DSN
JF-Expert Member
- Feb 2, 2011
- 2,837
- 1,674
Binafsi mimi si shabiki wala Mwanachama Wa Chama Chochote cha kisiasa, lakini swala la siasa linanihusu kwa kuwa SIASA ni sehemu ya maisha yangu kama ilivyo kwa Mwananchi yoyote yule aliye raia wa Tanzania.Kwa kuwa katiba ya Jamhuri Ya Muungano Ya Tanzania 1977 inatoa fursa ya kila raia kushiriki katika harakati za uchaguzi wa viongozi wake, iwe ni kwa yeye kuchaguliwa kuongoza watanzania wenzie ngazi yoyote ile ama yeye kuchagua kiongozi wa kumuongoza yeye mchaguaji katika ngazi yoyote ile.
Katika hatua tuliyonayo sasa binafsi natamani kuona mbio za uchaguzi wa mwaka huu 2015 katika nafasi ya Urais iwe ni kati ya Mwanaccm Kwa Jina la Charles Julius Kambarage Nyerere [CJ] dhidi ya Mwanachadema ambae pia ni Mwanaukawa DK Wilbrod Slaa [WS] nafasi ya juu ya uongozi kwa Taifa zikiwa na sura ya wafuatao kama endapo watajitokeza kuomba na wao kupewa baraka na vyama vyao kuwa na dhamana ya kichama na kupewa kukimbiza mbio za vijiti vya URAIS WA TANZANIA toka kizazi kimoja kwenda kingine.
Ukiacha makando kando ya maswala binafsi watajwa wana sifa bora na toshelezi za kuongoza Taifa kwa kiwango chenye utoshelezi wa kusimamia maono [Vision] yao dhidi ya kile wanacho kiamini bila kuyumba.
Sifa nzuri ya Rais bora ni uwezo wa kusikiliza wengi na kuchambua mawazo mengi aliyosikia na kuibuka yeye binafsi na wazo bunifu toka kwenye shauri tolewa na kutoa jibu sahihi kwa wakati huo na kusonga mbele kwa hatua nyingine.
Ukibisha Waangalie Charles Na Slaa Nyuso Zao,kisha kumbuka wosia wa Baba wa Taifa kwamba tukikuangalia usoni tuseme huyu nae....akimaanisha kuwa kile unachokitetea na kukisema tunaweza kukisoma kwenye sura ya msemaji na wapokeaje wakaamini bila wasiwasi kuwa yasemwayo na msemaji wako pamoja nae kuyasema na kuyatete popote pale.
Charles na Slaa ni aina ya watu wenye HAIBA ya kuweza kusema hili ni Koleo na sio kuwa Koleo ni Kijiko Kikubwa.Taifa liko katika hatua [Stage] ambayo Watanzania wamepata mwamko kiasi wa Kidemokrasia na sasa wanapaswa kupata fursa ya mwamko na mafanikio ya Kiuchumi yanayoendana na ustawi wa maisha bora kwa kila Mwananchi mmoja mmoja na hatimae kwa Taifa.
Ukiacha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, viongozi wengine waliofuata baada yake walijenga uchumi wa kitanzania kutoka juu kuja chini.Hii ni sawa na kusema waliangalia uchumi wa uwekezaji wenye kuangalia multi nations companies na matajiri wawekezaji wa ndani kuja kuinvest Nchini na kutoa fursa ya wakubwa hao toka juu kuwa na hati milki ya uchumi.Kwa style hiyo uchumi mkubwa wa Taifa ukamea mikononi mwa aina fulani ya kundi la Wafanyabiashara wa ndani na wa nje, na baadhi yao wakishirikiana na Viongozi waliopata fursa kupitia siasa iliyo wawezesha kupata mitaji.
