Leak
JF-Expert Member
- Feb 22, 2012
- 51,961
- 41,438
Mzee Makamba anasema Askofu Gwajima na Polepole hawavumiliki ndani ya CCM kwakuwa wamekuwa wamekuwa wakipingana na Serikali hasa kwenye swala hili la chanjo.
Mzee Makamba anasema baadhi ya viongozi wa CCM wamekuwa wakimdharau sana Rais samia hivyo ametaka washughulikiwe mara moja.
Mzee Makamba anasema yeye si msemaji wa CCM lakini anashangaa ukimya wa baadhi ya Wana CCM na viongozi wa CCM hasa katika hali ya Rais kuonekana ana dharauliwa na baadhi ya wana CCM.
Mzee Makamba ametaka wana CCM kuwachukulia hatua Gwajima na Pole pole.. kwani hawavumiliki.
=====
BAADHI ya viongozi waandamizi ndani ya chama tawala nchini Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Serikali, wanadaiwa kuwa na mkakati wa makusudi wa kumdharau Rais wa Taifa hilo, Samia Suluhu Hassan.
Taarifa kutoka ndani ya chama hicho, zinasema hatua ya viongozi wake wakuu, kunyamazia matendo ya Mbunge wa Kawe, Askofu Josephat Gwajima na mwenzake, Humphrey Polepole, inatafsiriwa ni dalili tosha kuwa “wanamdharau na kumpuuza,” Rais Samia.
Polepole, ambaye ni mbunge wa kuteuliwa na Rais na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, pamoja na Askofu Gwajima, wamekuwa na kampeni ya wazi ya kupinga chanjo ya corona, kinyume na maelekezo ya chama chao.
Kutokana na hayo, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Mzee Yusuf Makamba, Naibu Katibu Mkuu Bara wa NCCR-Mageuzi, Anthony Komu na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Profesa Edward Hoseah wamezungunzia kadhia hiyo na hatari wanayoiona ndani ya serikali na CCM.
Undani wake, soma Gazeti la Raia Mwema toleo la leo Ijumaa tarehe 20 Agosti 2021.
Mzee Makamba anasema baadhi ya viongozi wa CCM wamekuwa wakimdharau sana Rais samia hivyo ametaka washughulikiwe mara moja.
Mzee Makamba anasema yeye si msemaji wa CCM lakini anashangaa ukimya wa baadhi ya Wana CCM na viongozi wa CCM hasa katika hali ya Rais kuonekana ana dharauliwa na baadhi ya wana CCM.
Mzee Makamba ametaka wana CCM kuwachukulia hatua Gwajima na Pole pole.. kwani hawavumiliki.
=====
BAADHI ya viongozi waandamizi ndani ya chama tawala nchini Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Serikali, wanadaiwa kuwa na mkakati wa makusudi wa kumdharau Rais wa Taifa hilo, Samia Suluhu Hassan.
Taarifa kutoka ndani ya chama hicho, zinasema hatua ya viongozi wake wakuu, kunyamazia matendo ya Mbunge wa Kawe, Askofu Josephat Gwajima na mwenzake, Humphrey Polepole, inatafsiriwa ni dalili tosha kuwa “wanamdharau na kumpuuza,” Rais Samia.
Polepole, ambaye ni mbunge wa kuteuliwa na Rais na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa, pamoja na Askofu Gwajima, wamekuwa na kampeni ya wazi ya kupinga chanjo ya corona, kinyume na maelekezo ya chama chao.
Kutokana na hayo, Katibu Mkuu mstaafu wa CCM, Mzee Yusuf Makamba, Naibu Katibu Mkuu Bara wa NCCR-Mageuzi, Anthony Komu na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Profesa Edward Hoseah wamezungunzia kadhia hiyo na hatari wanayoiona ndani ya serikali na CCM.
Undani wake, soma Gazeti la Raia Mwema toleo la leo Ijumaa tarehe 20 Agosti 2021.