Mysol ni kampuni ya kitapeli, imewatapeli Wazazi wangu. Wananchi chukueni tahadhari

misskijiji

Member
Feb 23, 2023
27
72
Naandika kwa uchungu sana Ndugu zangu wa Jamii Forums.

Mimi ni mdada mjasiriamali mdogo ambaye nimepambana kutafuta Ajira baada ya kumaliza Degree yangu 2021 bila mafanikio.Kupitia biashara zangu ndogongodo,nimefanikiwa kuwajengea nyumba ndogo ya vyumba viwili Wazazi wangu huko Kijijini kwetu Ikungi, Singida.

Kwa kuwa umeme bado haujafika, niliwatumia Pesa Wazee wangu mwezi Januari mwaka huu ili wakakope Sola ya Kampuni ya MYSOL ili wapate mwanga. Walienda ofisini kwao wakiongozana na mdogo wangu wa Kidato cha Nne, wakajaza Fomu zao na kulipa malipo ya awali ya shilingi 220,000 tarehe 11 Januari 2023. Hivi ninavyoandika, leo ni tarehe 20 Machi na hao wahusika wa Kampuni hawajawahi kwenda kuifunga Sola hiyo nyumbani kama makubaliano yalivyo.

Kila nikiwapigia simu ni danadana na sasa wameni-block kabisa. Jitihada za kwenda ofisini kwao mara kwa mara nazo hazijazaa matunda. Na ikumbukwe kutoka Kijijini kwetu mpaka Mjini kwenye Ofisi zao ni kilometa 278 hivyo mtu hawezi kwenda kufuatilia kila siku hasa ukitilia maanani Wazazi wangu ni wazee.

Niliwasiliana na Kituo cha Polisi Ikungi nao wamenijibu kwamba hiyo si Kesi ya Jinai ni Kesi ya Madai hivyo hawawezi kushughulikia. Naomba msaada kwa anayejua jinsi ya kutatua tatizo hili ili wanirudishie Pesa yangu.

Na pia nawapa ANGALIZO NA ONYO Watanzania wenzangu hasa wa vijijini kuiogopa Kampuni hii ya Sola ya MYSOL ambayo zamani ilikuwa inaitwa MOBISOL maana ni MATAPELI NA MAJAMBAZI WAKUBWA.

Nitashukuru Sana Kwa Msaada wa Ushauri nitakaopata.

ASANTENI Ndugu zangu, MBARIKIWE sana
 
Naandika kwa uchungu sana Ndugu zangu wa Jamii Forums.

Mimi ni mdada mjasiriamali mdogo ambaye nimepambana kutafuta Ajira baada ya kumaliza Degree yangu 2021 bila mafanikio.Kupitia biashara zangu ndogongodo,nimefanikiwa kuwajengea nyumba ndogo ya vyumba viwili Wazazi wangu huko Kijijini kwetu Ikungi, Singida.

Kwa kuwa umeme bado haujafika, niliwatumia Pesa Wazee wangu mwezi Januari mwaka huu ili wakakope Sola ya Kampuni ya MYSOL ili wapate mwanga. Walienda ofisini kwao wakiongozana na mdogo wangu wa Kidato cha Nne, wakajaza Fomu zao na kulipa malipo ya awali ya shilingi 220,000 tarehe 11 Januari 2023. Hivi ninavyoandika, leo ni tarehe 20 Machi na hao wahusika wa Kampuni hawajawahi kwenda kuifunga Sola hiyo nyumbani kama makubaliano yalivyo.

Kila nikiwapigia simu ni danadana na sasa wameni-block kabisa. Jitihada za kwenda ofisini kwao mara kwa mara nazo hazijazaa matunda. Na ikumbukwe kutoka Kijijini kwetu mpaka Mjini kwenye Ofisi zao ni kilometa 278 hivyo mtu hawezi kwenda kufuatilia kila siku hasa ukitilia maanani Wazazi wangu ni wazee.

