Mzee wa Mchemsho Ezekiel Maige umechanganyikiwa?

rosemarie

JF-Expert Member
Mar 22, 2011
6,887
3,412
KELELE anazopiga Mbunge wa Msalala, Ezekiel Magolyo Maige, zinanichefua. Analalamika kila uchao na kibaya zaidi anatumia vyombo vya habari.

Malalamiko yake yanasababishwa na kupokwa dhamana ya uwaziri wa Maliasili na Utalii aliyopewa kwa muda tu na Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Kikwete.
Anasema kilichomtoa kwenye nafasi hiyo ni majungu na fitina za kipumbavu zilizotengenezwa dhidi yake na makada wenzake wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwamo Rais Kikwete, ambaye ni mwenyekiti wa taifa wa chama hicho tawala.

Dakika za mwisho na punde baada ya uamuzi wa mwajiri wake kumfuta kazi ya uwaziri alinukuliwa akitamka maneno ya kiungwana yenye kutaka imani ya Watanzania juu yake na kuonyesha wazi kwamba husuda na chuki za wenzake zimetokana na ununuzi wa hekalu lake la dola 700,000 za Marekani.Ezekiel Maige anatamani kuenguliwa kwake kwenye nafasi hiyo kuwe ajenda ya taifa ndiyo maana anatumia mitandao ya kijamii, vyombo vya habari, watu mmoja mmoja, vikundi na hata wazee kwa kuwapa ‘mshiko' ili wamwamini na wakubali kwamba Rais Kikwete amemwonea.

Huyu mtu baada ya kutimuliwa kwenye uwaziri anarudi jimboni eti kuzungumza na aliowaita wazee na wapiga kura aliowapa cha kuwapa nao wanajifanya kumwonea huruma na kudiriki kusema watamuunga mkono kwa uamuzi wowote atakaochukua hata ikibidi kukihama chama kilichompa dhamana ya kukiwakilisha kwenye ubunge.

Hebu wajiulize enzi za uwaziri wake alikwenda mara ngapi jimboni kuzungumza na waliomchagua kuwa mbunge? Ni kweli Ezekiel Maige alikuwa anaketi nao kwenye vilabu vya pombe kama ilivyokuwa enzi za kampeni mwaka 2005?
Au kwa vile sasa hana gari lenye namba za W MU? Hatumii tena mafuta ya serikali, hataalikwa tena kwenye mikutano ya kimataifa kuiwakilisha nchi kama waziri? Akirudi bungeni atakaa kwenye viti vya nyuma na kuwa muuliza maswali si mtoa majibu? Nini kinamhangaisha Ezekiel Maige?

Hizi filamu za wasanii wa serikali ya awamu ya nne tulianza kuziona mwaka 2008 wakati aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, alipowajibika kwa hiyari baada ya watendaji wa chini yake kuboronga kwenye mkataba tata wa Kampuni ya kufua umeme kutoka Marekani ya Richmond.


Lowassa na mawaziri wenzake wawili waliwajibika. Wenye busara tuliwapongeza licha ya wao kuamua kutafuta faraja kama anavyofanya Maige ambaye mtindo anaoutumia unampambanua kuwa si mvumilivu.


Nawashauri wapiga kura wa Msalala wasikubali giriba wanazofanyiwa na mbunge wao wa sasa kwa sababu kufukuzwa kwake kwenye uwaziri kulitokana na uroho wa madaraka aliokuwa nao, kwa kuwa alishindwa kuwajibika kama watangulizi wake.


Nilizungumza na rafiki yangu akaniambia zamani watoto wa kiume waliokuwa wakipelekwa kufanyiwa tohara kikubwa walichousiwa huko ni uvumilivu, ndiyo maana walikuwa wakitahiriwa bila ganzi.


Hali hiyo ipo kwenye baadhi ya makabila hadi sasa.
"Tohara ya kienyeji ina maumivu sana ndiyo maana watoto wa kiume wakiwa jando kila siku wanaambiwa kuwa wavumilivu kwenye kila jambo watakalokutana nalo maishani… mtoto wa kiume ukimwambia siri lazima awe na kifua cha kuitunza. Huyo tunamwita jasiri," alisema rafiki huyo.Kwa maelezo hayo nimejiridhisha kwamba Ezekiel Maige si mvumilivu, hana ujasiri, tena ni mwoga aliyeamini kwamba uwaziri ni sehemu ya ngozi ya mwili wake, atakufa nao, ndiyo maana hakujiandaa kuondoka kwa wakati ule.

