My Opinion: Kati ya hawa watatu LAZIMA mmoja awe rais 2015

kibavu unavyoiona tanzania imefikia wakati wa kuongozwa na mwanamke nauliza tu.
Kwako Luteni, kwanza naomba nikushukuru kwa kusoma mchango wangu na kuchokoza hoja; jibu langu ni kama ifuatavyo:-
Mkuu jibu langu halitakuwa la moja kwa moja, i.e. litakuwa na mzunguko kidogo, na nitarejesha baadhi ya hoja kwako. Nipo tayari kukosolewa.
Mosi, Kwa mtazamo wako unadhani Anna Makinda alikua mgombea bora zaidi kwa nafasi ya uspika kuliko wagombea wote ndani ya chama cha mapinduzi? Je ni kweli ilikua ni dhamira ya dhati kumuweka mwanamke kwenye ile nafasi ambayo ni muhimu kwa kuzingatia kwamba bunge ni moja ya mihimili mitatu ya dola? Jibu la hapa linaweza kukupa picha ya kwanini nimedhani kwamba 2015 kunaweza kusimamishwa mgombea mwanamke toka CCM.

Pili, kama ukirejea hotuba ya mwalimu J.K. Nyerere mwaka 1995 kwamba mgombea anayeteuliwa na CCM kwa kiasi kikubwa ni kama ni Rais tayari. Sababu unaweza kuwa unazijua kwani sina shaka na utashi wako. Moja wananchi bado wanachagua chama zaidi kuliko mgombea, mbili CCM bado ina faida ya kucheza kama ‘mwenyeji’ na ‘bingwa mtetezi’ na mtunga kanuni za mchezo na waamuzi pia.

Tatu, suala la msingi hapa kujiuliza liwe huyo mwanamke ni nani kuliko kuuliza kama Tanzania iko tayari kuongozwa na mwanamke. Binafsi si muumini wa mfumo dume naamini katika uwezo zaidi kuliko jinsia, dini, kabila au eneo mtu anakotokea. Nadhani wewe pia unaweza kuungana nami kwamba tuna mawaziri na viongozi wengine ambao ni wanawake na ambao utendaji na uongzi wao ni bora mara mia zaidi ya baadhi wanaume. Nakumbuka nilishawahi kumueleza jamaa yangu mmoja kwamba ni bora kuwa na kiongozi mwanamke anayewaza na kutenda kama binadamu kuliko kuwa na kiongozi mwanamke anayewaza na kutenda kwa kujaribu kuwaonesha wanaume kwamba yupo sawa na wanaume au ni zaidi ya wanaume.

Na mwisho
…ningependa swali lako uniulize kwamba je kuna mwanamke ambaye yupo tayari kuongoza Tanzania(kwa maana ya uwezo), na sio kama watanzania wapo tayari kuongozwa na rais mwanamke? Kwani kwa mtindo huo mwingine atakuja na kuuliza je Watanzania wapo tayari kuongozwa na Mmasai, mchagga, Mngoni n.k. Wengine watasema je Tanzania ipo tayari kuendelea kuongozwa na Mkristo/Muisilamu/Mkatoriki.n.k. Au wengine watasema je Tanzania ipo tayri kuongozwa na mtu wa kusini/Kaskazini/magharibi/Mashariki….nk. Matokeo ya huo mvurugano nadhani yapo wazi sina haja ya kuyaelezea hapa

Najumuisha hoja yangu kwa kusema suala ni uwezo wa huyo atayekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kujali jinsia yake, dini yake, kabila lake, au kule anakotokea(nikimanisha eneo) au Chama chake.
Asante komrade Luteni...tuendelee kulumbana kwa hoja.
 
Ushauri wangu kwako mkuu, Malizia bandiko lako kwa voting weka YES au NO au NO COMENT!
Thanks.
Mwisho wa siku kieleweke.
 
tutakuwa wajinga kumchagua mtoto alikuwa wa rais aliyepita tz hakuna hilo,baba alikuwa kondoo ndani chui,
lets seek for new life tz slaa oyee au kama vipi kiwa mbwahi mbwahi basi wangu low-sa awajibike na pesa zetu
Conquest-at the risk of seeming rediculace true.......... feellllllling of loooveeee
 
