Elections 2010 My take katika uchaguzi wa Spika wa Bunge

Mkodoleaji

JF-Expert Member
Apr 27, 2008
458
138
Katika wiki hii na hasa siku mbili zilizopita nimefuatilia mijadala kuhusu uchaguzi wa Spika wa Bunge kwenye media zetu (TV na Magazeti). Wengi wa waliochangia walikuwa wanaonyesha kwamba Samuel Sitta anafaa ila anawekea mizengwe na mafisadi ndani ya CCM.

Maoni yangu ni kwamba kama vyombo vyetu vya habari vinataka tupate Spika mzuri visiegemee upande mmoja na kuanza kusema upande mwingine vibaya (tabia ambayo ilifanyika na wanamtandao 2005). Vinachotakiwa kufanywa ni kuweka mizani sawa ya uchambuzi katika masuala yaliyofanywa na wagombea wote (mabaya kwa mazuri). Kwa mfano wagombea wawili Chenge na Sitta mimi kwa kuanza ningeweza kuwaweka ifuatavyo. Chenge amekuwa mwanasheria mkuu wa serikali kwa muda mrefu, hivyo ana uzoefu katika masuala ya sheria na upeo ambao unaweza kusaidia kuongoza bunge. Lakini katika kipindi chake cha uanasheria mkuu ndipo serikali iliingia mikataba mingi ya kiufisadi kwa kisingizio ambayo inaitia hasara kubwa nchi yetu. Kwa upande wa Sitta naweza kusema kuwa amekuwa mbunge kwa muda mrefu, ameshawahi kuwa waziri wa sheria, amewahi kuwa mkurugenzi wa kituo cha uwekezaji na kwa sasa ni Spika aliyemaliza muda wake. Ukiangalia uzoefu wake anafaa kabisa kuongoza bunge, lakini katika kipindi chake cha kuwa Mkurugenzi wa TIC ndipo wawekezaji wanaoitia hasara nchi waliingia, akiwa Spika alionyesha kutokuwa na msimamo kwa kutumia mamilioni ya pesa katika ugomvi wa Mengi na Malima na mkosaji kutopewa adhabu yeyote, kumsimamisha Zitto Kabwe nk.

Wengine mnaweza kuongezea mengine kwa hawa wawili na wengine wote wanaogombea ili tuweze kusaidia kuwapata viongozi ambao kweli wana uchungu na nchi na siyo wenye kuendeleza bifu zao mjengoni.

Nawakilisha
 
Ingefaa kama wale wote waliochukua fomu za kugombea uspika toka CCM tungewapima peke yao kwani wale wa upinzani hawajulikani mpaka sasa hivi!
 
Ingefaa kama wale wote waliochukua fomu za kugombea uspika toka CCM tungewapima peke yao kwani wale wa upinzani hawajulikani mpaka sasa hivi!
Chenge haafai kugombea u spika maana amechafuka sana ananuka ufisadi anastahili afilisiwe kwaanza haata ubunge hatakiwi...hii inatokea tz pekeee duniani
 
Wale wenye kesi mahakaman kama vijisent kuna uwezekano wa kusimamishwa ubunge. Msijisumbue kumfikiria mzee vijisent.
 
CCM wanafanya makosa mkubwa tena ya kuligawa bunge endapo mmoja wa hao wawili atakuwa spika. Kumchagua Sitta ni kuendeleza unafiki bungeni wa kundi linalodai linapambana na ufisadi lakini kamwe haliwezi kufanya chochote ndani ya CCM. Kumchagua Chenge ni sawa na kulifanya bunge lote lionekane limekubaliana na ufisadi maana sijawahi kusmkia Chenge akitumia neno 'ufisadi'. Kwa hiyo wote wawili waachwe na atafutwe mtu anayeonekana no sober, kama huyu wa Dodoma (Mpwapwa).
 
CCM wanafanya makosa mkubwa tena ya kuligawa bunge endapo mmoja wa hao wawili atakuwa spika. Kumchagua Sitta ni kuendeleza unafiki bungeni wa kundi linalodai linapambana na ufisadi lakini kamwe haliwezi kufanya chochote ndani ya CCM. Kumchagua Chenge ni sawa na kulifanya bunge lote lionekane limekubaliana na ufisadi maana sijawahi kusmkia Chenge akitumia neno 'ufisadi'. Kwa hiyo wote wawili waachwe na atafutwe mtu anayeonekana no sober, kama huyu wa Dodoma (Mpwapwa).

Mbunge Mteule wa Mpwapwa anaitwa Gregory Teu, hajagombea na ni Mbunge mpya kabisa mjengoni, hii ni term yake ya kwanza. Nadhani wewe ulimaanisha Bwana Job Ndugai ambaye ni Mbunge Mteule wa Kongwa.
 
Kwa hali inavoelekea Sitta anapigwa chini na Mzee wa VIJISENTI-CHENGE anakalia kiti cha Usipika. Huwezi amini lakini huo ndo mkakati.

Watu wakiambiwa kuwa CCM inaendeshwa na MAFISADI watu wanakomaa tu bila sababu za msingi. Kwa hiyo KUNA SHINIKIZO KUBWA LA MAFISADI (R.Aziz,Chenge,Lowassa,Mramba n.k)NYUMA YA USPIKA WA BUNGE HILI KUWA SPIKA SITA HAFAI NA AKIENDELEA KUWA HAPO ATARUHUSU TENA MIJADALA YA UFISADI AMBAYO ITAWAGHARIMU TENA CCM! Kumbuka bado swala la RADA,KAGODA,DEEP GREEN,NA MEREMETA ZINATOKOTA.
Mimi nasema hivi wafanye haraka sana wampe huyo CHENGE awe supuka. Kwetu
sisi wana CHADEMA tutakuwa tunashangilia kwasababu hii ni kama kututengezea njia nyeupe kwa Uchaguzi 2015 au kabla ya hapo kama kutakuwa na anything hapo katikati.

Maana kama Wabunge 5 CHADEMA waliweza kusimama against wabunge zaidi ya 250 wa CCM vipi sasa wakti kuna Wabunge 50+ wa CHADEMA, ITAKUWA NI MOTO WA KUOTEA MBALI.

Tusubirini anguko kuu la CHAMA CHA MAFISADI-CCM!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom