#COVID19 Mwongozo wa Serikali kukabiliana na UVIKO katika Nyumba za Ibada

Informer

JF-Expert Member
Jul 29, 2006
1,582
6,627
Nyumba za ibada zikaguliwe mara kwa mara na kuhakikisha zinazingatia yafuatayo;

  • Ziweke vifaa vya kunawia mikono (maji safi tiririka na sabuni au Vitakasa mikonoSanitizers) na muumini atakaye simamia unawaji kwa wote.
  • Waumini wavae Barakoa
  • Waumini wakae umbali unaozidi mita moja kutoka mtu mmoja hadi mwingine pande zote.
  • Taratibu za kufanya usafi na utakasaji wa viti, meza na maeneo wanapokaa kabla na baada ya ibada ufanyike.
  • Alama katika viti ziwekwe kuonyesha umbali wa mita moja.
  • Wazee, Watoto na wale wote wenye matatizo ya kiafya yanayotambulika (Mfano. Kisukari, Shinikizo la Damu, Kansa n.k), wanashauriwa kujiepusha na ibada zenye mikusanyiko ya Watu wengi na wachukue tahadhari zote muda wote
  • Kama nyumba ya ibada ni ndogo uanzishwe utaratibu wa kusalia nje/maeneo ya wazi au kuongeza idadi ya vipindi vya ibada na kuruhusu idadi ya watu wachache kuingia ibadani na kuzingatia uvaaji wa Barakoa.
  • Ibada ziwe za muda mfupi usiozidi masaa mawili.
  • Huduma zinazohusisha kugusana ziepukwe
  • Kuwepo na ujumbe wa mara kwa mara kwa ajili ya kuwakumbusha waumini kuhusu namna ya kujikinga na UVIKO-19 na namba za kuwasiliana na huduma za afya iwapo atapatikana mgonjwa.
 
Usharika wangu wa nyumbani wanafanya hivyo tangu hii kitu imeanza.

Ila huu ugonjwa ni kipimo tosha Cha Imani.

Hapa Mungu anapata kazi rahisi sana kutambua wale waumini maslahi na halisi.

Yaani kipimo kidogo tu kwisha habari yake.
 
Serikali njooni mumuone Askofu Gwajima yeye anahamasisha watu wake wasivae mabarakoa wala sanitaiza🤣🤸‍♂️🐒
 
Muongozo original upo type tu muongozo wa UVICO 19 leo ni page 7 kila kundi limeelezewa kinagaubaga
 
Usharika wangu wa nyumbani wanafanya hivyo tangu hii kitu imeanza.

Ila huu ugonjwa ni kipimo tosha Cha Imani.

Hapa Mungu anapata kazi rahisi sana kutambua wale waumini maslahi na halisi.

Yaani kipimo kidogo tu kwisha habari yake.
Na kwenye kipindupindu na malaria hapimi? Mbona mnatumia neti au wakati wa kipundupindu mnafuata kanuni? Kwa nini mmechagua ugonjwa mmoja tu uwe ndiyo kipimo cha Mungu?
 
Na kwenye kipindupindu na malaria hapimi? Mbona mnatumia neti au wakati wa kipundupindu mnafuata kanuni? Kwa nini mmechagua ugonjwa mmoja tu uwe ndiyo kipimo cha Mungu?
Kuna mtu anaingia kwenye nyumba ya Ibada na neti??

Ngoma ipo hapo ;

Unamuamini Mungu au kipande Cha kitambaa??

As simple as that.
 
Kuna mtu anaingia kwenye nyumba ya Ibada na neti??

Ngoma ipo hapo ;

Unamuamini Mungu au kipande Cha kitambaa??

As simple as that.
Kwenye nyumba za ibada hakuna mbu. Kwani Mungu yuko kwenye nyumba za Ibada tu?
 
Mama awe serious asiwaache wapuuzi wapoteze watu....kamata Gwajima huyo anavuruga nchi
 
Usharika wangu wa nyumbani wanafanya hivyo tangu hii kitu imeanza.

Ila huu ugonjwa ni kipimo tosha Cha Imani.

