Mzazi mwenzangu ananitishia kwenda kunishtaki Ustawi wa Jamii

kyanyangwe

JF-Expert Member
Oct 31, 2018
1,147
2,745
Habari za wakati huu waungwana?

Jamanimwenzenu nina changamoto nimeipata kuhusiana na mzazi mwenzangu.

Iko hivi huyu mwanamke tumezaa mtoto ambae kwa sasa ana umri wa mwaka mmoja na miezi 7. Kiukweli toka ajifungue huyu mtoto nimekuwa nikitoa pesa za matunzo vizuri tu bila shida, ofcoz naye amekuwa akinisaidia katika malezi kwa sababu ni muajiriwa mahala fulani

Sasa basi toka mwaka juzi niliamua kwenda shule kujiendeleza, nilimshirikisha na nikamwambia kwa vile ntakuwa masomoni hivyo hata biashara zangu huku hazitakuwa zinaenda kama ambavyo nipo mimi mwnyewe hivyo nikamuahidi kuwa nampa kiasi cha 150k kutoka 250k kila mwezi kama matumizi ya mtoto

Nashukuru alinielewa,tatizo limiejitokeza mwaka huu, kwa wakazi wa Arusha mtakuwa mashahidi. Toka hii kitu inaitwa covid-19 iingie biashara zimeyumba sana pale Arusha, hivyo na mie nimejikuta nimeyumba kiuchumi,kwa hivo nikashusha kiwango cha kumtumia kama matumizi ya mtoto kutoka 150k mpaka 70k nikamueleza hali halisi.

Toka wakati huo hatujawahi kuwa na maelewano kabisa, anaona kama namfanyia makusudi lakini ukweli ni kwamba siko vizuri kiuchumi kabisa, nimemtumia watu wake wa karibu wamueleweshe lakini ni kama hanielewi vile.

Leo asubuhi kanipigia simu ananiambia kesho anaamkia Ustawi kunishtaki eti nimemtelekeza mtoto wakati sio ukweli, ikumbukwe mwezi wa tano nilimtumia 70k ya matumizi akairudisha akisema eti ndogo haitoshi hata kununua maziwa ya mtoto hivyo mwezi huu sijamtumia kitu bado kwa sababu bado hatujakubaliana kiasi cha kutumiana.

Kiukweli wakuu sina kitu kwa sasa na biashara haziko poa kabisa.

Je, nimuache aende tu huko ustawi au nifanye kitu gani anielewe?
 
Hivi huko ustawi wa jamii sisi me hatuwezi kwenda mkuu ili kesi ziumane tu hukohuko maana naona me hatuna kimbilio hivyo nasi twendeni hukohuko mpaka kieleweke..
 
Usihofu mkuu, huko hamna kitu atapata cha msingi unampa hela hata kama ni kdg lkn unampa.
 
Kamanda wewe ni Jembe, Mungu akubalika sana, Mwambie muongozane huko ustawi, atakuwa na matumizi yake binafsi hivyo hiyo pesa anaitumia kbsa hata kwa kukopa akitaraji areplace ukimpa sasa kupanic na ujeuri vikiungana sijui inakuwaje.
 
kuna makabila siio ya kugusa yaan binti hata awe mzur vp lakn nkishajua tu anatokea hlo kabila yan namtema fastaaa
 
Tena mkitoka ustawi kapashe kiporo kabisa, inawezekana anataka mkagegedane ila anashindwa kukuambia
 
Mwaka mmoja na miezi saba na bado anatumia maziwa tu....wengine mwaka mmoja tu wanashindia mahindi
Mtoto aliyefikisha mwaka mmoha anatakiwa anywe maziwa ya ng'ombe glass moja asubuhi na jioni au walau mara moja tu.
Ni vike tu ugumu wa maisha tu
 
Inaonesha hamna mahusiano mazuri mna ugomvi.
Tatua hilo kwanza.
Mkishakuwa sawa mtaweza kuongea na kukabiliana changamoto hizo na kulea vyema mtoto.
 
nashukuruni waungwana,mmenipa mwanga.maana wengine maswala ya kesi huwa hatuyapendi kabisa.
 
Mkuu mwanamke uliyemzalisha bila kumuowa wanakuwaga na kisirani Tu si rahisi kukubali kirahisi kuachana naye wengi wanatuliaga baada ya mtoto kufika miaka mitatu sababu mtoto anakuja hasumbui sana lakin saivi ata uwe unatoa laki5 ataona humjalia mtoto kikubwa ni mwanaume kuwa kiburi na kutojali kelele zake atoe matumizi kulingana na kipato chake asitake kumfurahisha wangu aliniweke kiwango nikawa nashusha na kupandisha viwango vya pesa kama chati za clinik
 
Back
Top Bottom