Jile79
JF-Expert Member
- May 28, 2009
- 17,668
- 13,236
Wazee ni busara lkn uzee wa hivi ni hasara kubwa sn kwa taifa....Mpuuzi kiwango cha lami
Wazee ni busara lkn uzee wa hivi ni hasara kubwa sn kwa taifa....Mpuuzi kiwango cha lami
word!Mtu yeyote anayetaka kuonekana kuwa anayosema yanatija kwa watu ni lazima arejee waliosema wenzake kule nyuma.
Mwalimu Nyrere alisema nini kuhusu wale wanaohonga ili kwenda Ukulu.
"Mimi nimekaa Ikula kwa miaka 25, Ikulu ni matatizo tu, wale mnaohonga ili mwende Ikulu, Ikulu kuna biashara gani? Ikulu siyo pango la walanguzi"
Kiongozi maarufu na Rais Mstaafu unasema umpe asante Rais ya kumwongezea miaka 5 ya utawala Inchi ni kituko kikubwa.
Tusishangae sana kwa sababu Nyerere alisema, Ukiona kiongozi anafanya maamuzi Fulani mazito kuhusu Inchi halafu siku inayofuata anarudi ofisini na maamuzi tofauti, huyu kiongozi hafai.
Aliema hatutaki kiongozi ambaye anaongoza Inchi kwa ushauri wa mke wake.
Rais wetu aliyeko madarakani amefanya mambo mengi sana mazuri. Amejitoa muhanga na kujijengea maadui wengi mafisadi kwa ajili yetu. Siku zote anasema , niombeeni kwa Mungu.
Kama kuendelea kukaa madarakani muda mrefu kuna maslahi kwa kiongozi basi Yesu Kristo angekaa hata miaka 20 lakini alifanya kazi ya unabii miaka 3 na akaondoka.
Rais wetu akidhubutu kubadilisha Katiba, itatutesa baadaye kwa sababu atakayekuja kama ni mbaya hatataka kupunguza muda wa uongozi toka miaka 15 kurudi 10.
Rais wetu akitaka jina lake litukuke, aondoka wakati watu bado wanamtaka.
Yesu Kristo alikuwa anatenda kwa kunena lakini aliondoka mapema.