johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,915
- 141,873
Rais mstaafu mzee Mkapa amesoma salamu za rambirambi kutoka kwa Rais Magufuli katika msiba wa Mzee Moi.
Mzee Mkapa amesema yeye binafsi amefanya kazi na Mzee Moi kwa miaka 7, akiwa na Rais na mzee Kikwete aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje.
Mkapa amesema Rais Magufuli amewatuma wao wawili kama ishara ya upendo na ushirikiano wa kindugu kati ya nchi zetu mbili.
=======
Akitoa salamu hizo, Mzee Mkapa amesema:
“Rais wangu Dkt. John Joseph Magufuli, kwa dhati kabisa ametuleta sisi wawili (na Mzee Kikwete) kuthibitisha ukaribu, undungu na umoja uliopo kati ya nchi zetu mbili”
“Nimekuwa Rais kwa miaka 10. Katika miaka hiyo 10, miaka 7 nilikuwa nafanya kazi na Rais Moi. Kwahivyo, kama alivyosema Dkt. Ruto, pamoja na kwamba ni mzee wetu, lakini kwangu mimi alikuwa ‘mentor’ katika utawala na uongozi. Ndiyo sababu nilisema lazima nije na ku-pay tribute kwa uhusiano huu niliokuwa nao, lakini vilevile kushirikiana nanyi katika kumuombea apumzike mahali pema peponi, kwa Mungu wetu ambaye alimpenda sana”
Mzee Mkapa pia ameambatana na Rais wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete ambaye ameeleza kumfahamu Mzee Moi tangu yeye (Kikwete) akiwa shule akisoma.
“Nimemfahamu Mzee Moi tangu nikiwa shule, nikisoma habari za Kenya, harakati za kudai uhuru wa Kenya. Baadaye na mimi nilipokuwa katika Serikali, nikiwa Waziri, niliwahi kuja. Nilitumwa na Rais wangu, Rais Ali Hassan Mwinyi nikiwa Waziri wa Nishati na Madini, kuja kuzungumza naye juu ya ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya katika mradi tuliokuwa tumefikiria kuuanza wa kujenga bomba la gesi kutoka Songosongo kuja Dar es Salaam”
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benjamin W. Mkapa akiwasilisha salamu za rambirambi kwa Wakenya, kwa niaba ya Rais John Magufuli.
Rais wa Nne wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete akitoa salamu zake kwa Wakenya kufuatia kifo cha Mzee Moi. Kikwete ameeleza mchango mkubwa wa Mzee Moi katika kuimarisha umoja wa wana Afrika Mashariki.
Source: Citizen TV
Mzee Mkapa amesema yeye binafsi amefanya kazi na Mzee Moi kwa miaka 7, akiwa na Rais na mzee Kikwete aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje.
Mkapa amesema Rais Magufuli amewatuma wao wawili kama ishara ya upendo na ushirikiano wa kindugu kati ya nchi zetu mbili.
=======
Akitoa salamu hizo, Mzee Mkapa amesema:
“Rais wangu Dkt. John Joseph Magufuli, kwa dhati kabisa ametuleta sisi wawili (na Mzee Kikwete) kuthibitisha ukaribu, undungu na umoja uliopo kati ya nchi zetu mbili”
“Nimekuwa Rais kwa miaka 10. Katika miaka hiyo 10, miaka 7 nilikuwa nafanya kazi na Rais Moi. Kwahivyo, kama alivyosema Dkt. Ruto, pamoja na kwamba ni mzee wetu, lakini kwangu mimi alikuwa ‘mentor’ katika utawala na uongozi. Ndiyo sababu nilisema lazima nije na ku-pay tribute kwa uhusiano huu niliokuwa nao, lakini vilevile kushirikiana nanyi katika kumuombea apumzike mahali pema peponi, kwa Mungu wetu ambaye alimpenda sana”
Mzee Mkapa pia ameambatana na Rais wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Kikwete ambaye ameeleza kumfahamu Mzee Moi tangu yeye (Kikwete) akiwa shule akisoma.
“Nimemfahamu Mzee Moi tangu nikiwa shule, nikisoma habari za Kenya, harakati za kudai uhuru wa Kenya. Baadaye na mimi nilipokuwa katika Serikali, nikiwa Waziri, niliwahi kuja. Nilitumwa na Rais wangu, Rais Ali Hassan Mwinyi nikiwa Waziri wa Nishati na Madini, kuja kuzungumza naye juu ya ushirikiano kati ya Tanzania na Kenya katika mradi tuliokuwa tumefikiria kuuanza wa kujenga bomba la gesi kutoka Songosongo kuja Dar es Salaam”
Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benjamin W. Mkapa akiwasilisha salamu za rambirambi kwa Wakenya, kwa niaba ya Rais John Magufuli.
Rais wa Nne wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete akitoa salamu zake kwa Wakenya kufuatia kifo cha Mzee Moi. Kikwete ameeleza mchango mkubwa wa Mzee Moi katika kuimarisha umoja wa wana Afrika Mashariki.
Source: Citizen TV