Mzee Mwinyi: Robert Mugabe aliisaidia Tanzania wakati wa shida, ni rafiki wa kwanza wa Tanzania

Anasahau kuwa wakati huo Mugabe alikua anatumia pesa za Mabeberu wakiokua wamemkabidhi Nchi . Wakati huo Mugabe alikua na muda wa miaka 4 tu madarakani ,na uchumi wa Zimbabwe ulikua imara sana na haikua ni Juhudi zake Huyo Hayati Mugabe kujenga uchumi wa Zimbabwe.
Mugabe Aliikuta Zimbabwe ikiwa na uchumi Mzuri sana ,akawa anachota mapesa na kufanya mambo ya Hovyo mpaka Leo ameiacha nchi hiyo ikiwa na pesa yenye samani sawa karatasi za kuchorea kama sio pampers.

Hata hivyo tunamshukuru kwa jambo hilo zuri kwa nchi yetu japo sisi tulitoa wapiganaji wetu kwa ajili ya kuikomboa nchi hiyo na wakapoteza maisha yao ambayo yanathamani kubwa kuliko kitu chochote.
Acha kupotosha Mkuu.

Hata watu wa Magharibi wenyewe wanakiri kuwa Mugabe baada ya kuingia madarakani miaka 17 ya mwanzo "alileta" (sio aliendeleza) maendeleo na alifanya mambo makubwa sana hasa kwa Watu weusi ambao ndio walikuwa wengi (majority).

Hao ndugu zako wa Magharibi wanakiri kabisa kuwa Mugabe aliifanya Zimbabwe kuwa nchi yenye wasomi wengi kuliko nchi yoyote ya Afrika, hadi Waafrika na nchi nyingine zisizo za Kiafrika wakawa wanaitamani Zimbabwe.

Mugabe pia alisaidia sana raia wake hasa katika ya Sekta ya Afya. Haya yote yapo kwenye vyombo vya habari vya Magharibi kama BBC na vinginevyo. Kasome kabla haujaja kupotosha.

Mugabe amekuja "kuonekana" mzinguaji baada ya kuingilia Maslahi ya Wazungu, hasa Waingereza kwenye miaka ya 2000.

Pia alikuja kuharibu kung'ang'ania madarakani baada ya kushindwa mwaka 2008.

Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni.
 
Huyu huyu Mugabe mpenda sifa aisaidie Tanzania miaka yote hii asijigambe hadharani!? 😳😳😳😳

Alitusaidia kitu gani!? 😳😳😳

Huyu Mzee aache kuropoka ropoka.

View attachment 1202823
Rais mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi amesema kuwa alipoingia madarakani mwaka 1985, ailikuta hazina ya Tanzania ikiwa haina kitu

Hali hiyo ya ukata ilitokana na Tanzania kutumia fedha nyingi wakati wa vita vya Kagera(Tanzania dhidi ya Uganda) na IFM kuisusia Tanzania baada ya Mwalimu Nyerere kukataa masharti yao

Mwinyi asema aliamua kumfuata Mwalimu Nyerere akamuuliza, afanye nini? Nyerere akamwambia Tanzania ina marafiki kadhaa, ikiwemo nchi ya Zimbabwe na India, nenda kaombe msaada

Hayati Robert Mugabe akawa kiongozi wa kwanza kuisaidia Tanzania
 
Kwahiyo mzee Mwinyi alikuta hazina iko empty?

Ama kwa hakika ufisadi ulianza kitambo.....kwani Mtei alistaafu lini pale BoT?!!

..Mtei alishaondoka BOT mwaka 1974.

..Nafasi yake ilichukuliwa na Charles Nyirabu a ndiye aliyekuwa gavana wa BOT wakati Mzee Mwinyi anaingia madarakani.

..pia Mtei alishajiulizulu Uwaziri wa Fedha, na nadhani nafasi yake ilichukuliwa na Amir Jamal, na baadae Prof.Kighoma Ali Malima.

..Tafuta kitabu alichoandika Mzee Mtei kuhusu maisha na utumishi wake. Kuna mengi ya kujifunza ktk kitabu hicho. Na naamini Mzee Mtei alitumikia kwa uadilifu.