Ninalazimika kuamini kwamba Ezekiel Maige alikuwa na biashara inayoitwa ‘uwaziri', sasa amepata hasara kwa sababu biashara imefilisika kabla hajapata faida aliyoitegemea ndiyo maana anawayawaya, hana pa kushika, analia moyoni, machoni na hadharani, hataki kuamini.

Nawashauri wapiga kura wa Msalala mwaka 2015 wajiandae kumpata mbunge mwingine jasiri mwenye uvumilivu, atakayekuwa karibu yao muda wote, si wakati mgumu pekee kama anavyofanya Ezekiel Maige sasa.Naamini maumivu ya uwaziri yakipoa hatarudi tena jimboni hadi wakati wa kampeni, kwa hiyo kuweni makini naye, atakachowapa pokeeni, akili kichwani kwenye sanduku la kura, unachokifanya ni siri yako.

Ezekiel Maige anahitaji ushauri nasaha.

 
Ajutie madudu yake aliyoyafanya Maliasili mbona hayo hakuyasema kabla mpaka Mwenyekiti alipomuumbua hongera Mh Lembeli.
 
Mkuu this is very true and serious!Hana lolote mbona haya yote hakuyasema muda wote?, haya ni maumivu ya kuukosa uwaziri! Kama ametolewa kwenye uwaziri ya nini kwenda kulalama jimboni? Je wana jimbo lake walimchagua kuwa waziri au mbunge! Mimi nadhani hata wapigakura wake wangefurahi kuona kwamba mbunge wao kapunguziwa majukumu na kupata fursa ya kuwa karibu naye ili kulijenga jimbo kimaendeleo na siyo kutamka kwamba aseme lolote na sisi tuko tayari kumfuata!
 
umaarufu wote alioupata bado tu hajaridhika, haaaaa maige
 
serikali ichukue lile hekalu kabla hajalipiga bei kwa sababu amechanganyikiwa na hana amani nalo.
 
Hofu iko kwenye kupoteza hakalu la $700,000,lazima uchanganyikiwe,hell has broken loose nilijua tu siku yenu itafika hakuna dhambi nzuri,feel the pains of sufferer Tanzanians due to your selfishness.
 
Huyu mpuuzi hajui kazi yake ilimtaka nini, mbona KAGASHEKI kaweza kuukata mbuyu uliomshinda maige,huyu ni kibaraka wa mafisadi walimpa hongo akashindwa kutekeleza majukumu, kubwa jinga na CPA-T yake umewaangusha wahasibu kwa kushindwa ku-apply QT katika kufanya infomed decisions.kwishaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Analalama kama mwanamke aliyepewa talaka na kujisafisha mitaani kwa kumtangaza huyo mtalaka wake kuwa si chochote si lolote hali anaumia roho kwa kuachwa. Miage hukubatizwa kuwa waziri ulichoiba kinatosha, kwanza unastahili kwenda mahakamani kwa ufisadi ni kwa vile hii Takukuru yetu ni Taasisi ya kuendeleza na kuboresha rushwa
 
Huyu ni gamba kweli....hata demu akiachika halalamiki kiasi hiki....kwani alizaliwa kuwa waziri?
 
Kuna tetesi jamaa mpya aliyeingia maliasili hakuamini aliyoyakuta. Maana hajui hata aanzie wapi. Watu wanagawana taratibu taratibu tu
 
mimi simuonei huruma kabisa huyu MAIGE. lipi huyu anaweza kujivunia ameifanyia hiyo wizara achilia mbali jimbo lake. hata 2015 naomba aangukie pua!!!!! nitafurahi wewe.
 
alilewa madaraka akasahu kuna siku atayakosa na kuwa mtu wa kawaida,leo tungekuwa seriously huyu alipaswa apandishwe mahakamani
 
