Mzee Mandela hakuwa anaamini ile dhana inayosema kuchapiwa ni siri ya ndani?

Huo ni mtazamo wako,hivi unaweza kumlinganisha Mandela na yule mchonga pua,kwa plastic surgery,kwa ajili ya kuutafuta uzungu kwa nguvu,Michael Jackson?!

Kama Mandela hakuwa maarufu,ni kwa nini basi hivi sasa,vyombo vya habari hivi sasa vinabashiri kuwa,mazishi yake yanaelekea ndiyo yatakayovunja record,kwa kuhudhuriwa na watu webfoot maarufu,yakiyazidi hata yale ya Pope John Paul wa pili na yale ya Churchil,mazishi ambayo,ndiyo yanasemekana kuwa ndiyo mazishi yaliyohudhuriwa na watu wengi zaidi,kuliko mazishi ya binadamu mwingine yeyote katika karne iliyopita ya 20 na karne tunayoendelea nayo ya 21.

Mimi sikusema kuwa Mandela hakuwa maarufu, anao umaarufu wake lakini si maarufu namba moja duniani, kumbuka hilo.

Mchonga pua hakuna asiyemjuwa duniani. Mpaka leo anashika chati.

Source:Most Famous Person 2013 Awards
 
Nimetembelea list zote za watu mashuhuri duniani nilizoweza kuzipata kwenye mtandao sijaona kuwa Mandela ndiye binaadam maarufu duniani. Hajashika namba moja kwenye list yoyote ile.

Nimeona list moja ametajwa Michael Jackson. List nyingine Sir Isaac Newton. Nyingine Marilyn Monroe. Mandela hayumo katika namba moja.

Kwanini uzuwe?
FaizaFoxy wazungu kamwe hawawezi kumwandika Mandela kuwa ndiye binadamu maarufu duniani na hata muandishi hajasema kuwa Mandela ndiye binadamu maarufu duniani bali amesema Mandela ni mtu anayeaminika kuwa, ndiye binadamu maarufu kuliko yeyote katika watu wote walioishi karne hizi za 20 na 21. lakini pia msije mkadhani kwamba wazungu walikuwa wanampenda Mandela bali ni wanafiki tu......
 
Mkuu Madiba angeishi Tanzania, asikaa apate heshima hiyo kwani alikuwa mdhaifu sna kwa wanawake!!!! Binnti yake kwa mkewa kwanza hadi sasa ana mlaani sana kwa kitendo cha kumwacha mama yao...ilhali nie aliempa Mandela hela za kusomea digrii ya sheria kwa miaka mitatu!! Mtoto wa Madiba anasema aliambiwa na mama yake kuwa baba yake alimwacha kwakuwa anapemda sana mademu wazuri..alimwona yeye (mke wa kwanza) kazeeka!! Ingekuwa TZ..aah!! angeshikishwa adabu na wana CCM...abao wako bize na ku link matatizo ya ndoa za viongozi na uwezo wao wa kungoza!!

Katika gazeti la mwananchi la tar.8/12 ukisoma ile habari ya MANDELA NA FAMILIA,imeandikwa kuwa mke wa kwanza aliachana na Mandela kwa kuwa yeye(mke) alikuwa ni "SHAHIDI WA YEHOVA",na kwamba mashahidi wa Yehova hawaoani na wanasiasa...vipi, tuamini kauli yako mkuu?
 
Ndugu yangu Mystery swala la Winnie Mandela kuachika halikuwa ni uzinzi pekee ingawa hii inaweza ikawa ndiyo sababu kubwa, lakini pia zilikuwepo sababu nyingi zikiwemo tuhuma za mauaji yaliyokuw ayakiendeshwa na timu yake ya Mandela Footbal Club zilizoibuliwa katika tume ya Maridhiano iliyoundwa na Mandela mwenyewe, hata hivyo tuhuma hizi mandela alikuwa anazifahamu kabla ya kutoka gerezani lakini hata baada ya kutoka gerezani na kukomeshwa kwa siasa za ubaguzi na Mzee Mandela kushinda nafasi ya Uraisi lakini bado Winnie alikuwa anaishi maisha ambayo yalikuwa yanamdhalilisha Mzee Mandela .....................