..Miaka ya zamani, kabla mataga na uv-ccm hawajavamia JF Mzee Mtei alikuwa akichangia mada zetu mbalimbali.


Cc Pascal Mayalla, Nguruvi3
 
Nina uhakika kwa asilimia mia kuwa Mugabe hakuwahi kuisaidia Tanzania hata senti tano. Mugabe kama Mugabe hakuwa na uwezo wowote wa kifedha kusaidia Tanzania. Mzee Mwinyi samahani sana, usidhalilishe taifa letu. Mtu hawezi kuisaidia nchi. Yeye kuidhinisha kutoa msaada wowote ni nchi imetoa na siyo mtu (Mugabe) katia mfukoni make, la hasha.

Hata USAID wanakuandikia kabisa ni msaada wa watu wa Marekani, lakini umeshindwa kuelewa hilo Mzee wangu? Pole sana mzee, mimi nakupinga japo sijawahi kuwa rais wa nchi. Tumia lugha stahiki, angalau basi sema serikali ya Zimbabwe iliamua kutusaidia, lakini siyo mtu aliyetusaidia. Mtu ananufaika na nchi, kamwe hawezi kuisaidia nchi. Na akipata mamlaka hufanya kwa niaba ya nchi na wananchi wote.
pengine hiyo inatokana na kuwa head of the state ndio mwenye kauli ya mwisho, anaweza kusema ndio au hapana.
 
Uko sahihi kimantiki lakini sio kiuhalisia, kwa hizi katiba zetu rais ndiyo mwenye maamuzi ya kutoa pesa hazina bila ruhusa ya yoyote na asifanywe lolote. Rejea manunuzi ya ndege hapa nchini, je yaliidhinishwa na bunge? Huoni siku hizi hapa kwetu rais anatoa pesa kwenye miradi mbalimbali na inatajwa kuwa yeye ndio katoa, na kuna kejeli fulani kwamba huo mradi kama sio yeye mbona watangulizi wake hawakufanya?
Ni bahati mbaya sana kwa nchi yetu kama bado wapo binadamu wanaofikiri kuwa rais au kiongozi yeyote anazo pesa anazoweza kutoa kama yeye kutekeleza wajibu wake.

Rais akitaka kutambulika inampasa aanzishe taasisi yake binafsi au atoe yeye binafsi kutoka kwenye mshahara wake kama anavyochangia harusi au anapotoa sadaka. Mengine yote, hata akifanya ni nchi imefanya na yeye ametekeleza wajibu wake kusimamia hilo alilofanya lifanyike. Na zaidi ya hapo, analipwa mshahara mnono kwa kazi hiyo.
 
Marehemu Mzee Nyrerere alikuwa na akili sana. Hata Mwinyi licha ya kuwa rais alishindwa cha kufanya mpaka karudi kwa Nyerere kuomba ushauri na akashauriwa vyema kabisa.
 
Kuna watu wanadai eti tulisaidiwa na Zimbabwe na siyo Mugabe- Hiyo Zimbabwe ilikuwa inajiendesha yenyewe?, Mugabe angekataa kutoa hizo fedha kutusaidia hiyo Zimbabwe ingetusaidiaje?

Mambo ya nchi huwa yapo kwenye dhamana ya mkuu wa nchi!
Tunaposema Nyerere kakomboa nchi nying za Afrika kiufupi huwa tunamaanisha kilekile kuwa Tanzania imesaidia kukomboa nchi nyingi za Afrika.
 
Nina uhakika kwa asilimia mia kuwa Mugabe hakuwahi kuisaidia Tanzania hata senti tano. Mugabe kama Mugabe hakuwa na uwezo wowote wa kifedha kusaidia Tanzania. Mzee Mwinyi samahani sana, usidhalilishe taifa letu. Mtu hawezi kuisaidia nchi. Yeye kuidhinisha kutoa msaada wowote ni nchi imetoa na siyo mtu (Mugabe) katia mfukoni make, la hasha.

