Mzee hataki mdogo wangu aoe binti aliyelelewa na Single Mother

LICHADI

JF-Expert Member
Feb 4, 2015
4,124
11,113
Wakuu poleni na majukumu

Mdogo wangu wa kiume alileta taarifa za kuoa kwa mzee wetu nyumbani Marangu Mamba Lekura, mkoa wa Kilimanjaro, Binti aliyehitaji kumuoa ni Mwenyeji wa Mkoa wa Bukoba huko

So mzee alipokea swala lake kwa mikono miwili, wakaitwa wazee wengine siku ikapangwa kuelekea nyumbani kwa Binti Bukoba kwa wazazi wake ili kuweka mambo sawa, kilichotokea baada ya kufika huko mzee akawakuta ndugu wa binti upande wa mama yake lanini upande wa mwanaume hajaonekana hata mmoja

Mzee kuona hivyo ikabidi ahoji kuwa ndugu wa binti kuanzia baba yake mzazi na baba zake wadogo hadi shangazi zake wako wapi, anahitaji kuwaona na kuwafahamu, mama mtu akasema kuwa waliachana na baba wa binti mda hivyo yeye ndio kila kitu kwa Binti

Mzee kusikia hivyo akaliamsha popo kuwa hapa hamna cha ndoa wala kuchumbia , akampiga mkwara mdogo wangu kuwa pale sio pa kuowa ataowa majanga hivyo mzee wakaondoka na wazee wenzake kurudi marangu wakamuacha dogo kule kasusa kurudi na wazee

Mzee ana hoja hizi kwa nilivyomsikia mimi

* Anasema kuoa Binti ambaye alikosa malezi ya baba,kutokana na ugomvi kati ya wazazi wake huwa ni majanga

*Mzee anasema kuwa mabinti wengi walioshuhudia kuachana kwa wazazi wao hasa ukute mama ndio alikuwa na majanga basi na wao mbeleni huwa ni wasumbufu vile vile maana mama zo huwajaza sumu kuhusu wanaume

* Mzee anadai familia yoyote unayoenda kuowa baba wa mwanamke lazima awepo hata kama kashafariki basi ndugu wa baba kama baba wadogo wawepo la sivyo yakitokea matatizo huko mbeleni hutokuwa na mtu wa kumkemea huyo binti kama ana majanga, na ndoa haitokuwa na Baraka

* Mzee pia anadai kuwa masingle mother wengi huachwa na wanaume kutokana n matatizo mbali mbali hasa kutokujielewa hivyo huwalea watoto na kuwajaza sumu kuhusu wanaume hivyo binti huwa tayari kashalelewa vibaya na ashaona mama yake ameishi mwenyewe hivyo hata mkipishana kauli kukwambia achana nae aishi mwenyewe haoni tabu

* Pia anadai mabinti wengi wanaolelewa na mama zao tu wakati baba wapo hai, huwa wana matatizo hata ukioa hiyo ndoa haitodumu

Dogo kapagawa, na mzee ndio msimamo wake sijui nyie wakuu wa hapa JF manasemaje mzee yupo sawa?
 
Mzee Yuko sahihi upande wake maana hataki yatokee mabaya huko mbeleni, lakini afahamu mapenzi hayashauriki hasa kwa mtu aliyependa kupitiliza...amuweke chini amuelezee kijana asiporidhika amuache na ndoa ifungwe maana anaenda kuishi nae yeye hata likitokea tatizo mzee asiwe kwenye lawama kuliko kuwa kwenye lawama ya kumzuia kuoa ilihali hamfahamu binti na kutokuwa na mzazi wa kiume asichukulie Kama kigezo.
 
Kwa hiyo mzee wako shida Ni baba tu angehedhuria hiyo sherehe na sio awe amemlea Wala Nini, he is very wrong
Hamna mwanamke anayependa kulea watoto mwenyewe hata siku moja jaman Ni katika purukushani za maisha tu.
Na Mara nyingi wa hivyo ndo wanakuaga wazuri as hatopenda wanae wapate malezi Kama yake
Mzee atakua kakutana na mchepuko wake wa zaman Nini🏃🏃
 
Bila kusahau wengi huwa hawana heshima kwa wanaume zao au waume zao

Sio wote ila asilimia kubwa, ndio maana malezi ya wazazi wote wawili kwa mtoto ni muhimu sana unless itokee sababu iliyo nje ya uwezo wa kibinadamu kama kifo

On the other point, hata mimi nimejiuliza, kama mama alishaachana na baba wa huyo binti, na hakuwepo ndugu yeyote wa kiumeni....yaani hata shangazi, hapo ni pa kujuliza mara mbili, that means ukigombana na baba wa mtoto unagombana na ukoo mzima? Ameshindwa hata kuwashirikisha bava wadogo au mashangazi za huyo binti? Siamini kama wameshirikishwa wakagoma kufika au hata kutuma mwakilishi

On contrary, pengine upande wa kiumeni ulisusa labda binti sio mtoto wao walibambikiwa.

