- Thread starter
- #41
Muache kudanganya wananchi kwamba mabeberu ndio wanawatia njaa.Shida wengi hamuelewi ubeberu ni nini labda hadi muelezwe maana ya ubeberu kwa kingereza. Ubeberu maana yake kwa kingereza ni 'imperialism'. Mataifa makubwa ya ulaya ya magharibi hasa uingereza ufaransa na ubeljiji ni imperialists. Walitawala nchi zingine na wanaendelea kuzitawala kiuchumi. Ubeberu sio tusi. Haohao wanaotupa misaada ndio pia mabeberu. Mabeberu ni pamoja na marekani. Inatawala dunia kiuchumi na wanafanya kila hila kudhibiti uchumi wa dunia.
Nyie mnaowapenda wazungu hadi kupata kichefuchefu tukiwaita mabeberu mnashangaza. Hata wao hawaoni ni ajabu kuwaita mabeberu na hapohapo tukipokea misaada kutoka kwao.