Hata USAID wanakuandikia kabisa ni msaada wa watu wa Marekani, lakini umeshindwa kuelewa hilo Mzee wangu? Pole sana mzee, mimi nakupinga japo sijawahi kuwa rais wa nchi. Tumia lugha stahiki, angalau basi sema serikali ya Zimbabwe iliamua kutusaidia, lakini siyo mtu aliyetusaidia. Mtu ananufaika na nchi, kamwe hawezi kuisaidia nchi. Na akipata mamlaka hufanya kwa niaba ya nchi na wananchi wote.
Marais wa African states ni executive presidents, marais watendaji, ndio wenye maamuzi ya mwisho, hivyo Mwinyi is right aliyetusaidia ni Mugabe hata kama ni kwa fedha za Wazimbabwe, all the credits goes to the top. Hata katika vita, Tanzania tulipigana na nchi ya Uganda, lakini tuliposhinda, hatusemi tumewapiga Waganda, tumempiga Amini, hata Uganda iliposaidiwa na Libya tulisema Ghadafi amemsaidia Amini.

Hata sasa kwenye credits or failures tunamtaja mtu na sio nchi, Awamu ya Nyerere alifanya hiki na kile, kama ilivyo sasa kwa Magufuli, tuko kwenye Tanzania ya Magufuli kama tunavyoishi kwenye Darisalamu ya Makonda.

RIP Comredi Robert Mugabe, rafiki wa kweli wa taifa hili la Tanzania.
P
 
Huyu huyu Mugabe mpenda sifa aisaidie Tanzania miaka yote hii asijigambe hadharani!?

Alitusaidia kitu gani!?

Huyu Mzee aache kuropoka ropoka.
Mkuu haukuwepo wakati tunakula Ugali wa Yanga?
 
Kumbe uomba omba haukuwa bahati mbaya ni maagizo!

Makubwa haya.
Maisha yanaenda kasi sana..kwahiyomwe bibi siku hizi mpinzani...mh kweli siku zote teknoloji na mda haudawahi danganya

RIP comrade MUGABE true son of Africa
 
Hivi nini kinawatuma wakae kumtetea yule mzee dikteta? Kwa kua kafa basi mabaya yote aliyofanya yamefutika? Jamaa alikua kalio moja kubwa sana africa, kaiharibu sana Zimbabwe yeye na familia yake. Hakuna lolote akalale vibaya ovyo kabisa
 
Marais wa African states ni executive presidents, marais watendaji, ndio wenye maamuzi ya mwisho, hivyo Mwinyi is right aliyetusaidia ni Mugabe hata kama ni kwa fedha za Wazimbabwe, all the credits goes to the top. Hata katika vita, Tanzania tulipigana na nchi ya Uganda, lakini tuliposhinda, hatusemi tumewapiga Waganda, tumempiga Amini, hata Uganda iliposaidiwa na Libya tulisema Ghadafi amemsaidia Amini.

Hata sasa kwenye credits or failures tunamtaja mtu na sio nchi, Awamu ya Nyerere alifanya hiki na kile, kama ilivyo sasa kwa Magufuli, tuko kwenye Tanzania ya Magufuli kama tunavyoishi kwenye Darisalamu ya Makonda.

RIP Comredi Robert Mugabe, rafiki wa kweli wa taifa hili la Tanzania.
P
Nakuelewa sana P, lakini with due respect, mimi siyo muumini wa mtu anayetumia kodi yangu kula, kusafiria, kujilinda binafsi, nk, kisha atumie hiyo hiyo kodi kupeleka msaada mahali aseme ni yeye katoa.
I TOTALLY DISAGREE WITH SUCH KIND OF THINKING
 
Nakuelewa sana P, lakini with due respect, mimi siyo muumini wa mtu anayetumia kodi yangu kula, kusafiria, kujilinda binafsi, nk, kisha atumie hiyo hiyo kodi kupeleka msaada mahali aseme ni yeye katoa.
I TOTALLY DISAGREE WITH SUCH KIND OF THINKING
Naunga mkono hoja yako na msimamo wako, everybody has the right of his/her opinions, hivyo naheshimu msimamo wako, wakati mimi niliendelea kukubali Tanzania ya sasa ni Tanzania ya Magufuli ninaishi kwenye jiji la Darisalamu ambayo ni Jiji la Makonda au Darisalamu ya Makonda, baada ya kupita kwa ile Darisalamu ya Kandoro, na Daisaaamu ya Mgoshi wa Kaya ndugu yetu Makamba.
P
 
Back
Top Bottom