donlucchese
JF-Expert Member
- Mar 23, 2011
- 17,043
- 21,517
Nilikua naangalia muvi ya kihindi iitwayo 'Khabi Kush Khabi Gham' ambayo kwa wale walioiona ni yakuteka hisia. Kwa kifupi inahusu kijana ambaye ni mtoto wa tajiri mkubwa lakini akatokea kuzimika kimapenz kwa mtoto wa maskini ambaye mama wa binti huyo ni mfanyakazi kwenye kasri la baba yake na huyo kijana. Kitendo hiki kilimkera mzee wake na kijana hata kupelekea kumfukuza kijana wake huyo ili asitie aibu familia. Sasa inakuaje kwa mzaz kuingilia penz la mwanaye? Na je,unaweza pata laana kwenda against na mzaz wako kwa kitendo cha kufuata moyo wako? Mapenz sidhan kama yanaangalia vigezo ivi,japo ashakum c matusi hawa watanzania wenzetu wenye asili ya kiarabu ni mwiko kuolewa na mtu wa nje ya race yako(mweus) au mtu maskin. We unaonaje? Unaweza kwenda against na mzaz wako 4the sake of yo own happiness?