicha usiozidi mtaji wa shilingi 5000 kisha ukapata faida kubwa kimiujiza baada ya kupanda mbegu ya shilingi 50,000 ukajenga nyumba ya ghorofa tatu na ukanunua gari la shilingi milioni 100 n.k.

Ni makanisa haya tunaona MIUJIZA feki ya kufufua watu, watu kunyweshwa jiki, mafuta ya taa na hata kuamriwa kuvua nguo za ndani ili waombewe wapate watoto na wachumba.

Ni katika makanisa haya tunaona Wachungaji wakitembea juu ya migongo ya waumini wao. Yani migongo ya waumini ndio imegeuka kuwa majukwaa. Hawakanyagi chini.

Chakusitikisha haya makanisa yanajaa waumini ambao kila uchwao wanadumbukia kwenye lindi la umasikini huku Wachungaji wao wakitumia umasikini wa waumini hawa kuwa mabilionea. Nani hakumbuki ulaghai, wizi na ujambazi uliofanywa na Wachungaji hawa katika sakata la kupanda mbegu la DECI? Waumini walilizwa mchana kweupe na ni mabilioni hayo ambayo juzi tumesikia tena Serikali badala iwarudishie waumini masikini waliolizwa fedha zao badala yake serikali nayo imetumia wizi huo kupora fedha hizo na kuzitaifisha eti zitapangiwa miradi ya maendeleo!

Ipo haja ya kuyapiga msasa haya makanisa na Wachungaji wake. Yasiyokidhi vigezo yafutiliwe mbali na Wachungaji wake wafutiwe leseni.

Remmy Cameroon
Sauti ya wasio na sauti

View attachment 1130222
Huyu jamaa kazi yake inajulikana,
Hakuna dini hapo,
 
Wewe hata ukaze sauti vipi MAGUFULI NI HADI 2025.Sio kila vita lazima upanga, zingine ni kukaa kimya tu.Vita ya kumtoa Jpm 2020 ni kujipotezea muda
Mh nyinyi wa akili za hivyo mngekuweko kipndi cha kupigania uhuru hadi leo tungekua tunatawaliwa
 
Mh nyinyi wa akili za hivyo mngekuweko kipndi cha kupigania uhuru hadi leo tungekua tunatawaliwa
Kipindi cha kupigania UHURU na saiz ni vitu viwili tofauti. Kwani saiz mnapigania nini?
 
Kipindi cha kupigania UHURU na saiz ni vitu viwili tofauti. Kwani saiz mnapigania nini?
Uhuru wa kisiasa (kujiunga ktk vyama vya siasa)
Uhuru wa kukosoa
Uhuru wa kumchagua umtakae
Uhuru wa kupata habari
Uhuru wa,,,,,,,,,,,,,,,,,
 
Kwani sheria inasemaje?
Huyu mzee anayasoma maandiko na kuyaelewa vizuri?

Je huwa anapata muda wa kuyatafakali kabla ya kunena?

Mungu atuhurumie
 
Back
Top Bottom