Prof Koboko
JF-Expert Member
- Aug 15, 2020
- 350
- 2,549
Hivi JK na CCM hamuoni hata aibu kwenda Zambia kuangalia wenzetu walivyopiga hatua kuhusu demokrasia yao ya vyama vingi na kuheshimu maamuzi ya wananchi wao? Yaani Makada wa CCM mmejaa kwenye ndege kwenda Zambia kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais halali aliyetoka na Upinzani, ninyi hamkufuta uchaguzi wa Zanzibar mwaka 2015 baada ya mambo kwenda ndivyo sivyo? Hata mshipa wa aibu hakuna kabisa na Mungu humuogopi?
Ninatambua kua JK alikua mwangalizi wa uchaguzi wa Zambia, amejifunza kitu gani kwenye siasa za wenzetu kwa yaliyotokea kwao? Mzee anajiskiaje kwa kilichotokea kule Zanzibar 2015? Kwa mujibu wa Marehemu Maalim Seif baada ya CCM kushindwa Zanzibar Mwenyekiti aliyekua anamaliza muda wake kwa maana ya JK alikataa Shein kuachia kiti matokeo yake wakaleta hoja ya kufuta matokeo ilimradi tu kiti kisiende CUF. Aibu iliyoje!
CCM na JK muogopeni Mungu ninyi hamna moral authority ya kuzungumzia uchaguzi wa Zambia, wenzetu siyo kama ninyi, wao walishavuka hatua tulipo sisi. Wakati mnawapongeza tazameni makando kando yenu na mkumbuke laana ya Mungu kwenu.Hamuwezi kuzungumzia demokrasia ya Zambia wakati yenu yamewashinda.
Tunafahamu na nnaelewa ya kwamba CCM imechokwa na Wananchi na huenda muda si mrefu mkaodoka, mmebakia kusimamiwa na dola lakini humuwezi kusimama kama chama cha siasa tena,dhuluma mnayoifanya kwenye chaguzi ina mwisho wake ambao kimsingi ndio mwisho wenu. Kwa bahati mbaya ubaya hua hauna maisha marefu sana.
Acheni kuisifu Zambia wakati kwenu shida ya demokrasia ni kubwa sana, kama kwenda kwenu Zambia ninaimami mmejifunza kwa sababu pia siamini kama chama Upinzani kilikialika chama tawala Tanzania, iwe somo kwenu mkirudi nyumbani mtulie na mjisikie aibu.
Ninatambua kua JK alikua mwangalizi wa uchaguzi wa Zambia, amejifunza kitu gani kwenye siasa za wenzetu kwa yaliyotokea kwao? Mzee anajiskiaje kwa kilichotokea kule Zanzibar 2015? Kwa mujibu wa Marehemu Maalim Seif baada ya CCM kushindwa Zanzibar Mwenyekiti aliyekua anamaliza muda wake kwa maana ya JK alikataa Shein kuachia kiti matokeo yake wakaleta hoja ya kufuta matokeo ilimradi tu kiti kisiende CUF. Aibu iliyoje!
CCM na JK muogopeni Mungu ninyi hamna moral authority ya kuzungumzia uchaguzi wa Zambia, wenzetu siyo kama ninyi, wao walishavuka hatua tulipo sisi. Wakati mnawapongeza tazameni makando kando yenu na mkumbuke laana ya Mungu kwenu.Hamuwezi kuzungumzia demokrasia ya Zambia wakati yenu yamewashinda.
Tunafahamu na nnaelewa ya kwamba CCM imechokwa na Wananchi na huenda muda si mrefu mkaodoka, mmebakia kusimamiwa na dola lakini humuwezi kusimama kama chama cha siasa tena,dhuluma mnayoifanya kwenye chaguzi ina mwisho wake ambao kimsingi ndio mwisho wenu. Kwa bahati mbaya ubaya hua hauna maisha marefu sana.
Acheni kuisifu Zambia wakati kwenu shida ya demokrasia ni kubwa sana, kama kwenda kwenu Zambia ninaimami mmejifunza kwa sababu pia siamini kama chama Upinzani kilikialika chama tawala Tanzania, iwe somo kwenu mkirudi nyumbani mtulie na mjisikie aibu.