Maige awambie watanzania hicho anachokiita majungu, husuda na Chuki dhidi yake ni kipi katika ripoti ya mheshimiwa Lembeli?! aache ngonjera awe muwazi ataje jungu, husuda etc 1,2,3 ili watu wachambue, kwa sababu tuhuma ziko wazi, kama tuhuma yaTwiga kuuzwa kinyemela ni majungu kwa nini alimtimua kazi aliyekuwa mkurugenzi wa wanyama pori? Je usafirishaji wa magogo nchi za nje kinyume cha sheria ni majungu, kugawa vitalu vya uwindaji kinyume cha taratibu zilizowekwa ni majungu? ubadhirifu wa fedha TANAPA na Ngorongoro conservation ni majungu na husuda? Maige wacha kuwahadaa wanyantuzu wako, wambie ukweli hata mungu atakusaidia acha kuendeleza uongo wa kuisafisha dhambi.
 
KELELE anazopiga Mbunge wa Msalala, Ezekiel Magolyo Maige, zinanichefua. Analalamika kila uchao na kibaya zaidi anatumia vyombo vya habari.

Malalamiko yake yanasababishwa na kupokwa dhamana ya uwaziri wa Maliasili na Utalii aliyopewa kwa muda tu na Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Kikwete.
Anasema kilichomtoa kwenye nafasi hiyo ni majungu na fitina za kipumbavu zilizotengenezwa dhidi yake na makada wenzake wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwamo Rais Kikwete, ambaye ni mwenyekiti wa taifa wa chama hicho tawala.

Dakika za mwisho na punde baada ya uamuzi wa mwajiri wake kumfuta kazi ya uwaziri alinukuliwa akitamka maneno ya kiungwana yenye kutaka imani ya Watanzania juu yake na kuonyesha wazi kwamba husuda na chuki za wenzake zimetokana na ununuzi wa hekalu lake la dola 700,000 za Marekani.Ezekiel Maige anatamani kuenguliwa kwake kwenye nafasi hiyo kuwe ajenda ya taifa ndiyo maana anatumia mitandao ya kijamii, vyombo vya habari, watu mmoja mmoja, vikundi na hata wazee kwa kuwapa ‘mshiko’ ili wamwamini na wakubali kwamba Rais Kikwete amemwonea.

Huyu mtu baada ya kutimuliwa kwenye uwaziri anarudi jimboni eti kuzungumza na aliowaita wazee na wapiga kura aliowapa cha kuwapa nao wanajifanya kumwonea huruma na kudiriki kusema watamuunga mkono kwa uamuzi wowote atakaochukua hata ikibidi kukihama chama kilichompa dhamana ya kukiwakilisha kwenye ubunge.

Hebu wajiulize enzi za uwaziri wake alikwenda mara ngapi jimboni kuzungumza na waliomchagua kuwa mbunge? Ni kweli Ezekiel Maige alikuwa anaketi nao kwenye vilabu vya pombe kama ilivyokuwa enzi za kampeni mwaka 2005?
Au kwa vile sasa hana gari lenye namba za W MU? Hatumii tena mafuta ya serikali, hataalikwa tena kwenye mikutano ya kimataifa kuiwakilisha nchi kama waziri? Akirudi bungeni atakaa kwenye viti vya nyuma na kuwa muuliza maswali si mtoa majibu? Nini kinamhangaisha Ezekiel Maige?

Hizi filamu za wasanii wa serikali ya awamu ya nne tulianza kuziona mwaka 2008 wakati aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, alipowajibika kwa hiyari baada ya watendaji wa chini yake kuboronga kwenye mkataba tata wa Kampuni ya kufua umeme kutoka Marekani ya Richmond.


Lowassa na mawaziri wenzake wawili waliwajibika. Wenye busara tuliwapongeza licha ya wao kuamua kutafuta faraja kama anavyofanya Maige ambaye mtindo anaoutumia unampambanua kuwa si mvumilivu.


Nawashauri wapiga kura wa Msalala wasikubali giriba wanazofanyiwa na mbunge wao wa sasa kwa sababu kufukuzwa kwake kwenye uwaziri kulitokana na uroho wa madaraka aliokuwa nao, kwa kuwa alishindwa kuwajibika kama watangulizi wake.


