My Apology to JamiiForums, by Chris Lukosi

Status
Not open for further replies.

Chris Lukosi

JF-Expert Member
Aug 23, 2012
4,581
2,937
Ndugu zanguni,

Kwanza kabisa napenda kumtakia Maxence Melo afya njema na namuombea Mungu amponye haraka majeraha aliyopata kwenye ajali ya gari.

Kama mjuavyo hakuna binadamu alie sawa asilimia mia hapa duniani.
Kila mtu ana mampungufu yake na mimi pia nina mapungufu yangu.

Kwa namna moja au nyingine, Jana niliwakwaza Wamiliki wa JF hapa na baadhi ya members hapa jukwaani.

Tunajua kuwa kila mtanzania ana haki ya kuongea atakacho lakini cha muhimu ni kuzingatia kuwa huwaharibii siku wenzako au kwa lugha nyingine usiwakwaze wengine.

JF ni jukwaa huru pekee Tanzania ambalo linatumiwa na watu wa kila aina hapa kuanzia mawaziri mpaka wakulima vijijini wenye access kwenye mtandao.

Ndugu zanguni, tukae tukijua kuwa kila tunachoandiaka hapa kinabaki hapa na kinasomwa na wengi na kila mtu anakipokea kivyake. Jf wametupatia jukwaa la siasa ili wanasiasa na wengineo tuweze kulitumia kukosoana na kupeana za uso ikibidi, lakini mimi binafsi niliteleza kidogo na kuwahusisha JF kwenye siasa.

Nilifanya kosa kuwatuhumu JF kuwa wanatumiwa na Dr Slaa na Freeman kushinikiza nipigwe ban lakini leo nimegundua ni kauli yangu mwenyewe iliyosababisha ban kwani ni hawa hawa JF walioniruhusu nitumie jukwaa kuwarushia madongo ya uso Dr Slaa na Freeman bila kujali kuwa nao watakuwa na feelings kuwa mimi napendelewa hapa JF kwa kuwa nimeachiwa niwapige madongo ya ukweli. Bila kusahau jamaa yangu Lema.

Nimejifunza kitu kimoja.

JF ni kama mpira, kila mtu anaona ameonewa, na pia ni kama centre ya mizani ambapo wapinzani huzani mzani unapendelea uzito wa upande mwingine.

Nawashauri verified user wenzangu tujibishane kwa kuzingatia hoja na tuachane na siasa za majitaka.
Pia nawashauri kama mnaona mmeonewa au hamjui sheria za JF basi muingie hapa(LINK 1 - JamiiForums Rules na LINK 2 Topic gani hufungwa au kufutwa kabisa JF? )

Nawaomba radhi Mods na wamiliki wa JF kwa kuwakwaza

Na pia nawaomba members wenzangu wote radhi kama nimewakwaza, WENGI MNAJUA MIMI NI MHEHE HIVYO SOMETIMES HUWA NASHINDWA KUJIZUIA, ukileta za kuleta nakupa za uso mwisho wake wote tunakuwa kama wasyria tu. na ninawashauri tusitumie jazba kwenye mahojiano tunapochangia hoja, matusi hayajengi bali yanleta chuki tu na nadhani members wenzangu pia watajitambua kama mimi.
1176228100KzEdD5.jpg


JITAMBUE!
 
Ndo ulivyo na hutobadilika, njano haiwezi kuwa nyekundu
Sasa mkuu nimeomba msamaha bado unakataa ,
Kweli tutafika? nyie ndio kama wale wa syria, hamtaki suluhu mnataka kuuana tu.
Maisha ni kusameheana, mtu akikubali kosa unamsamehe lkaa sivyo utanyonga wote ubaki peke yako duniani kama shetani tu
 
Umekuwa kama mtu aliyetolewa pepo wachafu hivi..unaomba msamaha kwa nguvu kama vile akili haikuwa yako wakati huo..
 
Unakaribishwa kwa moyo mweupe na roho ya ridhaa, Mie binafsi sina soneneko. Mkuu unakubalika kwa ushujaa wako.
Good luck ...
 
Dah jamaa anajpgia promo, kwanza cjui ni nan katka nin? Mlamba viatu na mpga debe wa familia ya mfalme unayesubir huruma ya wanaccm wachache wanaoifaid nchi waishio masaki. Utakufa vbaya acha ukondakta wenzako wanakung'ong'a.
 
my apologise....
Kwa hiyo wewe hufanya siasa za majitaka kwa makusudi? Yaani huu ni 'umbuni' kweli kweli.

Halafu acha upuuzi wa kuusingizita 'uhehe' wako pindi unashindwa kuJidhibiti.
 
Sasa mkuu nimeomba msamaha bado unakataa ,
Kweli tutafika? nyie ndio kama wale wa syria, hamtaki suluhu mnataka kuuana tu.
Maisha ni kusameheana, mtu akikubali kosa unamsamehe lkaa sivyo utanyonga wote ubaki peke yako duniani kama shetani tu

Sijaona msamaha ulioomba hapa zaidi ya kuendeleza makorokocho yako.

Siku zako zinahesabika ndani ya CCM, waulize wenzako.
 
Unaomba msamaha na ndani yake unapiga majungu yasiyokuwa na tija kwa kuongea mambo ya kinafiki. Kitendo hicho si cha kiungwana bali unadhihirisha ni jinsi gani unavyotumika pasipo kushughulisha akili yako.
 
hizo sentence tatu za mwisho zinaonyesha wazi kwamba wala hukuwa na nia ya kuomba msamaha bali kujionyesha who you are.Kuna sig humu inasema"ficha upumbavu wako"am not a politician ila umenikera ulivyoandika
 
makubwaaaaa


muhehe na siasa za maji taka...

vipi umeumizwaaaa na ccm nini...

ulifikiri utalipwaaaa

heheheeeeee...wenzio wanagonga na kudansi hao unaowafanyia maji taka..


sisi wa chini ndio tutaishia kuwa maadui tu, wao akhaaaa......wako round table wana gonga glasi


chezea siasa za bongo wewe.
 
Status
Not open for further replies.
16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom