rosemarie
JF-Expert Member
- Mar 22, 2011
- 6,887
- 3,412
KELELE anazopiga Mbunge wa Msalala, Ezekiel Magolyo Maige, zinanichefua. Analalamika kila uchao na kibaya zaidi anatumia vyombo vya habari.
Malalamiko yake yanasababishwa na kupokwa dhamana ya uwaziri wa Maliasili na Utalii aliyopewa kwa muda tu na Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Kikwete.Anasema kilichomtoa kwenye nafasi hiyo ni majungu na fitina za kipumbavu zilizotengenezwa dhidi yake na makada wenzake wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwamo Rais Kikwete, ambaye ni mwenyekiti wa taifa wa chama hicho tawala.
Dakika za mwisho na punde baada ya uamuzi wa mwajiri wake kumfuta kazi ya uwaziri alinukuliwa akitamka maneno ya kiungwana yenye kutaka imani ya Watanzania juu yake na kuonyesha wazi kwamba husuda na chuki za wenzake zimetokana na ununuzi wa hekalu lake la dola 700,000 za Marekani.Ezekiel Maige anatamani kuenguliwa kwake kwenye nafasi hiyo kuwe ajenda ya taifa ndiyo maana anatumia mitandao ya kijamii, vyombo vya habari, watu mmoja mmoja, vikundi na hata wazee kwa kuwapa ‘mshiko' ili wamwamini na wakubali kwamba Rais Kikwete amemwonea.
Huyu mtu baada ya kutimuliwa kwenye uwaziri anarudi jimboni eti kuzungumza na aliowaita wazee na wapiga kura aliowapa cha kuwapa nao wanajifanya kumwonea huruma na kudiriki kusema watamuunga mkono kwa uamuzi wowote atakaochukua hata ikibidi kukihama chama kilichompa dhamana ya kukiwakilisha kwenye ubunge.
Hebu wajiulize enzi za uwaziri wake alikwenda mara ngapi jimboni kuzungumza na waliomchagua kuwa mbunge? Ni kweli Ezekiel Maige alikuwa anaketi nao kwenye vilabu vya pombe kama ilivyokuwa enzi za kampeni mwaka 2005?Au kwa vile sasa hana gari lenye namba za W MU? Hatumii tena mafuta ya serikali, hataalikwa tena kwenye mikutano ya kimataifa kuiwakilisha nchi kama waziri? Akirudi bungeni atakaa kwenye viti vya nyuma na kuwa muuliza maswali si mtoa majibu? Nini kinamhangaisha Ezekiel Maige?
Hizi filamu za wasanii wa serikali ya awamu ya nne tulianza kuziona mwaka 2008 wakati aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, alipowajibika kwa hiyari baada ya watendaji wa chini yake kuboronga kwenye mkataba tata wa Kampuni ya kufua umeme kutoka Marekani ya Richmond.
Lowassa na mawaziri wenzake wawili waliwajibika. Wenye busara tuliwapongeza licha ya wao kuamua kutafuta faraja kama anavyofanya Maige ambaye mtindo anaoutumia unampambanua kuwa si mvumilivu.
Nawashauri wapiga kura wa Msalala wasikubali giriba wanazofanyiwa na mbunge wao wa sasa kwa sababu kufukuzwa kwake kwenye uwaziri kulitokana na uroho wa madaraka aliokuwa nao, kwa kuwa alishindwa kuwajibika kama watangulizi wake.
Nilizungumza na rafiki yangu akaniambia zamani watoto wa kiume waliokuwa wakipelekwa kufanyiwa tohara kikubwa walichousiwa huko ni uvumilivu, ndiyo maana walikuwa wakitahiriwa bila ganzi.
Hali hiyo ipo kwenye baadhi ya makabila hadi sasa."Tohara ya kienyeji ina maumivu sana ndiyo maana watoto wa kiume wakiwa jando kila siku wanaambiwa kuwa wavumilivu kwenye kila jambo watakalokutana nalo maishani… mtoto wa kiume ukimwambia siri lazima awe na kifua cha kuitunza. Huyo tunamwita jasiri," alisema rafiki huyo.Kwa maelezo hayo nimejiridhisha kwamba Ezekiel Maige si mvumilivu, hana ujasiri, tena ni mwoga aliyeamini kwamba uwaziri ni sehemu ya ngozi ya mwili wake, atakufa nao, ndiyo maana hakujiandaa kuondoka kwa wakati ule.
Ninalazimika kuamini kwamba Ezekiel Maige alikuwa na biashara inayoitwa ‘uwaziri', sasa amepata hasara kwa sababu biashara imefilisika kabla hajapata faida aliyoitegemea ndiyo maana anawayawaya, hana pa kushika, analia moyoni, machoni na hadharani, hataki kuamini.
Nawashauri wapiga kura wa Msalala mwaka 2015 wajiandae kumpata mbunge mwingine jasiri mwenye uvumilivu, atakayekuwa karibu yao muda wote, si wakati mgumu pekee kama anavyofanya Ezekiel Maige sasa.Naamini maumivu ya uwaziri yakipoa hatarudi tena jimboni hadi wakati wa kampeni, kwa hiyo kuweni makini naye, atakachowapa pokeeni, akili kichwani kwenye sanduku la kura, unachokifanya ni siri yako.