Rejea uzi nwangu huu hapa chini kuhusu tuhuma hizo:

https://www.jamiiforums.com/mahusia...mandela-na-tuhuma-za-mauaji-ya-kutisha-3.html
 
Last edited by a moderator:
FaizaFoxy wazungu kamwe hawawezi kumwandika Mandela kuwa ndiye binadamu maarufu duniani na hata muandishi hajasema kuwa Mandela ndiye binadamu maarufu duniani bali amesema Mandela ni mtu anayeaminika kuwa, ndiye binadamu maarufu kuliko yeyote katika watu wote walioishi karne hizi za 20 na 21. lakini pia msije mkadhani kwamba wazungu walikuwa wanampenda Mandela bali ni wanafiki tu......

Ni kweli kabisa. Aliwafunza adabu kwa kuto ku give up japonwalimfunga 27 years akatoka na akawa rais wa kwanza mweusi na kuwaashibu kisaikolojia zaidi akawasamehe na wengine akawapa nafasi katika serikali yake.
 
Hata hivyo, lipo eneo moja tu, ambalo mzee Mandela alishindwa kusamehe, na eneo hilo si lingine bali ni lile, alipopata ushahidi wa kutosha kuwa, wakati anatumikia kifungo jela, na hata baada ya kutoka jela, mkewe Winnie, alikuwa "akichapwa" na mwanasheria wao wa familia, jambo ambalo hatimaye, lilimlazimisha mzee wetu huyo, anayeheshimika sana duniani kwa uvumilivu wake, wa mambo makubwa yaliyomkumba maishani mwake, kutoweza kulivumilia hilo, hadi kusababisaha, kumpa talaka mkewe Winnie na kumwoa, mjane wa Samora Matchel, bi Graca Matchel!

Winnie Mandela alikuwa mke kicheche. Inasemekana kuna wakati alikuwa 'caught with her pants down' akimegwa. Ni mwanaume gani anayejielewa ambaye angeweza kuvumilia ukicheche wa namna hiyo?

Okay, wakati Nelson akiwa lupango, kwa shingo upande, mtu unaweza kuelewa na labda hata kumsamehe mwanamke kama huyo. Lakini hata baada ya kutoka jela mwanamama bado tu akawa anaendelea kumegwa na nje na lawyer wake.

Nijuavyo mimi hakuna mwanaume wa maana awezaye kuvumilia dharau na udhalilishwaji wa namna hiyo.

Hebu ona hiki kipande cha makala kilichoandikwa kwenye gazeti la The Independent, la Uingereza.

You might have thought the obstacles she faced would stop her. Take, for example, the publication in the Johannesburg Sunday Times in September 1992 of a letter she had written to her lover six months earlier.

The letter was dated 17 March 1992 and addressed to Dali Mpofu, one of her lawyers in the trial in which she was convicted of the assault and kidnapping of 14-year-old 'Stompie' Moeketsi Seipei and three others.

Mpofu was also her deputy in the ANC's welfare department. The letter confirmed long-standing suspicions both about their affair and the whereabouts of missing ANC funds.

Mrs Mandela, who was 56 at the time, accused Mpofu, who was 30, of having affairs with other women. 'You're running around ----ing at the slightest emotional excuse,' she wrote.

'The fact that I haven't been speaking to Tata (Nelson Mandela) for five months now over you is no longer your concern. I keep telling you the situation is deteriorating at home, you are not bothered because you are satisfying yourself every night with a woman. I won't be your bloody fool, Dali.'
Source

Sasa hebu ona huo upuuzi wake. Ni nani mwenye akili timamu anayeweza kuvumilia uchafu kama huo? Pengine wapo wanaoweza, lakini Nelson hakuweza. Hata ingekuwa mimi nisingeweza. Tena naona Nelson ni mvumilivu sana. Ingekuwa mimi ningekuwa nishampiga chini zamani mno.

Sasa hapo ndipo ninajiuliza, hivi mzee Mandela, hakuwa anaiamini falsafa ya mwanumuziki Richi Maboko, kuwa kuchapiwa ni siri ya ndani, ambapo wana ndoa, wanapaswa kuyamaliza wenyewe ndani, badala ya kuyatoa nje, na kuwapa faida walimwengu, ambao hayawahusu mambo hayo?!!

Hiyo ni falsafa ya kijinga kabisa. Mwanaume mzima na gonads zako uvumilie ujinga kama huo kisa unaogopa kuwapa faida walimwengu? Hapana aisee. Na potelea mbali kama walimwengu watafaidika au la, mimi nakumwaga at the initial suspicion.
 
