Ni kweli tatizo la wizi wa vifaa vya magari limekuwa sugu sana DSM nzimaHivi hawa polisi wa TZ wanalipwa mishahara ya kufanya nini haswa jamani! maana mbona sieleweio kabisa.
pole sana ndg...jamaa wamekuibia maeneo ya wapi?maana mi nnayo nissan primera kama yako hii,nilikuwa najipa sana moyo kutokana na uchache wa magari yenyewe hapo mjini...kumbe siku hizi hawachagui
Wizi wa Power window vioo vya magari hasa hizi sight mirror, na head rest vinaibiwa sana , waibaji wengi huvaa vizuri sana , wengi ni watoto mashombe wa kiarabu, hawa watu hutembea na gari zuri kuliko hata la kwako, hutembea na nyundo ndogo yenye ncha ya almasi huweka kitambaa kizito kuzuia mlio , ugonga kioo mara moja na kumwagika kisha kufungua kama yao, vitu hivyo huuzwa Arusha, Mwanza kama wewe umeandika kioo cha gari hapo hawasumbuki sana , wanachukua fremu na mashine alafu wanachukua kioo cha gari makubwa kinauzwa elfu nane pale saba general wanakata vizuri na kufitisha alafu wanauza kama kipya au tshs 30,000 mpaka 50,000.00 jamaa hawa wanapatikana kariakoo pale big bon au kidongo chekundu. sasa hivi wapo wengi na police wanawafahamu sana wengine hutumia piki piki kubwa baja hazina namba na police hawana uwezo wa kuwafukuza kwa piki piki wala gari, baja ni sports bike hivyo huruka wanavyotaka.
Wapi inauzwa hizo alarm hapa Dar?Kwavile Polisi wameshindwa au hawajakuwa na nia ya kudhibiti wimbi la wizi wa vifaa vya magari, ni wajibu wetu kutafuta mbinu ya kutupunguzia hasara zinazotokana na adha hii. Mimi kwa uzoefu wangu, nilifunga 2 way alarm ambayo inakupa notification kwa baadhi ya matukio kwenye gari yako. Gharama yake ni around 250,000, lakini inakuokoa na madhira mengi.
Ahsante kwa ushauri mkuu.... nahisi kama unajambo la maana unataka kuniambia ila lugha imekuwa ngumu. mimi nataka vitu vyangu niambie nitavipataje bila kuvinunua?Mkuu nakushauri usivinunue, tafuta wahuni wape laki mbili maliza kazi... ukiweza jitahidi upate mmoja wa wezi washa ya moto au tumia wazee wa kazi (sauzi shop) wafanye kweli, hutaona tena unaibiwa na watakuheshimu
POLISI NDIO VINARA WA HUO WIZI,