Nimeandika sababu zangu kwa kifupi sana lakini nafikiri zinabeba maana kubwa believe me..................Vote for Dr. W. Slaa .........................OR ...........Vote for Hon. H Mwinyi ........ OR.......... Vote For Hon E. Lowassa
images
......................
images
......................
images
..............Chadema Candidate................................................... CCM Candidate............................... Independent Candidate ......Serikali ya Utawala wa Sheria na Haki...................... Serikali ya Umoja na Mshikamano................... Serikali ya UwajibikajiUna maoni gani kati ya haya majina matatu ni yupi unayempa asilimia kubwa na kwa sababu gani kama kwa haya majina matatu hakuna unayehisi ni mgombea anayefaa ni yupi unayeona atafaa na kwa sababu zipi, natanguliza shukurani.
hongera mwana JFI LUTENI, Rais atakuwa ni dr wa ukweli mh wilbroad slaa
 
Kwako Luteni, kwanza naomba nikushukuru kwa kusoma mchango wangu na kuchokoza hoja; jibu langu ni kama ifuatavyo:-
Mkuu jibu langu halitakuwa la moja kwa moja, i.e. litakuwa na mzunguko kidogo, na nitarejesha baadhi ya hoja kwako. Nipo tayari kukosolewa.
Mosi, Kwa mtazamo wako unadhani Anna Makinda alikua mgombea bora zaidi kwa nafasi ya uspika kuliko wagombea wote ndani ya chama cha mapinduzi? Je ni kweli ilikua ni dhamira ya dhati kumuweka mwanamke kwenye ile nafasi ambayo ni muhimu kwa kuzingatia kwamba bunge ni moja ya mihimili mitatu ya dola? Jibu la hapa linaweza kukupa picha ya kwanini nimedhani kwamba 2015 kunaweza kusimamishwa mgombea mwanamke toka CCM.

Pili, kama ukirejea hotuba ya mwalimu J.K. Nyerere mwaka 1995 kwamba mgombea anayeteuliwa na CCM kwa kiasi kikubwa ni kama ni Rais tayari. Sababu unaweza kuwa unazijua kwani sina shaka na utashi wako. Moja wananchi bado wanachagua chama zaidi kuliko mgombea, mbili CCM bado ina faida ya kucheza kama 'mwenyeji' na 'bingwa mtetezi' na mtunga kanuni za mchezo na waamuzi pia.

Tatu, suala la msingi hapa kujiuliza liwe huyo mwanamke ni nani kuliko kuuliza kama Tanzania iko tayari kuongozwa na mwanamke. Binafsi si muumini wa mfumo dume naamini katika uwezo zaidi kuliko jinsia, dini, kabila au eneo mtu anakotokea. Nadhani wewe pia unaweza kuungana nami kwamba tuna mawaziri na viongozi wengine ambao ni wanawake na ambao utendaji na uongzi wao ni bora mara mia zaidi ya baadhi wanaume. Nakumbuka nilishawahi kumueleza jamaa yangu mmoja kwamba ni bora kuwa na kiongozi mwanamke anayewaza na kutenda kama binadamu kuliko kuwa na kiongozi mwanamke anayewaza na kutenda kwa kujaribu kuwaonesha wanaume kwamba yupo sawa na wanaume au ni zaidi ya wanaume.

Na mwisho
…ningependa swali lako uniulize kwamba je kuna mwanamke ambaye yupo tayari kuongoza Tanzania(kwa maana ya uwezo), na sio kama watanzania wapo tayari kuongozwa na rais mwanamke? Kwani kwa mtindo huo mwingine atakuja na kuuliza je Watanzania wapo tayari kuongozwa na Mmasai, mchagga, Mngoni n.k. Wengine watasema je Tanzania ipo tayari kuendelea kuongozwa na Mkristo/Muisilamu/Mkatoriki.n.k. Au wengine watasema je Tanzania ipo tayri kuongozwa na mtu wa kusini/Kaskazini/magharibi/Mashariki….nk. Matokeo ya huo mvurugano nadhani yapo wazi sina haja ya kuyaelezea hapa

Najumuisha hoja yangu kwa kusema suala ni uwezo wa huyo atayekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kujali jinsia yake, dini yake, kabila lake, au kule anakotokea(nikimanisha eneo) au Chama chake.
Asante komrade Luteni...tuendelee kulumbana kwa hoja.
Asante kibavu kwa maoni yako na mimi niwie radhi nitakujibu kwa kuzunguka.

