Na Salma Said, Zanzibar
MTANZANIA aliyekamatwa na makachero wa Marekani kwa kuhusishwa na ugaidi, Suleiman Abdallah Salim (Morris), amerudishwa Zanzibar juzi na Shirika la Msalaba Mwekundu kutoka Afghanistan baada ya kubainika kwamba si gaidi.
Akizungumza na Mwananchi nyumbani kwao maeneo ya Mombasa, Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar, huku akionekana mchovu, alisema alikamatwa na makachero wa FBI nchini Somali mwaka 2003 akiwa katika shughuli zake za kibiashara na kuingizwa katika gari bila ya kufahamu anapopelekwa.
Akielezea mkasa uliomkuta akiwa eneo la Abusasu, Mjini Mogadishu alisema baada ya kukamatwa na kuingizwa katika gari hilo huku akipata kipigo kutoka kwa maafisa
hao alisafirishwa hadi Nairobi, Kenya na kutakiwa apeleke mtu wa kumdhamani, lakini aliwaambia kuwa yeye ni Mtanzania na kwamba hana ndugu yeyote jijini humo.
Waliniambia mimi ni Msomali nilikataa nikiwaambia kuwa ni Mtanzania. Kisha wakasema ni Myemen nikasema ni Mtanzania walipoona nasema Kiswahili wakaniambia mlete ndugu yako akuwekee dhamana, nikawaambia sina jamaa Nairobi mimi kwetu ni Tanzania, alisimulia Salim.
Alisema baadaye alirejeshwa tena Somali na kuwekwa kwenye kambi ya jeshi na kila mara alikuwa akiulizwa maswali huku akipata kipigo wakati akijibu maswali yao.
Alisema baadhi ya maswali aliyoulizwa yalihusu kama anawafahamu Khalfan, Marwan na Fahad na kutakiwa kusema hao ni akina nani kwake na kwamba aliwajibu kuwa anawafahamu kwa kuwa ni rafiki zake wa karibu aliokuwa akifanya nao kazi ya uvuvi maeneo ya Mombasa kabla ya kwenda Somali.
''Wamarekani wao wanakamata watu tu, yaani wakiona mtu ana ndevu wao wanamkamata na kusema ni gaidi kama Osama, lakini mimi kila mtu ananifahamu kuwa kazi yangu ni kuvua samaki na si Muislamu wa msimamo mkali.
Mimi si mla unga watu wananifahamu mpaka jina langu kwamba naitwa Morris, sasa huo uislamu wa msimamo mkali uko wapi? alisema na kuhoji Salim.
Alisema kutoka Somali alisafirishwa akiwa amefungwa pingu mikononi na miguuni hadi Afghanistan katika jela la Kimarekani liitwalo Darkness ambalo alisema mtu anapoingia humo hawezi kufahamu kama ni mchana wala usiku kutokana na giza totoro lililopo.
''Sisi tunaliita darkness kwa sababu huwezi kujua leo ni lini? Sasa hivi saa ngapi wala kama ni usiku au mchana ni giza tupu huoni mtu huko,'' alisema.
Alifahamisha kuwa katika jela hiyo ambayo inatisha husikika sauti za muziki wa kutisha huku baadhi ya nyimbo za Kiswahili zikisema hakuna Mungu pamoja na sauti za baadhi ya wanyama kama mbwa, paka na simba.
Nyimbo za Kiswahili nilizisikia zinasema hakuna Mungu, Uislamu sio dini lakini pia kuna milio mikali ya sauti za kutisha kama mabati yanavunjwa, kengele za kanisani, sauti za mbwa anayebweka na milio ya kutisha, alisema.
Salim alisema baadaye alihamishiwa katika gereza lingine liitwalo Chatem bila ya kufahamu siku kwani hakuwa anafahamu kama siku imemalizika kwa sababu kulikuwa na mwanga wakati wote.
''Mimi sikuwa najua kama leo ni siku gani wala sikuwa na mtu wa kumuuliza ingawa kulikuwa na watu wengine, lakini hatukuwa tunaruhusiwa kuzungumza kwani wanajeshi walikuwa wametusimamia.
