My confession: Nilipenda niwe daktari nikashindwa, nimebakiza heshima kwao.

Mjenda Chilo

JF-Expert Member
Jul 20, 2011
1,467
513
Nilijitahidi kusoma Pcb ili nikasome muhimbili medicine nikachemka, hata nilipokuwa Bcom bado nilire-seat biology mambo yakagoma. Nikaachana na udaktari lkn nikapitia wateule wa kozi hiyo nikakutana na A za kumwaga kwenye results zao. Nikaamini kumbe kichwa bora zaidi kwa maana ya matokeo ndo huchaguliwa pale. Nikaangalia kama kuna mtu wa combination za HGE,ECA,HGL,EGM nk sikuwakuta nakutana na hasahasa kitu cha pcb, nikacheki class kwetu nikawakuta pcb,pcm,egm,hge nk tumo. Nikaamini mwili wa binadamu kweli umepewa heshima stahiki. Nikawapigia saluti jamaa zangu walioanza course ya medicine, baada ya miaka 3 nikamaliza na kupata kakazi kangu na kamshahara kangu na mara kagari mara kauwanja nk. baada ya miaka mitatu nikaenda muhimbili pale chuo nakutana na jamaa yangu ndo ameanza internship. Akanizungusha mawodini nakutana na mazingira halisi ya hospitali zetu. Jamaa akaniambia hapa ndo ofisini kwangu, basi nikavuta picha ya ofisi yangu, kiyoyozi mazingira nk. Nikamwambia hongera naona uko busy na ofisi yako na ndo maana mi ninawaheshimu sana. Nikauliza vp mnapwaje lkn? Sio mbaya sana akanijibu kwa upole na kuniomba tuagane nae. Naiomba serikali yangu, mimi siwezi kulalamika eti flan analipwa kidogo ukilinganisha na dr, ntalalamika pale mlinzi wa Tra atakapomzidi mshahara mwalimu basi. Chonde chonde kaeni na hawa ma Dr na muwaongezee halali ya toka mioyoni mwao na mwetu angalieni mpunguze wapi na hata kama ni kidogo muwaongezee jamani watu tunakufaa. My confession!
 
Bado una nafasi ya kuwa Daktari mkuu.Vyuo viko vingi siku hizi..Kairuki,IMTU,India nk nk..Msuli wako tu
 
Usijaribu kuitamani hii fani. Ni fani ya kishenzi sana. Katika mafunzo walimu wanaringa, wanatukana wanafunzi na wanaviburi sana. Ukweli ni kwamba hii course ya udaktari hauna raha kuanzia unaposoma hadi kazini. Mimi najuta sana kuja kusomea hii course.Kuna dr mmoja katika chuo kimoja huko kanda ya ziwa kazi yake ni kutukana tu wanafunzi wodini badala ya kufundisha. Wewe acha tu ndugu yangu, kama ulisoma Bcom nakuomba uendelee ukasome MBA accounts utakula nchi bila pressure. Good luck.
 
Pole sana. Ungetafuta "path of least resistance" to prosperity ie the siasa path....... African context bila shaka.
 
Heri wewe mtoa post ulieshindwa na ukaamua kuwaheshimu.
Kuna wengne waliposhindwa kuwa madaktari wakajenga chuki na taaluma na wanataaluma wa udaktari, ht wapewapo nafasi za kufanya maamuzi kwa ma Dr, huwakomoa tu!
 
HA HA HAA, KAKA POLE SANA, NAONA ULIUTAKA UDAKTARI KWELI. MATOKEO YA FORM SIX JAMAA WAWILI MZUMBE WALIPATA DIV. 1.3 (A A A- PCB), MMOJA AKAENDA KUSOMA PHARMACY NA MWINGINE B.COM. NAOMBA NIHIFADHI MAJINA WANAJAMVI. SIDHANI KAMA HAWA WATAKUWA NA CHUKI ZAIDI YA KUSHANGILIA UAMUZI WAO KWANI JAMAA WANAMSHIKO WA HATARI SANA.
KI UKWELI, SERIKALI INAPOTEZA WATU MAKINI SANA AMBAO KWA SASA HAWAENDI KUSOMEA UDAKTARI, ESPECIALLY MIAKA YA 2005 MPAKA SASA, MADOGO WANACHANA NA WANASEPA B.COM, BAF, NK. SASA WANAKULA KUKU, NOBLE PROFESSIONALS KAMA MD. SERIKALI INALETA UTANI! INATIA HASIRA SANA MKUU. Pole mkuu kwa kukosa kuitwa Dr. kapige PhD ili uitwe tu man, hata hiyo MD bado unaweza kupiga, siku hizi vyuo vingi man!
 
Back
Top Bottom