Kwenye uchaguzi uliopita wa Marekani ushindani mkubwa ulionekana ni wa ndani ya chama cha Democrats zaidi ya ule wa vyama vya Demo na Rep. kuna wakati wamarekani walisema mgombea yeyote wa Democrats kati ya Obama na Hillary atakayeshinda ndiye atakayekuwa rais. Wanachama wa Demo na wananchi wakawa na hisia tofauti kwa sababu yeyote atakayeshinda kwenye primaries kati ya Obama na Hillary historia ya marais wa Marekani itakuwa imewekwa yaani kama Obama atashinda Marekani itakuwa na rais mwenye asili ya kiafrika Mweusi na kama Hillary atashinda atakuwa rais mwanamke wa kwanza. Swala likaja kwa wananchi je Wamarekani wako tayari kuongozwa na mwanamke au kuongozwa na mwanamme mweusi? wewe mwenyewe unaweza kumalizia jibu lake.

Nitakujibu kwa mpangilio wako jinsi ulivyoutoa

Mosi, kwa vile umesema unadhani mgombea anaweza kuwa mwanamke na mimi nakubaliana na wewe kwa mantiki yako lakini natoa tahadhari kama CCM watalazimisha kama walivyofanya kwa spika matokeo yake yatakuwa si mazuri kwa upande wao kama watavyotegemea.

Pili, Kama Nyerere alisema mgombea atakayeteuliwa na CCM tayari atakuwa rais that was then and this is now mazingira aliyosemea ni tofauti kabisa na ya leo mfano bunge aliloliacha Nyerere si hili tunaloliona na chama alichokiacha si hiki tunachokiona.

Tatu, hadi leo Afrika tuna rais mwanamke mmoja kati ya nchi zaidi ya 50, kwanini, mfumo dume wa utemi tuliorithi bado una nguvu sana sisemi kuwa mwanamke hana uwezo lakini umwinyi bado mwingi sana hasa kwa nchi za kiafrika, hata wanawake wenyewe kwa wenyewe bado wakiwekwa pamoja watakwaruzana nakuhakikishia wakiwekwa wagombea wawili mwanamke na mwanamme wanawake wako radhi kumchagua mwanamme kuliko mwanamke mwenzao.
 
Dr.wa ukweli halinganishwi na hao waliokwisha chafuka,EL huyu hakuna asiyejua uchafu alionao, H.mwinyi, anatembea na damu za watanzania aliowaua kwa mabomu gongo la mboto mara mbili na mbagala ni jeuri alitakiwa saa hizi awe anavua samaki kwao au awe jela anakula dona.anaokopa historia ya kujiuzulu kama iliyomtokea baba yake,isitoshe hapa hakuna kurithishana urais hatutaki,wa ukweli njia nyeupeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!
 
Mgombea wa CHADEMA sawa na inawezekana akawa zito Kabwe au yoyote ndani ya CDM kwani wanaamini wote wanauwezo,lakini hawa wa CCM ni majina tu uwezo wa kuongoza nchi hii kuitoa katika limbwi la ufisadi,mikataba mibovu,wizi wa rasilimali za umma n.k ambayo yameigubika CCM hadi kujivua gamba hawa hawawezi sanasana itakuwa ni kulinda maslahi ya mafisadi papa ndani ya chama.wenye uwezo wapo wengi sana lakini hawapewi nafasi kwakuwa hawana fedha za kujitangaza.hii nchi anatakiwa mtu kama Marehemu Mwanawasa wa Zambia ambae haangalii sura.yeye ni kufagia tu.huyo ndiye Rais ajae.na tuombe mungu ajitokeze mwenye sifa za kutokuwa mwoga.wakimzingua anaunda chama chake kama Mbingu wa mutharika wa huko Malawi huyo ndiyo tunaemtaka na siyo hawa tayari ni possesed.
 
Katika wote hao, Lowasa ndiye anaitaji miujiza kuwa rais! Watanzania wameamka kuliko wengi tunavyofikiria.

Ni kweli kachafuka, lakini anafaa mara Trillion kuliko huyo Hussein Mwinyi....
 