Niliwasiliana na Kituo cha Polisi Ikungi nao wamenijibu kwamba hiyo si Kesi ya Jinai ni Kesi ya Madai hivyo hawawezi kushughulikia. Naomba msaada kwa anayejua jinsi ya kutatua tatizo hili ili wanirudishie Pesa yangu.

Na pia nawapa ANGALIZO NA ONYO Watanzania wenzangu hasa wa vijijini kuiogopa Kampuni hii ya Sola ya MYSOL ambayo zamani ilikuwa inaitwa MOBISOL maana ni MATAPELI NA MAJAMBAZI WAKUBWA.

Nitashukuru Sana Kwa Msaada wa Ushauri nitakaopata.

ASANTENI Ndugu zangu, MBARIKIWE sana
pole sana
mimi mbona wananihudumia vizuri
niliwanunulia wazazi wangu, wakwe zangu, na nilihitaji taa ya nyongeza niliwatumia hela wakaipeleka wenyewe na kuiunganisha
betri ilivo zingua baada ya miaka mitano wakanipa utaratibu wa kubadilisha nikaufuata, mambo safi
 
Screenshot_20230320-132613_Chrome.jpg
 
Nawashukuru sana ndugu zangu,hakika niliingia choo cha kiume badala ya cha kike,hii ni Kampuni Babaishaji,Ya MATAPELI NA MAJAMBAZI wakubwa,nasafiri kesho kwenda huko Ikungi ili niende Mahakamani kuishtaki,maisha magumu lakini Kampuni UCHWARA kama hii inazidi kutunyonya tu Wananchi maskini na Serikali inaangalia tu
 
Naandika kwa uchungu sana Ndugu zangu wa Jamii Forums.

Mimi ni mdada mjasiriamali mdogo ambaye nimepambana kutafuta Ajira baada ya kumaliza Degree yangu 2021 bila mafanikio.Kupitia biashara zangu ndogongodo,nimefanikiwa kuwajengea nyumba ndogo ya vyumba viwili Wazazi wangu huko Kijijini kwetu Ikungi, Singida.

Kwa kuwa umeme bado haujafika, niliwatumia Pesa Wazee wangu mwezi Januari mwaka huu ili wakakope Sola ya Kampuni ya MYSOL ili wapate mwanga. Walienda ofisini kwao wakiongozana na mdogo wangu wa Kidato cha Nne, wakajaza Fomu zao na kulipa malipo ya awali ya shilingi 220,000 tarehe 11 Januari 2023. Hivi ninavyoandika, leo ni tarehe 20 Machi na hao wahusika wa Kampuni hawajawahi kwenda kuifunga Sola hiyo nyumbani kama makubaliano yalivyo.

Kila nikiwapigia simu ni danadana na sasa wameni-block kabisa. Jitihada za kwenda ofisini kwao mara kwa mara nazo hazijazaa matunda. Na ikumbukwe kutoka Kijijini kwetu mpaka Mjini kwenye Ofisi zao ni kilometa 278 hivyo mtu hawezi kwenda kufuatilia kila siku hasa ukitilia maanani Wazazi wangu ni wazee.

Niliwasiliana na Kituo cha Polisi Ikungi nao wamenijibu kwamba hiyo si Kesi ya Jinai ni Kesi ya Madai hivyo hawawezi kushughulikia. Naomba msaada kwa anayejua jinsi ya kutatua tatizo hili ili wanirudishie Pesa yangu.

Na pia nawapa ANGALIZO NA ONYO Watanzania wenzangu hasa wa vijijini kuiogopa Kampuni hii ya Sola ya MYSOL ambayo zamani ilikuwa inaitwa MOBISOL maana ni MATAPELI NA MAJAMBAZI WAKUBWA.

Nitashukuru Sana Kwa Msaada wa Ushauri nitakaopata.

ASANTENI Ndugu zangu, MBARIKIWE sana
Utapeli ni biashara kubwa sana na HALALI KABISA Tanzania
 
Back
Top Bottom