Mzee wa Upako atokwa povu kutopewa nafasi kuiombea Dreamliner

Hashpower7113

JF-Expert Member
Sep 26, 2011
1,353
2,137
Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) Anthony Lusekelo maarufu kama Mzee wa Upako, amelalamika kubaguliwa katika mapokezi ya ndege mpya, Boeing 787-8 Dreamliner, ambapo wachungaji wengine walipewa nafasi ya kusema chochote na kuiombea ndege hiyo lakini yeye akabaguliwa.

Mzee wa Upako amejitapa kwamba mvua iliyonyesha siku hiyo, ilikuwa ni ufunuo wa Mungu kuonesha jinsi yeye alivyobarikiwa kwani eneo alilokaa yeye tu, ndiyo mvua haikufika na kusababisha viongozi wengine kukimbilia ili kukaa naye.

Akazidi kufunguka kwamba watu wanamu-ignore sana na wanasubiri siku atakapokufa ndiyo waje kutoa ushuhuda wa jinsi alivyokuwa na upako mtakatifu.
 
aende zake huko, si anasema anayemlaumu jiwe anachuki nae binafsi. Halaf Sio kila aombaye anaombea mema wengne wanaombea nuksi we unaishia kusema ASHINDWEE mwenzako anasema ASHINDEEE
 
Mzee wa Upako amejitapa kwamba mvua iliyonyesha siku hiyo, ilikuwa ni ufunuo wa Mungu kuonesha jinsi yeye alivyobarikiwa kwani eneo alilokaa yeye tu, ndiyo mvua haikufika na kusababisha viongozi wengine kukimbilia ili kukaa naye.

Akazidi kufunguka kwamba watu wanamu-ignore sana na wanasubiri siku atakapokufa ndiyo waje kutoa ushuhuda wa jinsi alivyokuwa na upako mtakatifu.


Huyu naye ameanza kufilisika mawazo, mvua ikinyesha ni adhabu kwa wanaoipata? kule kwao Mbeya na hasa Tukuyu, mvua ni nyingi sana je ile ni adhabu ya Mungu na pigo kwa wanatukuyu? Je na kama yeye angepewa nafasi kuiombea, ndege wale ambao wangekosa nafasi hiyo wakanung'unika angewaambiaje?
 
vipi wateja wamepungua kanisani kwake?? hadi leo bado sielewi inakuaje mtu mzima na akili zake anaibiwa kirahisi na hawa "manabii/wachungaji" kwa kuahidiwa "matumaini" !!!!
 
Back
Top Bottom