Dr.wa ukweli halinganishwi na hao waliokwisha chafuka,EL huyu hakuna asiyejua uchafu alionao, H.mwinyi, anatembea na damu za watanzania aliowaua kwa mabomu gongo la mboto mara mbili na mbagala ni jeuri alitakiwa saa hizi awe anavua samaki kwao au awe jela anakula dona.anaokopa historia ya kujiuzulu kama iliyomtokea baba yake,isitoshe hapa hakuna kurithishana urais hatutaki,wa ukweli njia nyeupe!
Unasema EL amechafuka lakini anaonekana ana wafuasi wengi, utafanyaje, unasema pia Hussein Mwinyi anatembea na damu ya mabomu lakini baada ya kuteuliwa na chama chake, chama ndicho kitakuwa na wajibu wa kumpigia kampeni na kumsafisha kwa gharama yeyote.
 
Wakuu msishangae kwa nini nimewajibu kwa pamoja ni kwa sababu wote mmeonekana kuwa na maoni yanayofanana kuhusu Mwinyi Jr lakini naomba sababu kwanini mnasema hafai na je mnamaoni gani ikiwa atapendekezwa na chama chake.

Mkuu labda utusaidie wewe ni Wizara gani ambayo huyu Bwana alishawahi kuiongoza kwa Ufanisi..
Mabomu ya Mbagala yameua ndugu zetu yeye akiwa Waziri wa Ulinzi, akaahidi halitatokea tena..
Mabomu ya Gongolamboto yakaua tena chini ya Uongozi wake, badala ya kujadili namna ya kupambana na tatizo akawa anakimbilia kusema kuwa hatajiuzulu.. Si ni bora Lowasa alikubali kuwajibika, kuliko huyu Mroho wa Madaraka aliyewekwa madarakani kwa sababu ya jina la Baba'ke..
 
Nimeandika sababu zangu kwa kifupi sana lakini nafikiri zinabeba maana kubwa believe me.

.................Vote for Dr. W. Slaa .........................OR ...........Vote for Hon. H Mwinyi ........ OR.......... Vote For Hon E. Lowassa
images
......................
images
......................
images


..............Chadema Candidate................................................... CCM Candidate............................... Independent Candidate

......Serikali ya Utawala wa Sheria na Haki...................... Serikali ya Umoja na Mshikamano................... Serikali ya Uwajibikaji

Una maoni gani kati ya haya majina matatu ni yupi unayempa asilimia kubwa na kwa sababu gani kama kwa haya majina matatu hakuna unayehisi ni mgombea anayefaa ni yupi unayeona atafaa na kwa sababu zipi, natanguliza shukurani.

we ni mwanasiasa??
uchaguzi uliopita ulikua lini?? sio 2010??
uchaguzi ujao ni lini?? sio 2015
fanya japo kwanza kazi basi, mpaka 2015 tuone tutakua tumefika wap!
ikfika wakati huo ndotutmjua nanai anafaa sio sasa.
huu ni wakati wa kutumikia miaka mingine mitano kwa maendeleo binafsi na maendeleo ya taifa.
 
Mimi nilmetoa sababu moja (muwajibikaji) ingawa ni ya jumla nyie mna sababu zipi.

Ni mthubutu..
Nakumbuka jinsi alivyojitahidi kuifumua NUWA ya wakati ule akiwa waziri wa Maji kama sikosei..
Nakumbuka mkakati wake wa kuhakikisha anawapatia maji safi wakazi wanaozunguka ziwa Viktoria kutoka chanzo cha ziwa Victoria..
Tangu alipoondoka madarakani Serikali yetu imefyata mkia na mkwara wa Misri..
 
Asante kibavu kwa maoni yako na mimi niwie radhi nitakujibu kwa kuzunguka.

Kwenye uchaguzi uliopita wa Marekani ushindani mkubwa ulionekana ni wa ndani ya chama cha Democrats zaidi ya ule wa vyama vya Demo na Rep. kuna wakati wamarekani walisema mgombea yeyote wa Democrats kati ya Obama na Hillary atakayeshinda ndiye atakayekuwa rais. Wanachama wa Demo na wananchi wakawa na hisia tofauti kwa sababu yeyote atakayeshinda kwenye primaries kati ya Obama na Hillary historia ya marais wa Marekani itakuwa imewekwa yaani kama Obama atashinda Marekani itakuwa na rais mwenye asili ya kiafrika Mweusi na kama Hillary atashinda atakuwa rais mwanamke wa kwanza. Swala likaja kwa wananchi je Wamarekani wako tayari kuongozwa na mwanamke au kuongozwa na mwanamme mweusi? wewe mwenyewe unaweza kumalizia jibu lake.

Nitakujibu kwa mpangilio wako jinsi ulivyoutoa

Mosi, kwa vile umesema unadhani mgombea anaweza kuwa mwanamke na mimi nakubaliana na wewe kwa mantiki yako lakini natoa tahadhari kama CCM watalazimisha kama walivyofanya kwa spika matokeo yake yatakuwa si mazuri kwa upande wao kama watavyotegemea.

Pili, Kama Nyerere alisema mgombea atakayeteuliwa na CCM tayari atakuwa rais that was then and this is now mazingira aliyosemea ni tofauti kabisa na ya leo mfano bunge aliloliacha Nyerere si hili tunaloliona na chama alichokiacha si hiki tunachokiona.

Tatu, hadi leo Afrika tuna rais mwanamke mmoja kati ya nchi zaidi ya 50, kwanini, mfumo dume wa utemi tuliorithi bado una nguvu sana sisemi kuwa mwanamke hana uwezo lakini umwinyi bado mwingi sana hasa kwa nchi za kiafrika, hata wanawake wenyewe kwa wenyewe bado wakiwekwa pamoja watakwaruzana nakuhakikishia wakiwekwa wagombea wawili mwanamke na mwanamme wanawake wako radhi kumchagua mwanamme kuliko mwanamke mwenzao.
.


Luteni nimependa sana majibu yako na ukomavu wa hoja ulizotoa….majibu yangu nimeyatoa kwa wino uliokozwa (bolded font) mbele ya kila hoja yako.

Mosi, kwa vile umesema unadhani mgombea anaweza kuwa mwanamke na mimi nakubaliana na wewe kwa mantiki yako lakini natoa tahadhari kama CCM watalazimisha kama walivyofanya kwa spika matokeo yake yatakuwa si mazuri kwa upande wao kama watavyotegemea…..Katika hili itategemea pia watachezaje karata zao. Inaweza pia ikawa ndio mwanzo wa kuzaliwa Tanzania mpya eidha yenye MATUMAINI au yenye minyukano ya kiitikadi na ghasia. Tuombe uzima tuwepo 2015, na Muumba aendelee kuibariki Tanzania tufike hiyo 2015, maana kwa hali ilivyo lolote laweza tokea kabla ya 2015.

Pili, Kama Nyerere alisema mgombea atakayeteuliwa na CCM tayari atakuwa rais that was then and this is now mazingira aliyosemea ni tofauti kabisa na ya leo mfano bunge aliloliacha Nyerere si hili tunaloliona na chama alichokiacha si hiki tunachokiona. ….Nakubaliana na wewe katika hili, lakini pia kumbuka mimi na wewe ni sehemu ndogo sana ya watanzania hivyo mitazamo yetu haitoshi kutoa tathmini ya hali halisi. Unaweza kuwa umeona kwenye chaguzi zetu kwamba kuna wagombea walibebwa na chama zaidi na sio kukubalika kwao, mifani ipo mingi na wewe unaweza kuwa unaifahamu. Pili kama ulivyojibu kwenye hoja yako hapo juu kuhusu mpambano ndani ya democrat hali bado yaweza kuwa hivyo ndani ya CCM 2015. Pia kumbuka hao wamama wawili kwa mujibu wa rekodi za UN ndio wanawake Waafrika walioweza kufika ngazi za juu kabisa kwenye Umoja wa Mataifa.

Tatu, hadi leo Afrika tuna rais mwanamke mmoja kati ya nchi zaidi ya 50, kwanini, mfumo dume wa utemi tuliorithi bado una nguvu sana sisemi kuwa mwanamke hana uwezo lakini umwinyi bado mwingi sana hasa kwa nchi za kiafrika, hata wanawake wenyewe kwa wenyewe bado wakiwekwa pamoja watakwaruzana nakuhakikishia wakiwekwa wagombea wawili mwanamke na mwanamme wanawake wako radhi kumchagua mwanamme kuliko mwanamke mwenzao……..Katika hili Mfumo dume sio Africa tu kwani hata Marekani pamoja na majigambo yao kwamba wana haki sawa, bado hawajaweza kuwa na mwanamke alifikia hata kuwa Makamu wa Rais. Lakini kila historia huwa ina mwanzo wake hivyo mshindi anaweza kutokea Chama cha Upinzani kwa mara ya kwanza au akawa mwanamke kwa mara ya kwanza.
Nawasilisha
 
Back
Top Bottom