Kwa kuwa hapa tulipo ni majibu ya matokeo au mazao ya mambo makuu mawili makubwa kutokea kwa wakati mmoja yani Mageuzi ya Siasa [East & West Politics /Cold War] na Uchumi [The Comming of Globalization] Duniani. Hayo yakitokea Taifa kama Taifa halikuwa limejiandaa kwa mageuzi hayo. Yani Taifa linabadilisha utawala [Administration] kutoka kwa muasisi wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, huku akiwa na maono ambayo kwa nyakati hizo yalikuwa yanakinzana na baadhi ya siasa za kimataifa, siasa ambazo Muasisi wa Taifa akiamini katika siasa za UJAMAA WA KIAFRIKA, lakini changamoto zilizo mbele ya Rais mpokea kijiti ni siasa zinazosukuma Taifa na Mataifa mengi Duniani kuegemea siasa za Uchumi wa Soko huru [Tafsiri Ruksa] .
Ni kwa siasa hizo ambazo Taifa kwa umri wake na msimamo wa mjenzi wa kwanza wa Msingi wa Taifa viliibua changamoto kubwa sana kisiasa na uchumi kiasi kuwa hata ulipofika muda kuwa Taifa liingie kwenye mfumo wa vyama vingi [Multi-Partism] asilimia karibia 80% walisema hapana Taifa lisiingie Kwenye vyama vingi.Lakini kwa maono ya muasisi wa Taifa alitoa ushauri kwa Taifa kuwasikiliza asilimia 20% na leo tuko hapa.
Changamoto zote tulizopita kama Taifa ambazo pia zilipelekea baadhi ya viongozi wetu kuhalalisha kutekeleza mageuzi ya Kisiasa na Uchumi [Polical & Economic Justification] kwa namna ambayo wao waamuaji waliona inafaa ama kuzingatia au kutozingatia maslahi ya Taifa kwa ujumla wake. Ni kwa baadhi ya maamuzi hayo ambayo mengine yalitendwa kwa kutozingatia misingi iiyowekwa na MUASISI [FOUNDER] basi Taifa limepita kwenye misukosuko ya Kisiasa na Kiuchumi ambayo walio wengi wana matamanio ya kuona Watanzania wote wakiwa wamepiga hatua kimaisha kama ambavyo walifundishwa wakiwa chini ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kuwa kupitia juhudi zao kwa pamoja wapige vita maadui wakuu wa Taifa ili wajiletee maendeleo yao wenyewe.
Tulipofika kama Taifa kumepatikana maendele ya vitu [Material things] kutoka tulipo Taifa laitaji Kiongozi atakewekeza kwenye utawala utakao simamia na kutoa USTAWI wa Taifa [Standard of Living] toka ngazi ya mtu mmoja kwenda kwenda ngazi ya Taifa kwa ujumla wake.Hii ni kuanzia ngazi ya mtu mmoja mmoja, familia, jamii, kikundi cha watu na kwa ujumla wake kama Taifa zima.Ni muda ambao Taifa linaitaji aina ya kiongozi atakae zingatia uchumi wa kutoka chini kwenda juu.Uchumi ambao unampa fursa raia wa kawaida Mtanzania kushiriki kwenye ujenzi wa Uchumi wa Taifa lake kwa kuzingatia vigezo vya HAKI na fursa zenye viwezesho na vinavyo kidhi vigezo stahiki na ufanisi wenye kuhesabika kwa kila mmoja.
Ustawi wa mtu mmoja mmoja [Standard of Livingi ] hauwezi kupatikana kama Taifa halina MISINGI YA HAKI NA MIIKO....ustawi wa Taifa kwa kukosa hayo upoteza UWAJIBIKAJI, RUSHWA NA UFISADI, USHAMILI, MAOVU USTAWI, MAADILI UPOTEA, UZALENDO UPATA NAJISI, CHUKI NA UONGO USTAWI, HUDUMA UGEUKA KUWA HISANI, UCHOYO NA UBINAFSI UPATA KIBALI NA KUSTAWI, HOFU YA MUNGU UTOWEKA, UZEMBE NA UVIVU UTAMALAKI, MALALAMIKO NA MIGOGOLO ISIYOKWISHA UPATA HIFADHI NDANI YA JAMII, USALAMA NA AMANI UGEUKA KUOMBWA BADALA YA KUWA NI TABIA MIOYONI MWA WANANCHI, HESHIMA NA UNDUGU WA KIAFRIKA UPOTEZA MWELEKO, KIBULI NA MAJIVUNO UJENGA MASKANI KWENYE OFISI NA MAJUMBANI,
Hayo na mengineyo tajwa yanaitaji mtu mwenye JICHO la ndani asiye na mawaa bali ukimuona USONI unakili moyoni kuwa huyu akisema RUSHWA HAIPENDI basi kweli Rushwa inatoweka haraka.
Kwa miongo mitatu 3 [3 decade] sisi kama Taifa tulifundishwa na watawala kuendesha maisha yetu kiuchumi tukiwa tumezingatia sana uchumi wa soko huru [Free Market] -chini ya kivuli cha uwekezaji. Sasa ni muda mwafaka na tosha sana kama Taifa kuachana na Uchumi wa majaribio na kujikita kwenye fursa ya uchumi inayozingatia namna gani Mtanzania atastawi yeye na familia yake kwa kupitia maliasili alizo nazo Mtanzania.Rais ajae awe ni Rais anae kerwa na mfumo wa maisha ya mlo wa Mtanzania, afya yake, Kazi zake, Elimu yake, Makazi yake, na kwa kero hizo awe na kiu ya kubolesha maisha yao kwa kiwango ambacho Mtanzania akilinganishwa na Mataifa mengine Afrika basi awe ni namba moja na Taifa la kuigwa kuwa Tumewezaje.Kinachostawisha maisha ya watu ni SERA [POLICY] huku sera hizo zikiwa na usimamizi thabiti toka juu mpaka ngazi ya chini ya uongozi.Usimamizi wa sera zisizo zaa madaraja wala dhuruma dhidi ya mwingine bali utoaji wa fursa zenye mazingira ya kumwinua Mtanzania ngazi yoyote ile toka Mkulima wa Kilosa Morogoro mpaka Mmachinga wa Kariakoo Dar es Salaam.
Kama kwa CCM Charles hatojitokeza basi wafuatao wanaweza kidogo kusimama nyuma yake..
1: Magufuri 2: Benard Membe 3: Steven Wasira
Kwa Ukawa Vs Chadema
1: Aikael P Mbowe 2: Ibrahim Lipumba -ingawa anamezwa na tulivyojingea watanzania.
Ni Mtizamo..Tu...Get Ready
Katika hatua tuliyonayo sasa binafsi natamani kuona mbio za uchaguzi wa mwaka huu 2015 katika nafasi ya Urais iwe ni kati ya Mwanaccm Kwa Jina la Charles Julius Kambarage Nyerere [CJ] dhidi ya Mwanachadema ambae pia ni Mwanaukawa DK Wilbrod Slaa [WS] nafasi ya juu ya uongozi kwa Taifa zikiwa na sura ya wafuatao kama endapo watajitokeza kuomba na wao kupewa baraka na vyama vyao kuwa na dhamana ya kichama na kupewa kukimbiza mbio za vijiti vya URAIS WA TANZANIA toka kizazi kimoja kwenda kingine.
Ukiacha makando kando ya maswala binafsi watajwa wana sifa bora na toshelezi za kuongoza Taifa kwa kiwango chenye utoshelezi wa kusimamia maono [Vision] yao dhidi ya kile wanacho kiamini bila kuyumba.
Sifa nzuri ya Rais bora ni uwezo wa kusikiliza wengi na kuchambua mawazo mengi aliyosikia na kuibuka yeye binafsi na wazo bunifu toka kwenye shauri tolewa na kutoa jibu sahihi kwa wakati huo na kusonga mbele kwa hatua nyingine.
Ukibisha Waangalie Charles Na Slaa Nyuso Zao,kisha kumbuka wosia wa Baba wa Taifa kwamba tukikuangalia usoni tuseme huyu nae....akimaanisha kuwa kile unachokitetea na kukisema tunaweza kukisoma kwenye sura ya msemaji na wapokeaje wakaamini bila wasiwasi kuwa yasemwayo na msemaji wako pamoja nae kuyasema na kuyatete popote pale.
