Infantry Soldier
JF-Expert Member
- Feb 18, 2012
- 15,893
- 16,317
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa Jamiiforums. Mimi mdogo wenu (Last Born) Infantry Soldier nipo mzima kabisa wa afya. Thanks to God the Almighty. Eti ndugu zangu watanzania;
Mzazi mwenye uwezo kumpa mtoto chochote anachokitaka ni sawa na kumharibu? Na kumnyima napo ndio kumjenga?
Nimeamua kuuliza hivi kwa maana kwamba, nilipokuwa form one mnamo mwaka 2000 katika shule moja ya secondary tulipata kupewa T-shirts flani hivi rangi ya dark blue ambazo tulikuwa tunavaa siku ya Ijumaa kama sare ya shule kwa maana siku ile (Ijumaa) ilipangwa kuwa ndio siku ya michezo kwa wanafunzi. Hivyo ikifika saa 6 mchana tu baaaaas masomo yote husitishwa na wanafunzi wote huenda viwanjani kwa ajili ya michezo huku ndugu zetu waislamu wakielekea misikitini (Masjid) kwa ajili ya swala ya Ijumaa.
Sasa bwana ile t-shirt yangu nilikomaa nayo miaka mitatu. Yaaani form one yote ninayo, form two bado ninadunda nayo mpaka form three hiyo mwaka 2002 ngoma ninakomaa nayo ingawa akawa imepauka sana kwa maana wanadai zilikuwa zimetengenezwa kwa cheap cotton hivyo zilikuwa zinatoa rangi wakati wa kufua.
Ilipofika mwezi wa sita, baada ya kufungua likizo ndefu, basi toleo jipya la t-shirt likatolewa, t-shirt nzuri hiiiiizooo, dark blue flani hivi zinavutika vutika mkikaa pale assembling point basi zinang'aaaaa mpaka raha.
Karibia nusu ya rafiki zangu wengi walizinunua t-shirts zile mpaka wasichana. Nikawa ninajisikia inferior sana mbele za wenzangu.
Baada ya kuona vile, mimi niliporudi home tu nikasubiri jioni muda wa kula nikamwambia mama yangu kwa maana shida nyingi huwa ninaongea na mama na sio baba. Mama akalifikisha lile suala kwa mzee baba. Aisee mzee baba aliwaka sio mchezo. Mzee alikuwa anasema "mama Hassan (hilo Hassan ni jina la uongo) hawa watoto ukiwaendekeza kuwapa chochote wanachokitaka utawaharibu hawa, tukifa watashindwa kuishi kwa ndugu" ingawa ilipofika mwisho wa mwezi mama alipewa pesa na baba kisha akanipa mimi nikaenda nunua t-shirt mpyaaaa na mimi nionekane msafi mbele ya mademu wa form 3.
Wazazi mlipo humu Jamiiforums eti ni kweli kumpa mtoto kile anachokitaka ni kumharibu? Na kumyima napo ndio kumjenga?
Ninakaribisha maoni yenu.
OUR MOTTO: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Mzazi mwenye uwezo kumpa mtoto chochote anachokitaka ni sawa na kumharibu? Na kumnyima napo ndio kumjenga?
Nimeamua kuuliza hivi kwa maana kwamba, nilipokuwa form one mnamo mwaka 2000 katika shule moja ya secondary tulipata kupewa T-shirts flani hivi rangi ya dark blue ambazo tulikuwa tunavaa siku ya Ijumaa kama sare ya shule kwa maana siku ile (Ijumaa) ilipangwa kuwa ndio siku ya michezo kwa wanafunzi. Hivyo ikifika saa 6 mchana tu baaaaas masomo yote husitishwa na wanafunzi wote huenda viwanjani kwa ajili ya michezo huku ndugu zetu waislamu wakielekea misikitini (Masjid) kwa ajili ya swala ya Ijumaa.
Sasa bwana ile t-shirt yangu nilikomaa nayo miaka mitatu. Yaaani form one yote ninayo, form two bado ninadunda nayo mpaka form three hiyo mwaka 2002 ngoma ninakomaa nayo ingawa akawa imepauka sana kwa maana wanadai zilikuwa zimetengenezwa kwa cheap cotton hivyo zilikuwa zinatoa rangi wakati wa kufua.
Ilipofika mwezi wa sita, baada ya kufungua likizo ndefu, basi toleo jipya la t-shirt likatolewa, t-shirt nzuri hiiiiizooo, dark blue flani hivi zinavutika vutika mkikaa pale assembling point basi zinang'aaaaa mpaka raha.
Karibia nusu ya rafiki zangu wengi walizinunua t-shirts zile mpaka wasichana. Nikawa ninajisikia inferior sana mbele za wenzangu.
Baada ya kuona vile, mimi niliporudi home tu nikasubiri jioni muda wa kula nikamwambia mama yangu kwa maana shida nyingi huwa ninaongea na mama na sio baba. Mama akalifikisha lile suala kwa mzee baba. Aisee mzee baba aliwaka sio mchezo. Mzee alikuwa anasema "mama Hassan (hilo Hassan ni jina la uongo) hawa watoto ukiwaendekeza kuwapa chochote wanachokitaka utawaharibu hawa, tukifa watashindwa kuishi kwa ndugu" ingawa ilipofika mwisho wa mwezi mama alipewa pesa na baba kisha akanipa mimi nikaenda nunua t-shirt mpyaaaa na mimi nionekane msafi mbele ya mademu wa form 3.
Wazazi mlipo humu Jamiiforums eti ni kweli kumpa mtoto kile anachokitaka ni kumharibu? Na kumyima napo ndio kumjenga?
Ninakaribisha maoni yenu.
OUR MOTTO: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.