Nilizungumza na rafiki yangu akaniambia zamani watoto wa kiume waliokuwa wakipelekwa kufanyiwa tohara kikubwa walichousiwa huko ni uvumilivu, ndiyo maana walikuwa wakitahiriwa bila ganzi.


Hali hiyo ipo kwenye baadhi ya makabila hadi sasa.
“Tohara ya kienyeji ina maumivu sana ndiyo maana watoto wa kiume wakiwa jando kila siku wanaambiwa kuwa wavumilivu kwenye kila jambo watakalokutana nalo maishani… mtoto wa kiume ukimwambia siri lazima awe na kifua cha kuitunza. Huyo tunamwita jasiri,” alisema rafiki huyo.Kwa maelezo hayo nimejiridhisha kwamba Ezekiel Maige si mvumilivu, hana ujasiri, tena ni mwoga aliyeamini kwamba uwaziri ni sehemu ya ngozi ya mwili wake, atakufa nao, ndiyo maana hakujiandaa kuondoka kwa wakati ule.

Ninalazimika kuamini kwamba Ezekiel Maige alikuwa na biashara inayoitwa ‘uwaziri’, sasa amepata hasara kwa sababu biashara imefilisika kabla hajapata faida aliyoitegemea ndiyo maana anawayawaya, hana pa kushika, analia moyoni, machoni na hadharani, hataki kuamini.

Nawashauri wapiga kura wa Msalala mwaka 2015 wajiandae kumpata mbunge mwingine jasiri mwenye uvumilivu, atakayekuwa karibu yao muda wote, si wakati mgumu pekee kama anavyofanya Ezekiel Maige sasa.Naamini maumivu ya uwaziri yakipoa hatarudi tena jimboni hadi wakati wa kampeni, kwa hiyo kuweni makini naye, atakachowapa pokeeni, akili kichwani kwenye sanduku la kura, unachokifanya ni siri yako.

Ezekiel Maige anahitaji ushauri nasaha.

Kama alidhani UWAZIRI NIG*VI SASA KATAHIRIWA. ATULIE APONE NA AWE MWANAUMME WA KIUKWELI!!! WAJINGA SANA WATU WA NAMNA YAKE WANADHSNI HIZI NAFASI ZA KUWATUMIKIA WANANCHI NI UFALME...HADI AFE NDIO ANACHUKUA MWINGINE
 
Ndugu yangu atawafundisha wahasibu wetu namna bora na nzuri ya kuiba.Huyo hata kufundisha hatakiwi kabisa.Kwanza inabidi kuishauri Bodi ya Wahasibu kuwa wahasibu wote wanaokutwa na Ufisadi na wezi wa mali ya umma wanyanganywe certificates zao za CPA maana hawafai kuitwa wahasibu wanatuaibisha.Namuomba Maige atuombe radhi wahasibu ametutia aibu kubwa.
 
Anadhalilisha vijana kiasi kwamba wataonekana hawana uvumilivu hivyo kwakuwa amechanganyikiwa serikali imzindue kwa kumpandisha kizimbani
 
Unamnyanganya Simba nyama mdomoni?Unategemea nini?Huyo jamaa alikuwa akilamba mpaka dola laki tano kutoa kibali cha kitalu kimoja tu cha kuwindia!!Amechanganyikiwa alitegemea amalize na uwaziri huo awe billionea na hata kugombea Urais!Lakini mipango yake yote imeharibika?OOOOhh nimeonewa!nimefitiniwa"?yeye anafikirii vyombo vya dola vimelala?
Analamba madola ya vitalu akajisahau !!!Kila la kheri Maige!Get well soon!kwa maumivu ya kuukosa uwaziri!
 
Da nyuzi imetulia ila heading ya mchemsho kumbe ni kuchemka mi nikafikiri ile michemsho ya mbuzi maige aliyovimbishia shavu. Analalamika wkt b*kir* keshatolewa. Umeharibu kaa kimya msifie JK anaweza kukupa ukuu wa mkoa sasa umelikoroga ubunge utapigwa chini labda ugombee ujumbe wa nyumba kumi.
 
Kupewa dhamana ya kukodisha vitalu vya uwindaji sio mchezo mazee, kuna dili za mabilioni pale. Hizo $ 700,000 za hekalu ndogo saana.
 
Back
Top Bottom