Ukimuuliza mwenzako chochote unaambiwa unyanyue mikono juu kama vile Yesu anasulubiwa kwa masaa mawili bila ya kushusha na kama utashusha kwa uchovu unaambiwa anza yaani ilikuwa balaa,'' alisema huku akitokwa na machozi.
Salim alisema baadaye alihamishiwa katika Kambi ya Jeshi iitwayo Bagram akiwa amefungwa minyororo na vioo vya macho.
''Nilivalishwa minyororo na vioo vya macho kama mwendesha pikipiki na walikuwa wananipa chakula kila baada ya siku mbili, wakati huo nilikuwa naumwa sana na afya yangu haikuwa nzuri. Kuna siku makachero wa FBI walinifanyia interview mara mbili nikapata asilimia mia moja,'' alisema.
Salim ambaye vidole vyake vimevunjwa, alisema alipokamatwa aliambiwa kuwa ameiba fedha za Msomali mmoja, lakini alipopelekwa Afghanistan hakutajiwa hata siku moja kama anashtakiwa kwa kosa fulani hadi alipoachiwa na kurejeshwa nyumbani.
Alifahamisha kuwa baada ya kukaa miaka yote hiyo, maafisa wa kimarekani walimueleza kwamba hana hatia na kama anataka kupelekwa Marekani au Uingereza kuishi huko aseme ili afanyiwe utaratibu wa kuishi huko, lakini alikataa kwa kuwa hajaonana na wazazi wake miaka mingi sana.
Unajua waliniambia kama unataka kuishi Marekani sema nikawaambia hapana mimi nataka kurejeshwa Tanzania. Kwanza sikuamini kama nitarejeshwa kweli kwa sababu nilikuwa
nimeshachoka na nilikuwa tayri nimeshakata tamaa ya kuishi, alisema kwa huzuni
*********************************************************
Wadau Hii imekaaje?..Kuna Haki hapa?
MTANZANIA aliyekamatwa na makachero wa Marekani kwa kuhusishwa na ugaidi, Suleiman Abdallah Salim (Morris), amerudishwa Zanzibar juzi na Shirika la Msalaba Mwekundu kutoka Afghanistan baada ya kubainika kwamba si gaidi.
Akizungumza na Mwananchi nyumbani kwao maeneo ya Mombasa, Mkoa wa Mjini Magharibi, Zanzibar, huku akionekana mchovu, alisema alikamatwa na makachero wa FBI nchini Somali mwaka 2003 akiwa katika shughuli zake za kibiashara na kuingizwa katika gari bila ya kufahamu anapopelekwa.
Akielezea mkasa uliomkuta akiwa eneo la Abusasu, Mjini Mogadishu alisema baada ya kukamatwa na kuingizwa katika gari hilo huku akipata kipigo kutoka kwa maafisa
hao alisafirishwa hadi Nairobi, Kenya na kutakiwa apeleke mtu wa kumdhamani, lakini aliwaambia kuwa yeye ni Mtanzania na kwamba hana ndugu yeyote jijini humo.
Waliniambia mimi ni Msomali nilikataa nikiwaambia kuwa ni Mtanzania. Kisha wakasema ni Myemen nikasema ni Mtanzania walipoona nasema Kiswahili wakaniambia mlete ndugu yako akuwekee dhamana, nikawaambia sina jamaa Nairobi mimi kwetu ni Tanzania, alisimulia Salim.
Alisema baadaye alirejeshwa tena Somali na kuwekwa kwenye kambi ya jeshi na kila mara alikuwa akiulizwa maswali huku akipata kipigo wakati akijibu maswali yao.
Alisema baadhi ya maswali aliyoulizwa yalihusu kama anawafahamu Khalfan, Marwan na Fahad na kutakiwa kusema hao ni akina nani kwake na kwamba aliwajibu kuwa anawafahamu kwa kuwa ni rafiki zake wa karibu aliokuwa akifanya nao kazi ya uvuvi maeneo ya Mombasa kabla ya kwenda Somali.
