Mzee wa Upako awatimua waandishi

gumegume

JF-Expert Member
Jun 29, 2011
1,063
617
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo jijini Dar es Salaam, Anthony Lusekelo maarufu 'Mzee wa Upako', jana aliwagomea waandishi wa habari kusikiliza hotuba yake ya Ibada ya Krismasi, na kutuma wasaidizi wake wawaondoe waandishi hao.

"Samahani tunaomba muondoke kwani Mchungaji amesema hataki kumuona mwandishi yeyote hapa, hivyo tunaomba muende Makanisa mengine", alisema msaidizi huyo na kuhakikisha waandishi wote wanaondoka eneo hilo majira ya saa sita kasoro mchana.

Lusekelo maarufu 'Mzee wa Upako' hivi karibuni amekuwa akirushiana maneno na baadhi ya waandishi wa habari, baada ya kuandikwa akituhumiwa kuwa mlevi na kutukana hadharani.

CHANZO: HABARI LEO, 26.12.2016.
 
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo jijini Dar es Salaam, Anthony Lusekelo maarufu 'Mzee wa Upako', jana aliwagomea waandishi wa habari kusikiliza hotuba yake ya Ibada ya Krismasi, na kutuma wasaidizi wake wawaondoe waandishi hao.

"Samahani tunaomba muondoke kwani Mchungaji amesema hataki kumuona mwandishi yeyote hapa, hivyo tunaomba muende Makanisa mengine", alisema msaidizi huyo na kuhakikisha waandishi wote wanaondoka eneo hilo majira ya saa sita kasoro mchana.

Lusekelo maarufu 'Mzee wa Upako' hivi karibuni amekuwa akirushiana maneno na baadhi ya waandishi wa habari, baada ya kuandikwa akituhumiwa kuwa mlevi na kutukana hadharani.

CHANZO: HABARI LEO, 26.12.2016.
Tuache kuandika na kutangaza habari zake, regardless awe analipia au halipii, hii in dharau kubwa.BTW yale magari aliyodai amepewa yamelipiwa kodi?
 
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo jijini Dar es Salaam, Anthony Lusekelo maarufu 'Mzee wa Upako', jana aliwagomea waandishi wa habari kusikiliza hotuba yake ya Ibada ya Krismasi, na kutuma wasaidizi wake wawaondoe waandishi hao.

"Samahani tunaomba muondoke kwani Mchungaji amesema hataki kumuona mwandishi yeyote hapa, hivyo tunaomba muende Makanisa mengine", alisema msaidizi huyo na kuhakikisha waandishi wote wanaondoka eneo hilo majira ya saa sita kasoro mchana.

Lusekelo maarufu 'Mzee wa Upako' hivi karibuni amekuwa akirushiana maneno na baadhi ya waandishi wa habari, baada ya kuandikwa akituhumiwa kuwa mlevi na kutukana hadharani.

CHANZO: HABARI LEO, 26.12.2016.
Hivi aya gani inayosema utenge adui yako kiasi hiki?? na uwe na chuki na wapinzani wako?? au siku hizi Biblia kuna new version??
 
Sasa mzee wa upako mbona anaweweseka?

Hao waandishi wanaomwandika vibaya alisema kuwa amepata maono kuwa Kabla ya mwezi March mwakani wote watakuwa weshakufa........

Akasisitiza kuwa kama 'unabii' wake usipotimia yeye ataacha kazi ya kumtumikia Mungu na ataenda kuuza gongo!

Sasa ni vyema mzee wa upako akatulia na wananchi wanausubiri kwa hamu mwezi wa 3 kuona kama ni waandishi wa Habari 'watakaopukutika' au ni mzee wa upako kwenda kuuza chang'aa!
 
Waandishi nao wakati mwingine wana Lugha za Maudhi.Lusekelokama binadamu naye ana damu na Nyama.
 
Hawakupaswa kujitambulisha kwa kazi zao!!
Wangesema wameleta "Fungu la kumi"
 
Mzee wa upako mbona unatumia nguvu kudili wahandishi wakati umeshawambia wasubili kitacho wakuta
 
Back
Top Bottom