Samcezar
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 13,096
- 22,625
Mimi bado namkubali Babu wa taifa mzee wetu Nyerere. Yule mzee MUNGU ampe amani ya kudumu na amfutie adhabu kali za makosa yake ya kibinadamu. Ila mzee yule alionyesha utu na uzalendo kwa vitendo.
Alikataa kujengewe nyumba kule kwake butiama.
Aliwachomololea JWTZ kama sio JKT kumjengea barabara kuelekea kwake.
Familia yake iliishi maisha ya kawaida kabisa, mama maria alikuwa akila chakula anacholima kwa mikono yake.
Watoto wa Babu wa taifa aliwapiga marufuku kuingia katika siasa kwa mchezo wa kurithi nyayo zake. Watoto wake wameanza kushiriki siasa baada ya kifo chake.
Aliishi kwa mshahara wake na hakupenda marupurupu yasiyo ya lazima
Alikuwa na nafasi ya kutuuza au kujipatia milki na ufalme wa rasilimali na hakukuwa wa kumpinga miaka ile maana aliogopwa kama malaika pia taifa lilikuwa na ushamba na exposure ndogo kwa 90%. Ila akawa muungwana akaridhia kuwapa kijiti wenzake na yeye kubakia kuwa mshauri wa chama na viongozi.
Yeye ndio kisababishi kikubwa sana za vita dhidi ya matabaka ambayo pengine tusingekuwa serious au tungekuwa na viongozi takataka kama wa sasa basi tungejikuta tupo katika maisha mabaya sana ya wachache kuhodhi taifa na wengi kuwa mashakani.
Mzee Nyerere ndie musisi wa umoja wa taifa kupitia lugha ya kiswahili. Leo unaweza kwenda mkoa wowote na ukaongea na wenyeji wa huo mkoa bila shda na mkaelewana.
Leo maisha ya mjini ndio kimbilio la wengi na watu wanaishi bila hata ya kuulizana maswali ya kibaguzi. Viongozi washenzi wachache wanashindwa kusimamia haya mambo especially kwenye eneo la utofauti wa dini na kujikuta wao wanaijua sana dini mbwa hawa tuwadhibiti wasituharibie jamio yetu.
Mzee nyerere kafanya mengi. Kwa yale machache aliyokosea tukunjue roho ila tumuenzi kwa mazuri ambayo hadi leo yanatuweka hapa na kujiita watanzania kwa uhodari na umaridadi.
MUNGU ibariki afrika, MUNGU ibariki Tanzania, MUNGU wabariki watanzania. Lakini MUNGU baba walaani watu wanaojiita watanzania na kutwa kucha matendo yao yanalenga kuliangamiza taifa letu, walaani na kuwatokomeza hao mbwa. Milele Tanzania itasimama.
Alikataa kujengewe nyumba kule kwake butiama.
Aliwachomololea JWTZ kama sio JKT kumjengea barabara kuelekea kwake.
Familia yake iliishi maisha ya kawaida kabisa, mama maria alikuwa akila chakula anacholima kwa mikono yake.
Watoto wa Babu wa taifa aliwapiga marufuku kuingia katika siasa kwa mchezo wa kurithi nyayo zake. Watoto wake wameanza kushiriki siasa baada ya kifo chake.
Aliishi kwa mshahara wake na hakupenda marupurupu yasiyo ya lazima
Alikuwa na nafasi ya kutuuza au kujipatia milki na ufalme wa rasilimali na hakukuwa wa kumpinga miaka ile maana aliogopwa kama malaika pia taifa lilikuwa na ushamba na exposure ndogo kwa 90%. Ila akawa muungwana akaridhia kuwapa kijiti wenzake na yeye kubakia kuwa mshauri wa chama na viongozi.
Yeye ndio kisababishi kikubwa sana za vita dhidi ya matabaka ambayo pengine tusingekuwa serious au tungekuwa na viongozi takataka kama wa sasa basi tungejikuta tupo katika maisha mabaya sana ya wachache kuhodhi taifa na wengi kuwa mashakani.
Mzee Nyerere ndie musisi wa umoja wa taifa kupitia lugha ya kiswahili. Leo unaweza kwenda mkoa wowote na ukaongea na wenyeji wa huo mkoa bila shda na mkaelewana.
Leo maisha ya mjini ndio kimbilio la wengi na watu wanaishi bila hata ya kuulizana maswali ya kibaguzi. Viongozi washenzi wachache wanashindwa kusimamia haya mambo especially kwenye eneo la utofauti wa dini na kujikuta wao wanaijua sana dini mbwa hawa tuwadhibiti wasituharibie jamio yetu.
Mzee nyerere kafanya mengi. Kwa yale machache aliyokosea tukunjue roho ila tumuenzi kwa mazuri ambayo hadi leo yanatuweka hapa na kujiita watanzania kwa uhodari na umaridadi.
MUNGU ibariki afrika, MUNGU ibariki Tanzania, MUNGU wabariki watanzania. Lakini MUNGU baba walaani watu wanaojiita watanzania na kutwa kucha matendo yao yanalenga kuliangamiza taifa letu, walaani na kuwatokomeza hao mbwa. Milele Tanzania itasimama.