Idugunde
JF-Expert Member
- May 21, 2020
- 6,273
- 6,637
Huyu mzee ni muuza kahawa maarufu jijini Dar es salam na anasema historia ya nchi nii ipo kiganjani kwake. Anasema watu wanaomuita Bernad Membe eti ni kachero mbobezi hawajui historia ya Tanzania kwa undani. Maana kama ni ukachero Membe hawezi fikia hata robo ya ya umahiri wa Mrema.
Mzee anasema Mrema yupo vizuri na anajua kila kitu kuhusu uzandiki na mbinu zote za kikachero. Mzee Shomari anasisitiza kuwa Mrema kumuunga mkono Magufuli wa CCM ni sababu anajua namna Magufuli anachukia ufisadi kama yeye Mrema alivyo.
Bernad Membe anayo historia gani ya kuchukia ufisadi? Maana akifunuliwa hapo alipo ananukia ufisadi. Lakini Mrema alikuwa Dso kahama miaka ya nyuma kila mtu alimuogopa. Pia alikuwa waziri wa mambo ya ndani alipambana na ufisadi kama anavyofanya JPM. Alipokuwa waziri wa mambo ya ndani alikuwa halali kwake kuhakikisha mafisadi wanakamatwa.
Ni kashfa nzito ambazo zilihusu ufisadi zilisababishwa akafukuzwa CCM. Sasa safari hii ameona CCM ina kiongozi anayepinga ufisadi kama yeye ndio maana amemuunga mkono 100%.
Mzee Shomari ameninog'oneza kuwa Membe sio kachero mbobezi kama Lyatonga Mrema bali ni mjanjamjanja tu. Na wanaompaisha hawaijui hii Tanzania vizuri. Maana Mrema alikuwa akiongea majambazi wanasalimisha bunduki wenyewe. Ila ameshauri Chadema na Act wamtumie Membe kama mgombea wao ili kufuta aibu!
Mzee anasema Mrema yupo vizuri na anajua kila kitu kuhusu uzandiki na mbinu zote za kikachero. Mzee Shomari anasisitiza kuwa Mrema kumuunga mkono Magufuli wa CCM ni sababu anajua namna Magufuli anachukia ufisadi kama yeye Mrema alivyo.
Bernad Membe anayo historia gani ya kuchukia ufisadi? Maana akifunuliwa hapo alipo ananukia ufisadi. Lakini Mrema alikuwa Dso kahama miaka ya nyuma kila mtu alimuogopa. Pia alikuwa waziri wa mambo ya ndani alipambana na ufisadi kama anavyofanya JPM. Alipokuwa waziri wa mambo ya ndani alikuwa halali kwake kuhakikisha mafisadi wanakamatwa.
Ni kashfa nzito ambazo zilihusu ufisadi zilisababishwa akafukuzwa CCM. Sasa safari hii ameona CCM ina kiongozi anayepinga ufisadi kama yeye ndio maana amemuunga mkono 100%.
Mzee Shomari ameninog'oneza kuwa Membe sio kachero mbobezi kama Lyatonga Mrema bali ni mjanjamjanja tu. Na wanaompaisha hawaijui hii Tanzania vizuri. Maana Mrema alikuwa akiongea majambazi wanasalimisha bunduki wenyewe. Ila ameshauri Chadema na Act wamtumie Membe kama mgombea wao ili kufuta aibu!