Charles na Slaa ni aina ya watu wenye HAIBA ya kuweza kusema hili ni Koleo na sio kuwa Koleo ni Kijiko Kikubwa.Taifa liko katika hatua [Stage] ambayo Watanzania wamepata mwamko kiasi wa Kidemokrasia na sasa wanapaswa kupata fursa ya mwamko na mafanikio ya Kiuchumi yanayoendana na ustawi wa maisha bora kwa kila Mwananchi mmoja mmoja na hatimae kwa Taifa.
Ukiacha Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, viongozi wengine waliofuata baada yake walijenga uchumi wa kitanzania kutoka juu kuja chini.Hii ni sawa na kusema waliangalia uchumi wa uwekezaji wenye kuangalia multi nations companies na matajiri wawekezaji wa ndani kuja kuinvest Nchini na kutoa fursa ya wakubwa hao toka juu kuwa na hati milki ya uchumi.Kwa style hiyo uchumi mkubwa wa Taifa ukamea mikononi mwa aina fulani ya kundi la Wafanyabiashara wa ndani na wa nje, na baadhi yao wakishirikiana na Viongozi waliopata fursa kupitia siasa iliyo wawezesha kupata mitaji.
Kwa kuwa hapa tulipo ni majibu ya matokeo au mazao ya mambo makuu mawili makubwa kutokea kwa wakati mmoja yani Mageuzi ya Siasa [East & West Politics /Cold War] na Uchumi [The Comming of Globalization] Duniani. Hayo yakitokea Taifa kama Taifa halikuwa limejiandaa kwa mageuzi hayo. Yani Taifa linabadilisha utawala [Administration] kutoka kwa muasisi wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, huku akiwa na maono ambayo kwa nyakati hizo yalikuwa yanakinzana na baadhi ya siasa za kimataifa, siasa ambazo Muasisi wa Taifa akiamini katika siasa za UJAMAA WA KIAFRIKA, lakini changamoto zilizo mbele ya Rais mpokea kijiti ni siasa zinazosukuma Taifa na Mataifa mengi Duniani kuegemea siasa za Uchumi wa Soko huru [Tafsiri Ruksa] .
Ni kwa siasa hizo ambazo Taifa kwa umri wake na msimamo wa mjenzi wa kwanza wa Msingi wa Taifa viliibua changamoto kubwa sana kisiasa na uchumi kiasi kuwa hata ulipofika muda kuwa Taifa liingie kwenye mfumo wa vyama vingi [Multi-Partism] asilimia karibia 80% walisema hapana Taifa lisiingie Kwenye vyama vingi.Lakini kwa maono ya muasisi wa Taifa alitoa ushauri kwa Taifa kuwasikiliza asilimia 20% na leo tuko hapa.
Changamoto zote tulizopita kama Taifa ambazo pia zilipelekea baadhi ya viongozi wetu kuhalalisha kutekeleza mageuzi ya Kisiasa na Uchumi [Polical & Economic Justification] kwa namna ambayo wao waamuaji waliona inafaa ama kuzingatia au kutozingatia maslahi ya Taifa kwa ujumla wake. Ni kwa baadhi ya maamuzi hayo ambayo mengine yalitendwa kwa kutozingatia misingi iiyowekwa na MUASISI [FOUNDER] basi Taifa limepita kwenye misukosuko ya Kisiasa na Kiuchumi ambayo walio wengi wana matamanio ya kuona Watanzania wote wakiwa wamepiga hatua kimaisha kama ambavyo walifundishwa wakiwa chini ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kuwa kupitia juhudi zao kwa pamoja wapige vita maadui wakuu wa Taifa ili wajiletee maendeleo yao wenyewe.