Ezekiel Maige anahitaji ushauri nasaha.
Malalamiko yake yanasababishwa na kupokwa dhamana ya uwaziri wa Maliasili na Utalii aliyopewa kwa muda tu na Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Kikwete.Anasema kilichomtoa kwenye nafasi hiyo ni majungu na fitina za kipumbavu zilizotengenezwa dhidi yake na makada wenzake wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwamo Rais Kikwete, ambaye ni mwenyekiti wa taifa wa chama hicho tawala.
Dakika za mwisho na punde baada ya uamuzi wa mwajiri wake kumfuta kazi ya uwaziri alinukuliwa akitamka maneno ya kiungwana yenye kutaka imani ya Watanzania juu yake na kuonyesha wazi kwamba husuda na chuki za wenzake zimetokana na ununuzi wa hekalu lake la dola 700,000 za Marekani.Ezekiel Maige anatamani kuenguliwa kwake kwenye nafasi hiyo kuwe ajenda ya taifa ndiyo maana anatumia mitandao ya kijamii, vyombo vya habari, watu mmoja mmoja, vikundi na hata wazee kwa kuwapa ‘mshiko' ili wamwamini na wakubali kwamba Rais Kikwete amemwonea.
Huyu mtu baada ya kutimuliwa kwenye uwaziri anarudi jimboni eti kuzungumza na aliowaita wazee na wapiga kura aliowapa cha kuwapa nao wanajifanya kumwonea huruma na kudiriki kusema watamuunga mkono kwa uamuzi wowote atakaochukua hata ikibidi kukihama chama kilichompa dhamana ya kukiwakilisha kwenye ubunge.
Hebu wajiulize enzi za uwaziri wake alikwenda mara ngapi jimboni kuzungumza na waliomchagua kuwa mbunge? Ni kweli Ezekiel Maige alikuwa anaketi nao kwenye vilabu vya pombe kama ilivyokuwa enzi za kampeni mwaka 2005?Au kwa vile sasa hana gari lenye namba za W MU? Hatumii tena mafuta ya serikali, hataalikwa tena kwenye mikutano ya kimataifa kuiwakilisha nchi kama waziri? Akirudi bungeni atakaa kwenye viti vya nyuma na kuwa muuliza maswali si mtoa majibu? Nini kinamhangaisha Ezekiel Maige?
Hizi filamu za wasanii wa serikali ya awamu ya nne tulianza kuziona mwaka 2008 wakati aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, alipowajibika kwa hiyari baada ya watendaji wa chini yake kuboronga kwenye mkataba tata wa Kampuni ya kufua umeme kutoka Marekani ya Richmond.
Lowassa na mawaziri wenzake wawili waliwajibika. Wenye busara tuliwapongeza licha ya wao kuamua kutafuta faraja kama anavyofanya Maige ambaye mtindo anaoutumia unampambanua kuwa si mvumilivu.
Nawashauri wapiga kura wa Msalala wasikubali giriba wanazofanyiwa na mbunge wao wa sasa kwa sababu kufukuzwa kwake kwenye uwaziri kulitokana na uroho wa madaraka aliokuwa nao, kwa kuwa alishindwa kuwajibika kama watangulizi wake.
Nilizungumza na rafiki yangu akaniambia zamani watoto wa kiume waliokuwa wakipelekwa kufanyiwa tohara kikubwa walichousiwa huko ni uvumilivu, ndiyo maana walikuwa wakitahiriwa bila ganzi.
Hali hiyo ipo kwenye baadhi ya makabila hadi sasa."Tohara ya kienyeji ina maumivu sana ndiyo maana watoto wa kiume wakiwa jando kila siku wanaambiwa kuwa wavumilivu kwenye kila jambo watakalokutana nalo maishani… mtoto wa kiume ukimwambia siri lazima awe na kifua cha kuitunza. Huyo tunamwita jasiri," alisema rafiki huyo.Kwa maelezo hayo nimejiridhisha kwamba Ezekiel Maige si mvumilivu, hana ujasiri, tena ni mwoga aliyeamini kwamba uwaziri ni sehemu ya ngozi ya mwili wake, atakufa nao, ndiyo maana hakujiandaa kuondoka kwa wakati ule.
Ninalazimika kuamini kwamba Ezekiel Maige alikuwa na biashara inayoitwa ‘uwaziri', sasa amepata hasara kwa sababu biashara imefilisika kabla hajapata faida aliyoitegemea ndiyo maana anawayawaya, hana pa kushika, analia moyoni, machoni na hadharani, hataki kuamini.
Nawashauri wapiga kura wa Msalala mwaka 2015 wajiandae kumpata mbunge mwingine jasiri mwenye uvumilivu, atakayekuwa karibu yao muda wote, si wakati mgumu pekee kama anavyofanya Ezekiel Maige sasa.Naamini maumivu ya uwaziri yakipoa hatarudi tena jimboni hadi wakati wa kampeni, kwa hiyo kuweni makini naye, atakachowapa pokeeni, akili kichwani kwenye sanduku la kura, unachokifanya ni siri yako.
Ezekiel Maige anahitaji ushauri nasaha.