Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,644
- 218,093
Mzee Juma Duni Haji kwanza Shikamoo , waendeleaje na hali yako mzee wangu ?
Nimekusikia Mzee ukizungumzia sakata la Freeman Mbowe , umesema ukipata nafasi ya kusaidia Mbowe kutoka gerezani utafanya hivyo bila kujali kama UTATUKANWA , na ukaenda mbali kwa kudai kwamba wanaotaka Mbowe aendelee kusota jela wao wako Ulaya wakitumbua maisha mazuri .
Tunakushukuru sana Mzee wetu kwa huruma yako uliyoionyesha kwa Mbowe , kwa kujitoa kwako kutaka "usaidie" atoke jela, Tunakuombea kwa Mungu akulipe kwa moyo wako huo , Amina.
Bali tunachokutaarifu ni kwamba Freeman Mbowe hatotoka jela kwa kujidhalilisha , hatotoka gerezani kwa kumpigia magoti yoyote kwa TUHUMA ZA UONGO ZA UGAIDI ALIZOBAMBIKWA NA WATAWALA WAOGA wanaoogopa Katiba mpya , wewe Mzee Duni unawafahamu waliombambikia kesi ya Uongo Mbowe, hao ndio wanaotaka Mbowe afie jela, hawa ndio waliokubambikia wewe mwenyewe na wenzako KESI YA UHAINI miaka ya nyuma, usisahau Baba yako mzazi alivyopigwa Kibao Mahakamani hadi akaanguka alipokuwa anakuja kukusalimia , na tangu siku hiyo hukumuona tena Baba yako hadi alipokufa na kuzikwa , Mzee hawa ndio ambao hawataki Mbowe atoke jela , usiwasingizie walio Ulaya .
Wasiotaka Mbowe awe Huru ni hao CCM ambao wewe na chama chako cha ACT mmeunda serikali ya Mseto Zanzibar , kwamba wewe na wenzako ni sehemu ya serikali inayomkandamiza Mbowe, na sasa mmekubaliana kudanganya Dunia kwamba Mtaunda TUME HURU BILA KATIBA MPYA , Yaani bila Katiba Mpya Mahera au Jecha watakuwa wanaongoza TUME HURU ZA UCHAGUZI ! Hiki ni kituko cha Karne ! yaani Katiba ile ile inayomruhusu Mwenyekiti wa ccm kuteua na kufukuza atakavyo eti leo tuiundie Tume Huru !
Japo nimeandika mengi lakini lengo langu ni kukumbusha kwamba WANAOTAKA MBOWE AFIE JELA NI HAO HAO WASHIRIKA WENU WA MADARAKA , WALA SI WALE UNAODAI WAKO ULAYA , Kwa Umri ulionao na madhira uliyopitia hatukutegemea upotoshaji wa namna hii kutoka kwako , BADO NAAMINI ULINUKULIWA VIBAYA .
Wabillah Tawfiq
Nimekusikia Mzee ukizungumzia sakata la Freeman Mbowe , umesema ukipata nafasi ya kusaidia Mbowe kutoka gerezani utafanya hivyo bila kujali kama UTATUKANWA , na ukaenda mbali kwa kudai kwamba wanaotaka Mbowe aendelee kusota jela wao wako Ulaya wakitumbua maisha mazuri .
Tunakushukuru sana Mzee wetu kwa huruma yako uliyoionyesha kwa Mbowe , kwa kujitoa kwako kutaka "usaidie" atoke jela, Tunakuombea kwa Mungu akulipe kwa moyo wako huo , Amina.
Bali tunachokutaarifu ni kwamba Freeman Mbowe hatotoka jela kwa kujidhalilisha , hatotoka gerezani kwa kumpigia magoti yoyote kwa TUHUMA ZA UONGO ZA UGAIDI ALIZOBAMBIKWA NA WATAWALA WAOGA wanaoogopa Katiba mpya , wewe Mzee Duni unawafahamu waliombambikia kesi ya Uongo Mbowe, hao ndio wanaotaka Mbowe afie jela, hawa ndio waliokubambikia wewe mwenyewe na wenzako KESI YA UHAINI miaka ya nyuma, usisahau Baba yako mzazi alivyopigwa Kibao Mahakamani hadi akaanguka alipokuwa anakuja kukusalimia , na tangu siku hiyo hukumuona tena Baba yako hadi alipokufa na kuzikwa , Mzee hawa ndio ambao hawataki Mbowe atoke jela , usiwasingizie walio Ulaya .
Wasiotaka Mbowe awe Huru ni hao CCM ambao wewe na chama chako cha ACT mmeunda serikali ya Mseto Zanzibar , kwamba wewe na wenzako ni sehemu ya serikali inayomkandamiza Mbowe, na sasa mmekubaliana kudanganya Dunia kwamba Mtaunda TUME HURU BILA KATIBA MPYA , Yaani bila Katiba Mpya Mahera au Jecha watakuwa wanaongoza TUME HURU ZA UCHAGUZI ! Hiki ni kituko cha Karne ! yaani Katiba ile ile inayomruhusu Mwenyekiti wa ccm kuteua na kufukuza atakavyo eti leo tuiundie Tume Huru !
Japo nimeandika mengi lakini lengo langu ni kukumbusha kwamba WANAOTAKA MBOWE AFIE JELA NI HAO HAO WASHIRIKA WENU WA MADARAKA , WALA SI WALE UNAODAI WAKO ULAYA , Kwa Umri ulionao na madhira uliyopitia hatukutegemea upotoshaji wa namna hii kutoka kwako , BADO NAAMINI ULINUKULIWA VIBAYA .
Wabillah Tawfiq