Mzee Pinda kafungua rasmi kampeni za uchaguzi?

MKEHA

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
714
1,137
Nimemsikiliza Waziri Mkuu Mstaafu ndugu Kayanza Peter Pinda wakati akitoa salamu kwenye hafla ya kupokea ndege yetu.

Amesema Kanda ya Ziwa ina idadi kubwa sana ya watu ambao ni kama asilimia 20 hivi ya watu wote wa Tanzania.

Akatoa wito wakimchagua Rais kwa wingi wao kwingineko itakuwa ni kujazia jazia tu.

Wajuzi wa mambo sijui kama kampeni zimeruhusiwa kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwakani.

Au Mzee Pinda kajisahau kidogo. Je sheria za nchi zinaruhusu kampeni kuanza mapema kiasi hiki?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usiwe Na Hofu Wala Wasi Wasi Hao Ndiyo Walivyo Na Huu Ndiyo Muda Wao. Unadhani Angesemaje Kipindi Hiki
Chama Dola!!!
Uwe Mvumilivu Mpaka Watakapomaliza
 
Mzee Pinda ni muungwana na mtu makini sana, huenda hakuwa na nia mbaya kabisa. Japo akiwa kwenye hisia huwa na historia ya kuongea kauli tata sana ambazo huleta taharuki.

Watanzania walivyo na kisirani siku hizi, hii kauli inaweza tafsiriwa vibaya sana na itachambuliwa vilivyo huko mitandaoni hata kama alizungumza kwa nia njema tu. Imefika wakati hata tukiongea utani kuhusu kabila, jamii fulani au dini lazima itokee taharuki tu. Yaani tunaenda ndiko siko kama Taifa ambalo mwanzo lilikuwa na bashasha kubwa na kuvumiliana.

Binafsi siku hizi huwa najiepusha sana kuzungumzia kabila au kanda yoyote ile, iwe kwa mazuri, utani au nia njema. Watanzania wamekuwa na kisirani sana kwenye mambo madogo kama haya. Sijui chanzo kikuu ni nini lakini naamini siasa ni mojawapo.

Wanasiasa wetu wajifunze kuchunga sana kauli zao wakiwa wanazungumza na jamii ya watu wenye hasira na kisirani kama Tanzania ya sasa.

Jamani Amani Itawale Tanzania,
Tuiombee na kuipenda sana nchi yetu.
 
Nimemsikiliza waziri mkuu mstaafu ndugu Kayanza Peter Pinda wakati akitoa salam kwenye hafla ya kupokea ndege yetu .

Amesema kanda ya ziwa ina idadi kubwa sana ya watu ambao ni kama asilimia 20 hivi ya watu wote wa Tanzania.
Akatoa wito wakimchagua rais kwa wingi wao kwingineko itakuwa ni kujazia jazia tu.
Wajuzi wa mambo sijui kama kampeni zimeruhusiwa kwa ajiri ya uchaguzi mkuu wa mwakani.
Au Pinda kajisahau kodogo. Je sheria za nchi zinaruhusu kampeni kuanza mapema kiasi hiki.

Sent using Jamii Forums mobile app

Katika mambo yote aliyozungumza na yanayotokea huko Mwanza muda huu kwako hilo ndilo umeliona la maana!!!????
 
Katika mambo yote aliyozungumza na yanayotokea huko Mwanza muda huu kwako hilo ndilo umeliona la maana!!!????

Yeye hilo kwake ndio la maana, ww ungeweka hayo unayoona ni ya maana. Wali hata uwe mzuri na mtamu vipi, ukishakuwa na mawe haulipi.
 
Bwabwa tu Hilo ukilibana Sana linamwaga chozi
Nimemsikiliza waziri mkuu mstaafu ndugu Kayanza Peter Pinda wakati akitoa salam kwenye hafla ya kupokea ndege yetu .

Amesema kanda ya ziwa ina idadi kubwa sana ya watu ambao ni kama asilimia 20 hivi ya watu wote wa Tanzania.
Akatoa wito wakimchagua rais kwa wingi wao kwingineko itakuwa ni kujazia jazia tu.
Wajuzi wa mambo sijui kama kampeni zimeruhusiwa kwa ajiri ya uchaguzi mkuu wa mwakani.
Au Pinda kajisahau kodogo. Je sheria za nchi zinaruhusu kampeni kuanza mapema kiasi hiki.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jiwe awe makini sana na pinda anamchomesha!!!Pengo anahusika!!maana anamsapoti jiwe kuhusu ajenda ya ukanda!!!Kamati kuu watamchinjia baharini ngoja waendelee kukusanya evidence!!!!
 