FaizaFoxy wazungu kamwe hawawezi kumwandika Mandela kuwa ndiye binadamu maarufu duniani na hata muandishi hajasema kuwa Mandela ndiye binadamu maarufu duniani bali amesema Mandela ni mtu anayeaminika kuwa, ndiye binadamu maarufu kuliko yeyote katika watu wote walioishi karne hizi za 20 na 21. lakini pia msije mkadhani kwamba wazungu walikuwa wanampenda Mandela bali ni wanafiki tu......

Kumbuka kuwa umaarufu alionao Mandela umejengwa na hao hao wazungu kwa maslahi yao.

Kuna watu hawajawahi kumsikia kabisa, lakini waulize Michael Jackson, hata Watindiga wanamjuwa.

Unajuwa kuwa kuna watu Tanzania hii hata Kiswahili hawakijui lakini Michael Jackson wanamjuwa?
 
neno kuchapiwa siri ya ndani

soma andika yasisikukute mkuu ina mwenyewe hili
 
sababu ya winnie kupigwa talaka 3 ni kwamba alikua anamnyima unyumba mzee mandela baaada ya kutoka gerezani,kila akiombwa kutimiza haki hiyo ya msingi ya ndoa alikua haishi kutoa udhuru,mzee akaona ya kazi gani
 
Haha!
Hivi ile ya Mugabe kuchapiwa na Waziri wake, Imeishia wapi?
Mugabe ubabe wake unaishia kwa mahasimu wake wa kisiasa akina Tsangirai,lakini kwa huyo mkewe,former PS wake,hathubutu kumpa talaka,hata akimkuta red handed, anachapwa,kwa kuwa huyo mzee "amezimia" kwa huyo former PS wake,kiasi ambacho hakohoi wala hafurukuti!!
 
falsafa haiwezi kutumika ikiwa kila mtu anafahamu na dharau inaonyeshwa...
 
Hiyo ni ngumu aiseee wala haiwezekani.
Itabidi mods mumtafute huyo jamaa, kwa namba ya simu aliyoweka kwenye post yake, ili awalipe fee ya advertisement, kwa kuwa kama shamba lake, keshaliuza kwa shilingi milioni 5 kwa bei aliyoitangaza humu jamvini, basi angalau nyiye mods mlambe 10 percent ambayo ni laki 5.

Kwa kuwa humu JF, wanaotangaza biashara zao, kama vile akina voda bombastic, najua wanawalipa fee ya matangazo.
 
Hata Mungu yoote anasamehe ila inapotokea umechapiwa anaruhusu utoe talaka.......

..., Maandiko yap yanayokuruhusu ww kutoa talaka? Coz hata Mzee Mandela hapo amepotoka kwa kufuata zaid hisia zake badala ya kutumia Maandko/sheria zlzomfanya amuoe huyo Mtalaka wake!
 
Mimi sikusema kuwa Mandela hakuwa maarufu, anao umaarufu wake lakini si maarufu namba moja duniani, kumbuka hilo.

Mchonga pua hakuna asiyemjuwa duniani. Mpaka leo anashika chati.

Source:Most Famous Person 2013 Awards

wewe dada ni fulu komedi, wanguzu wakikuambia ww ni mwanaume unakubali.....! lol, kwa akili zako unaamini mtu kama Helle Berry au Tiger Woods, ni maariufu kuliko mandela?
 
Katika gazeti la mwananchi la tar.8/12 ukisoma ile habari ya MANDELA NA FAMILIA,imeandikwa kuwa mke wa kwanza aliachana na Mandela kwa kuwa yeye(mke) alikuwa ni "SHAHIDI WA YEHOVA",na kwamba mashahidi wa Yehova hawaoani na wanasiasa...vipi, tuamini kauli yako mkuu?

Mkuu name mie nilisoma maandishi mbali mbali, binti wa kwanza wa Madiba indie alive sema...mama game aliumia sana kuachwa name Mandela! hutaki?
 
wewe dada ni fulu komedi, wanguzu wakikuambia ww ni mwanaume unakubali.....! lol, kwa akili zako unaamini mtu kama Helle Berry au Tiger Woods, ni maariufu kuliko mandela?

Kuna watu hawamjui Mandela usione wewe unatazama TV unamjuwa kuna watu hawajui TV ni nini.

Hata useme nini, mimi naamini Michael Jackson anajulikana zaidi ya Mandela. Wengi wamemjuwa Mandela baada ya kutoka jela na si kabla, Michael Jakson ni maarufu kwa kui entertain dunia. Mziki hauna rangi hauna siasa hauna kabila hauna lugha.

Kuna watu duniani siasa hawana habari nayo kabisa, lakini nani asiye na habari na mziki? hata kama hapendi atausikia tu japo kwa mbali.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom