m_kishuri
JF-Expert Member
- Jan 27, 2010
- 1,484
- 372
Haya wanajamii, leo ni tarehe 7 Dec. Nadhani ni wakati muafaka wa kujiwekea maazimio muhimu kwa kwa ajili ya kuyafanyia kazi katika mwaka wa 2011. Binafsi sidhani kama kuna ubaya wowote, kwani kama wahenga wasemavyo, penye nia pana njia.
Kwa mwaka ujao (2011) nimeadhimia yafuatayo:
1. Kuitunza afya yangu, na nitaanza kwa kujiunga na GYM iliyokaribu na hapa kwangu. Nimeazimia kupoteza, kwa uchache kilo 15. Check !
2. Nimeazimia kwamba 2011 niongeze bambino wa pili, kwani kila nikijiangalia kwenye kioo naona umri unazidi kula jogging. CHECK !
3. Nimeazimia 2011 uwe mwaka wa amani na upendo kwa ndugu na jamaa ambao umeme ulikuwa haupiti, kwani nimegundua kwamba ugomvi na wanandugu unaathiri afya yangu. CHECK !
5. Nimeazimia kwamba katika mwaka 2011 ntakuwa mwaminifu kwa mama bambino wangu ! Lakini hapa ntahitaji msaada kutoka kwa wakina dada, haswa wale mashujaa walionikumbusha kwamba nina mtu nyumbani. CHECK !
6. Nimeadhimia kuacha kuacha FEGs na MASANGA, kwa sababu nimegundua kwamba hivi vitu viwili vinaendeleza umaskini na kuboronga afya yangu. Hayo ndio yangu kwa 2011. Je, ni nini maazimio yako ya 2011 ?
Kwa mwaka ujao (2011) nimeadhimia yafuatayo:
1. Kuitunza afya yangu, na nitaanza kwa kujiunga na GYM iliyokaribu na hapa kwangu. Nimeazimia kupoteza, kwa uchache kilo 15. Check !
2. Nimeazimia kwamba 2011 niongeze bambino wa pili, kwani kila nikijiangalia kwenye kioo naona umri unazidi kula jogging. CHECK !
3. Nimeazimia 2011 uwe mwaka wa amani na upendo kwa ndugu na jamaa ambao umeme ulikuwa haupiti, kwani nimegundua kwamba ugomvi na wanandugu unaathiri afya yangu. CHECK !
5. Nimeazimia kwamba katika mwaka 2011 ntakuwa mwaminifu kwa mama bambino wangu ! Lakini hapa ntahitaji msaada kutoka kwa wakina dada, haswa wale mashujaa walionikumbusha kwamba nina mtu nyumbani. CHECK !
6. Nimeadhimia kuacha kuacha FEGs na MASANGA, kwa sababu nimegundua kwamba hivi vitu viwili vinaendeleza umaskini na kuboronga afya yangu. Hayo ndio yangu kwa 2011. Je, ni nini maazimio yako ya 2011 ?