Tulipofika kama Taifa kumepatikana maendele ya vitu [Material things] kutoka tulipo Taifa laitaji Kiongozi atakewekeza kwenye utawala utakao simamia na kutoa USTAWI wa Taifa [Standard of Living] toka ngazi ya mtu mmoja kwenda kwenda ngazi ya Taifa kwa ujumla wake.Hii ni kuanzia ngazi ya mtu mmoja mmoja, familia, jamii, kikundi cha watu na kwa ujumla wake kama Taifa zima.Ni muda ambao Taifa linaitaji aina ya kiongozi atakae zingatia uchumi wa kutoka chini kwenda juu.Uchumi ambao unampa fursa raia wa kawaida Mtanzania kushiriki kwenye ujenzi wa Uchumi wa Taifa lake kwa kuzingatia vigezo vya HAKI na fursa zenye viwezesho na vinavyo kidhi vigezo stahiki na ufanisi wenye kuhesabika kwa kila mmoja.
Ustawi wa mtu mmoja mmoja [Standard of Livingi ] hauwezi kupatikana kama Taifa halina MISINGI YA HAKI NA MIIKO....ustawi wa Taifa kwa kukosa hayo upoteza UWAJIBIKAJI, RUSHWA NA UFISADI, USHAMILI, MAOVU USTAWI, MAADILI UPOTEA, UZALENDO UPATA NAJISI, CHUKI NA UONGO USTAWI, HUDUMA UGEUKA KUWA HISANI, UCHOYO NA UBINAFSI UPATA KIBALI NA KUSTAWI, HOFU YA MUNGU UTOWEKA, UZEMBE NA UVIVU UTAMALAKI, MALALAMIKO NA MIGOGOLO ISIYOKWISHA UPATA HIFADHI NDANI YA JAMII, USALAMA NA AMANI UGEUKA KUOMBWA BADALA YA KUWA NI TABIA MIOYONI MWA WANANCHI, HESHIMA NA UNDUGU WA KIAFRIKA UPOTEZA MWELEKO, KIBULI NA MAJIVUNO UJENGA MASKANI KWENYE OFISI NA MAJUMBANI,
Hayo na mengineyo tajwa yanaitaji mtu mwenye JICHO la ndani asiye na mawaa bali ukimuona USONI unakili moyoni kuwa huyu akisema RUSHWA HAIPENDI basi kweli Rushwa inatoweka haraka.
Kwa miongo mitatu 3 [3 decade] sisi kama Taifa tulifundishwa na watawala kuendesha maisha yetu kiuchumi tukiwa tumezingatia sana uchumi wa soko huru [Free Market] -chini ya kivuli cha uwekezaji. Sasa ni muda mwafaka na tosha sana kama Taifa kuachana na Uchumi wa majaribio na kujikita kwenye fursa ya uchumi inayozingatia namna gani Mtanzania atastawi yeye na familia yake kwa kupitia maliasili alizo nazo Mtanzania.Rais ajae awe ni Rais anae kerwa na mfumo wa maisha ya mlo wa Mtanzania, afya yake, Kazi zake, Elimu yake, Makazi yake, na kwa kero hizo awe na kiu ya kubolesha maisha yao kwa kiwango ambacho Mtanzania akilinganishwa na Mataifa mengine Afrika basi awe ni namba moja na Taifa la kuigwa kuwa Tumewezaje.Kinachostawisha maisha ya watu ni SERA [POLICY] huku sera hizo zikiwa na usimamizi thabiti toka juu mpaka ngazi ya chini ya uongozi.Usimamizi wa sera zisizo zaa madaraja wala dhuruma dhidi ya mwingine bali utoaji wa fursa zenye mazingira ya kumwinua Mtanzania ngazi yoyote ile toka Mkulima wa Kilosa Morogoro mpaka Mmachinga wa Kariakoo Dar es Salaam.
Kama kwa CCM Charles hatojitokeza basi wafuatao wanaweza kidogo kusimama nyuma yake..
1: Magufuri 2: Benard Membe 3: Steven Wasira
Kwa Ukawa Vs Chadema
1: Aikael P Mbowe 2: Ibrahim Lipumba -ingawa anamezwa na tulivyojingea watanzania.
Ni Mtizamo..Tu...Get Ready