Nimemsikiliza waziri mkuu mstaafu ndugu Kayanza Peter Pinda wakati akitoa salam kwenye hafla ya kupokea ndege yetu .

Amesema kanda ya ziwa ina idadi kubwa sana ya watu ambao ni kama asilimia 20 hivi ya watu wote wa Tanzania.
Akatoa wito wakimchagua rais kwa wingi wao kwingineko itakuwa ni kujazia jazia tu.
Wajuzi wa mambo sijui kama kampeni zimeruhusiwa kwa ajiri ya uchaguzi mkuu wa mwakani.
Au Pinda kajisahau kodogo. Je sheria za nchi zinaruhusu kampeni kuanza mapema kiasi hiki.

Sent using Jamii Forums mobile app
Vipi wale wanaoandika andika humu kuhusu Membe 2020!?
 
Pinda ndio zake hata safari iliyopita alianza mapema kabisa tena alianzia kule BBC
Lakini tulipita nae. Hizi mbwembwe ziache mwisho sisi ndio tutaamua
 
Mzee Pinda ni muungwana na mtu makini sana, huenda hakuwa na nia mbaya kabisa. Japo akiwa kwenye hisia huwa na historia ya kuongea kauli tata sana ambazo huleta taharuki.

Watanzania walivyo na kisirani siku hizi, hii kauli inaweza tafsiriwa vibaya sana na itachambuliwa vilivyo huko mitandaoni hata kama alizungumza kwa nia njema tu. Imefika wakati hata tukiongea utani kuhusu kabila, jamii fulani au dini lazima itokee taharuki tu. Yaani tunaenda ndiko siko kama Taifa ambalo mwanzo lilikuwa na bashasha kubwa na kuvumiliana.

Binafsi siku hizi huwa najiepusha sana kuzungumzia kabila au kanda yoyote ile, iwe kwa mazuri, utani au nia njema. Watanzania wamekuwa na kisirani sana kwenye mambo madogo kama haya. Sijui chanzo kikuu ni nini lakini naamini siasa ni mojawapo.

Wanasiasa wetu wajifunze kuchunga sana kauli zao wakiwa wanazungumza na jamii ya watu wenye hasira na kisirani kama Tanzania ya sasa.

Jamani Amani Itawale Tanzania,
Tuiombee na kuipenda sana nchi yetu.

..kizazi kilichopita kilikuwa na utani wa kufurahisha na kuchekeshana.

..pia ili utani uwe utani lazima kuwe na mazingira yenye upendo, kuaminiana, na umoja.

..lingine ni kwamba uwezo wetu wa kuwasiliana / communication skills ni wa kiwango cha chini kiasi kwamba inawezekana wahusika wanajaribu kutania lakini wanaishia kukashifu.

..nimewahi kumsikia mtu mmoja mkubwa ktk tukio la kuapisha watendaji mbalimbali Ikulu akimwambia aliyeteuliwa kuwa, "...tena wewe walikuwa wanakushangaa ni Mchagga gani asiyependa rushwa, hela..."

..sasa kauli kama hiyo ni utani au unyanyapaa?

..Utani tuliouzoea siyo ule wa kujenga picha mbaya dhidi ya makabila ya wenzetu, bali ni utani wa kuwafanya wenzetu wacheke na kufurahi.
 
Nimemsikiliza Waziri Mkuu Mstaafu ndugu Kayanza Peter Pinda wakati akitoa salamu kwenye hafla ya kupokea ndege yetu.

Amesema Kanda ya Ziwa ina idadi kubwa sana ya watu ambao ni kama asilimia 20 hivi ya watu wote wa Tanzania.

Akatoa wito wakimchagua Rais kwa wingi wao kwingineko itakuwa ni kujazia jazia tu.

Wajuzi wa mambo sijui kama kampeni zimeruhusiwa kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa mwakani.

Au Mzee Pinda kajisahau kidogo. Je sheria za nchi zinaruhusu kampeni kuanza mapema kiasi hiki?

Sent using Jamii Forums mobile app

Msajili wa vyama chukua hatua, vinginevyo jiuzulu.
 
Back
Top Bottom