Ni baadhi ya maswali ambayo mzee wako anajiuliza na hana majibu
 
Na huyo Mdogo wako msimamo wake ukoje? Amempenda?

Sio kila ushauri wa Mzazi ni mzuri, nao pia ni binadamu sio Malaika.

Mdogo wako ausikilize moyo wake
 
Bwan Lichad.

Mzee yuko sahihi kabisa. Binti yeyote alelewaye na Baba anatambua majukumu yake kwa mwanaume.
Anapokuwa Mtiifu na Mnyenyekevu kwa baba yake mzazi ndiko kunamfundisha kuwa mtiifu na mnyenyekevu kwa Mwanaume atayekuwa naye.

kitendo cha kwamba huyo binti ajapata malezi ya baba kuna maanisha kuwa huyo binti hayuko tayari kuwa mnyenyekevu na mtiifu kwa mwanaume.

Anapopata umri bila kuwa na social skill ya kutambua wajibu wake kwa mwanaume, kuna uwezekano mkubwa sana naye akaja kuwa Single Mother.
 
Bwan Lichad.

Mzee yuko sahihi kabisa. Binti yeyote alelewaye na Baba anatambua majukumu yake kwa mwanaume.
Anapokuwa Mtiifu na Mnyenyekevu kwa baba yake mzazi ndiko kunamfundisha kuwa mtiifu na mnyenyekevu kwa Mwanaume atayekuwa naye.

kitendo cha kwamba huyo binti ajapata malezi ya baba kuna maanisha kuwa huyo binti hayuko tayari kuwa mnyenyekevu na mtiifu kwa mwanaume.

Anapopata umri bila kuwa na social skill ya kutambua wajibu wake kwa mwanaume, kuna uwezekano mkubwa sana naye akaja kuwa Single Mother.
1. Hajapata malezi ya Baba;
2. Kabila lake nalo ni jambo kufikirisha zaidi.
 
Na huyo Mdogo wako msimamo wake ukoje? Amempenda?

Sio kila ushauri wa Mzazi ni mzuri, nao pia ni binadamu sio Malaika.

Mdogo wako ausikilize moyo wake

Ni kweli kuwa sio kila ushauri wa mzazi sio wa kuuzingatia. Ila kwenye suala la ndoa kama hili linahitaji ustaarabu wa kijana. Mzee ametoa sababu zake zilizo wazi kabisa ya kwanini huyo binti hamfai mwanaye.

Na bahati nzuri sababu zake zina mashiko kama alivyoelezea Mtende hapo juu.

Asilimia kubwa ya mabinti walio lelewa na Single moms huwa wanakosa ujuzi wa asili wa namna sahihi ya kuishi na mwanaume. ndio maana wanasema father figure kwenye familia anamsaada mkubwa sana kwa binti kuliko mother figure.
 
1. Hajapata malezi ya Baba;
2. Kabila lake nalo ni jambo kufikirisha zaidi.

Suala la Kabila wala halina MAshiko sana. Kama mzee angemzuia kuoa huyo binti kwa sababu ya Kabila basi sote humu tungemuona mshamba.

Malezi ya baba kwa binti humfundisha namna vile anavyopaswa kuenenda mbele ya mwanaume. kama amekosa malezi ya baba basi kuna kitu mzee anamuepushia mwanawe huko mbele.
 
Suala la Kabila wala halina MAshiko sana. Kama mzee angemzuia kuoa huyo binti kwa sababu ya Kabila basi sote humu tungemuona mshamba.

Malezi ya baba kwa binti humfundisha namna vile anavyopaswa kuenenda mbele ya mwanaume. kama amekosa malezi ya baba basi kuna kitu mzee anamuepushia mwanawe huko mbele.
Kabila pendwa Lina changamoto zake ndugu. Jaribu uone Moto utauona
 
Kabila pendwa Lina changamoto zake ndugu. Jaribu uone Moto utauona

Sijui nikwambie nini ila ngoja nikupe mfano huu:-

1. Classmate wangu alioa Mhaya, mpaka sasa ni miaka 5 wana watoto 2.
2. Kaka yangu ameoa Mhaya mpaka sasa ni miaka 10 wana watoto 3.
3. Boss wangu ofisini ameoa Mhaya na amezaa naye watoto 5.
4. Jamaa yangu wa karibu aliyetia mimba demu wangu miaka 5 iliyopita (ila waliachana)...ana mtoto 1 na mwanamke wa Kihaya wakiwa na miaka 3 kwenye ndoa hivi sasa.

Hebu niletee facts kuthibitisha wahaya wanashida kwenye ndoa.
 
Back
Top Bottom