''Wamarekani wao wanakamata watu tu, yaani wakiona mtu ana ndevu wao wanamkamata na kusema ni gaidi kama Osama, lakini mimi kila mtu ananifahamu kuwa kazi yangu ni kuvua samaki na si Muislamu wa msimamo mkali.
Mimi si mla unga watu wananifahamu mpaka jina langu kwamba naitwa Morris, sasa huo uislamu wa msimamo mkali uko wapi? alisema na kuhoji Salim.
Alisema kutoka Somali alisafirishwa akiwa amefungwa pingu mikononi na miguuni hadi Afghanistan katika jela la Kimarekani liitwalo Darkness ambalo alisema mtu anapoingia humo hawezi kufahamu kama ni mchana wala usiku kutokana na giza totoro lililopo.
''Sisi tunaliita darkness kwa sababu huwezi kujua leo ni lini? Sasa hivi saa ngapi wala kama ni usiku au mchana ni giza tupu huoni mtu huko,'' alisema.
Alifahamisha kuwa katika jela hiyo ambayo inatisha husikika sauti za muziki wa kutisha huku baadhi ya nyimbo za Kiswahili zikisema hakuna Mungu pamoja na sauti za baadhi ya wanyama kama mbwa, paka na simba.
Nyimbo za Kiswahili nilizisikia zinasema hakuna Mungu, Uislamu sio dini lakini pia kuna milio mikali ya sauti za kutisha kama mabati yanavunjwa, kengele za kanisani, sauti za mbwa anayebweka na milio ya kutisha, alisema.
Salim alisema baadaye alihamishiwa katika gereza lingine liitwalo Chatem bila ya kufahamu siku kwani hakuwa anafahamu kama siku imemalizika kwa sababu kulikuwa na mwanga wakati wote.
''Mimi sikuwa najua kama leo ni siku gani wala sikuwa na mtu wa kumuuliza ingawa kulikuwa na watu wengine, lakini hatukuwa tunaruhusiwa kuzungumza kwani wanajeshi walikuwa wametusimamia.
Ukimuuliza mwenzako chochote unaambiwa unyanyue mikono juu kama vile Yesu anasulubiwa kwa masaa mawili bila ya kushusha na kama utashusha kwa uchovu unaambiwa anza yaani ilikuwa balaa,'' alisema huku akitokwa na machozi.
Salim alisema baadaye alihamishiwa katika Kambi ya Jeshi iitwayo Bagram akiwa amefungwa minyororo na vioo vya macho.
''Nilivalishwa minyororo na vioo vya macho kama mwendesha pikipiki na walikuwa wananipa chakula kila baada ya siku mbili, wakati huo nilikuwa naumwa sana na afya yangu haikuwa nzuri. Kuna siku makachero wa FBI walinifanyia interview mara mbili nikapata asilimia mia moja,'' alisema.
Salim ambaye vidole vyake vimevunjwa, alisema alipokamatwa aliambiwa kuwa ameiba fedha za Msomali mmoja, lakini alipopelekwa Afghanistan hakutajiwa hata siku moja kama anashtakiwa kwa kosa fulani hadi alipoachiwa na kurejeshwa nyumbani.
Alifahamisha kuwa baada ya kukaa miaka yote hiyo, maafisa wa kimarekani walimueleza kwamba hana hatia na kama anataka kupelekwa Marekani au Uingereza kuishi huko aseme ili afanyiwe utaratibu wa kuishi huko, lakini alikataa kwa kuwa hajaonana na wazazi wake miaka mingi sana.
Unajua waliniambia kama unataka kuishi Marekani sema nikawaambia hapana mimi nataka kurejeshwa Tanzania. Kwanza sikuamini kama nitarejeshwa kweli kwa sababu nilikuwa
nimeshachoka na nilikuwa tayri nimeshakata tamaa ya kuishi, alisema kwa huzuni
*********************************************************
Wadau Hii imekaaje?..Kuna Haki hapa?