Mjenda Chilo
JF-Expert Member
- Jul 20, 2011
- 1,467
- 513
Nilijitahidi kusoma Pcb ili nikasome muhimbili medicine nikachemka, hata nilipokuwa Bcom bado nilire-seat biology mambo yakagoma. Nikaachana na udaktari lkn nikapitia wateule wa kozi hiyo nikakutana na A za kumwaga kwenye results zao. Nikaamini kumbe kichwa bora zaidi kwa maana ya matokeo ndo huchaguliwa pale. Nikaangalia kama kuna mtu wa combination za HGE,ECA,HGL,EGM nk sikuwakuta nakutana na hasahasa kitu cha pcb, nikacheki class kwetu nikawakuta pcb,pcm,egm,hge nk tumo. Nikaamini mwili wa binadamu kweli umepewa heshima stahiki. Nikawapigia saluti jamaa zangu walioanza course ya medicine, baada ya miaka 3 nikamaliza na kupata kakazi kangu na kamshahara kangu na mara kagari mara kauwanja nk. baada ya miaka mitatu nikaenda muhimbili pale chuo nakutana na jamaa yangu ndo ameanza internship. Akanizungusha mawodini nakutana na mazingira halisi ya hospitali zetu. Jamaa akaniambia hapa ndo ofisini kwangu, basi nikavuta picha ya ofisi yangu, kiyoyozi mazingira nk. Nikamwambia hongera naona uko busy na ofisi yako na ndo maana mi ninawaheshimu sana. Nikauliza vp mnapwaje lkn? Sio mbaya sana akanijibu kwa upole na kuniomba tuagane nae. Naiomba serikali yangu, mimi siwezi kulalamika eti flan analipwa kidogo ukilinganisha na dr, ntalalamika pale mlinzi wa Tra atakapomzidi mshahara mwalimu basi. Chonde chonde kaeni na hawa ma Dr na muwaongezee halali ya toka mioyoni mwao na mwetu angalieni mpunguze wapi na hata kama ni kidogo muwaongezee jamani watu tunakufaa. My confession!