My Birthday

Paw

Content Manager
Nov 14, 2010
2,109
1,360
Desemba 02 ya kila mwaka ni tarehe ambayo miongoni mwa wengi waliozaliwa siku hiyo, basi mimi kamtu kadoogo kasiko na umuhimu sana nilizaliwa.

Yes namshukuru Mwenyezi Mungu kwa yote, ameniongoza katika mengi ambayo leo nikigeuka nyuma siamini kama nilipita kule. Nakumbuka incident moja ambapo nilichelewa kupata usafiri wa kurudi nyumbani (Hadi saa nne usiku) kutoka shamba enzi hizo Changanyikeni (nyuma ya UDSM) na usafiri ulikuwa ni uda pekee. Nililazimika siku hiyo kulala juu ya mkorosho shambani maana nilikuwa naogopa mno muumiani hadi nikashindwa kuomba hifadhi kokote. Sitasahau siku hiyo maana usiku sikulala vizuri na nilishuhudia vitu kadhaa vitendekavyo usiku...

Kumbukumbu yangu ya kuzaliwa sitahitaji zawadi yeyote zaidi kwani yanayotukia serikalini katika safisha safisha ni zaidi ya zawadi kwangu.

Nawatakia heri nyote ambao siku kama ya leo mlizaliwa.

Naishukuru JF kipekee kwa kunikuza kifikra na kimsimamo.

Zawadi kwa King'ast wangu ni kuwa "Baby I will come home early today"
 
Last edited by a moderator:
Happy birthday dogo... Tumezaliwa mwezi mmoja lakini tumepishana siku saba...
 
aiss pole Paw ndo unaelekea kumaliza life span yako
 
Last edited by a moderator:
Heri ya kuzaliwa Bw. Mod!!! Mimi na mrs wangu tunasubiria mualiko kwenye kukata cake...
 
Happy birthday Paw.

Hiyo uda ilikuwa ya dala?
 
Last edited by a moderator:
Happy Birthday Paw, kindly receive our happy birthday wishes from me and my sweet pie NN.
Happy Birthday enjoy the day with your loved ones.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom