Leak
JF-Expert Member
- Feb 22, 2012
- 52,206
- 42,068
Salaam wana jamvi.
Toka muziki wa singeli umeanza kuwaingia vichwani na masikioni Watanzania, kumekuwa na ujio tofauti tofauti wa wasanii wa singeli lakini ni ukweli ulio wazi Msaga Sumu alikaa kileleni muda mrefu sana na ndiye masanii aliyeweka chachu sana kwenye muziki wa singeli na kuutangaza.
Lakini miaka ya hivi karibuni muziki wa singeli kama ilivyo Bongo Fleva umekuwa ukizalisha vipaji vingi kama wakina Man Fongo, Dullah Makabila, Mzee wa Bwax na wengine wengi.
Na muziki huu umekuwa ukileta changa moto kubwa sana kwa wasanii wa Bongo Fleva, hasa stejini na kucheza na mashabiki.
Mzee wa Bwax ameongeza chachu sana hasa jinsi ya kucheza na mashabiki stejini tofauti na wasanii wengine wa singeli na ukweli ni kwamba wasanii wa singeli hawahitaji kuwalazimisha mashabiki kushangilia au kupiga kelele bali mashabiki hulipuka na kujikuta kama vichaa vile.
Mzee wa Bwax ni mmoja ya wasanii nchini wenye nguvu kubwa na uwezo sana wawapo stejini na ninadiriki kusema ni msanii namba moja wa singeli kwa sasa.
Wasanii wa Bongo Fleva wanapata wakati mgumu sana wanapokutana na wasanii wa singeli stejini; ni wazi wanalo la kujifunza, hasa jinsi ya kucheza na mashabiki.
Bado najiuliza ni msanii gani wa Bongo Fleva anaweza pambana na mzee wa Bwax stejini.
Je, muziki wa Bongo Fleva umepata upinzani kamili stejini?
Wasalaam
Toka muziki wa singeli umeanza kuwaingia vichwani na masikioni Watanzania, kumekuwa na ujio tofauti tofauti wa wasanii wa singeli lakini ni ukweli ulio wazi Msaga Sumu alikaa kileleni muda mrefu sana na ndiye masanii aliyeweka chachu sana kwenye muziki wa singeli na kuutangaza.
Lakini miaka ya hivi karibuni muziki wa singeli kama ilivyo Bongo Fleva umekuwa ukizalisha vipaji vingi kama wakina Man Fongo, Dullah Makabila, Mzee wa Bwax na wengine wengi.
Na muziki huu umekuwa ukileta changa moto kubwa sana kwa wasanii wa Bongo Fleva, hasa stejini na kucheza na mashabiki.
Mzee wa Bwax ni mmoja ya wasanii nchini wenye nguvu kubwa na uwezo sana wawapo stejini na ninadiriki kusema ni msanii namba moja wa singeli kwa sasa.
Wasanii wa Bongo Fleva wanapata wakati mgumu sana wanapokutana na wasanii wa singeli stejini; ni wazi wanalo la kujifunza, hasa jinsi ya kucheza na mashabiki.
Bado najiuliza ni msanii gani wa Bongo Fleva anaweza pambana na mzee wa Bwax stejini.
Je, muziki wa Bongo Fleva umepata upinzani kamili stejini?
Wasalaam