Hapa Mungu anapata kazi rahisi sana kutambua wale waumini maslahi na halisi.

Yaani kipimo kidogo tu kwisha habari yake.
Ccm mmejaa wajinga. Yaani Mungu apate kazi rahisi kutambua waumini?
 
Gaidi Mbowe yupo chini ya ulinzi salama wa Polisi, nchi nzima imetulia hakuna matukio ya ajabu ajabu kama Uamsho walivyowekwa sehemu salama na Zenji ikatulia.
 
Ccm mmejaa wajinga. Yaani Mungu apate kazi rahisi kutambua waumini?
Haha

Vitabu vya dini vilishasema haya


Yaani binadamu anavyojiona mwerevu Kwa Mungu sio kitu.

Ndio maana ikaandikwa wataourithi ufalme wa Mbingu ni wale wataokuwa na akili kama za watoto wadogo.

Huwezi nielewa Kwa sasa ila ukiwa motoni utanikumbuka.
 
Usharika wangu wa nyumbani wanafanya hivyo tangu hii kitu imeanza.

Ila huu ugonjwa ni kipimo tosha Cha Imani.

Hapa Mungu anapata kazi rahisi sana kutambua wale waumini maslahi na halisi.

Yaani kipimo kidogo tu kwisha habari yake.
Protocols zote za C-19 zina nia ya ku-endorse ushetani.Hili liko wazi mkuu.Ni ajabu kwamba hata wale wanaojiita watumishi wameshindwa kuona ukweli huu.Obviously fikra zao zimepofushwa na Shetani.Very sad.Ni vipofu wanao ongoza vipofu,na Biblia inasema wote wataanguka shimoni.
 
Nyumba za ibada zikaguliwe mara kwa mara na kuhakikisha zinazingatia yafuatayo;

  • Ziweke vifaa vya kunawia mikono (maji safi tiririka na sabuni au Vitakasa mikonoSanitizers) na muumini atakaye simamia unawaji kwa wote.
  • Waumini wavae Barakoa
  • Waumini wakae umbali unaozidi mita moja kutoka mtu mmoja hadi mwingine pande zote.
  • Taratibu za kufanya usafi na utakasaji wa viti, meza na maeneo wanapokaa kabla na baada ya ibada ufanyike.
  • Alama katika viti ziwekwe kuonyesha umbali wa mita moja.
  • Wazee, Watoto na wale wote wenye matatizo ya kiafya yanayotambulika (Mfano. Kisukari, Shinikizo la Damu, Kansa n.k), wanashauriwa kujiepusha na ibada zenye mikusanyiko ya Watu wengi na wachukue tahadhari zote muda wote
  • Kama nyumba ya ibada ni ndogo uanzishwe utaratibu wa kusalia nje/maeneo ya wazi au kuongeza idadi ya vipindi vya ibada na kuruhusu idadi ya watu wachache kuingia ibadani na kuzingatia uvaaji wa Barakoa.
  • Ibada ziwe za muda mfupi usiozidi masaa mawili.
  • Huduma zinazohusisha kugusana ziepukwe
  • Kuwepo na ujumbe wa mara kwa mara kwa ajili ya kuwakumbusha waumini kuhusu namna ya kujikinga na UVIKO-19 na namba za kuwasiliana na huduma za afya iwapo atapatikana mgonjwa.
Huo muongozo upo katika nyumba za ibada tu ama hata katika maeneo mbalimbali yenye mikusanyiko ya watu. Muongozo unasemaje kuhusu usafiri wa umma, matamasha, makongamano, semina, warsha, maeneo ya michezo na burudani, mbio za mwenge wa Uhuru, mikutano ya kisiasa ya CCM na mengine kama hayo.
 
Haha

Vitabu vya dini vilishasema haya


Yaani binadamu anavyojiona mwerevu Kwa Mungu sio kitu.

Ndio maana ikaandikwa wataourithi ufalme wa Mbingu ni wale wataokuwa na akili kama za watoto wadogo.

Huwezi nielewa Kwa sasa ila ukiwa motoni utanikumbuka.
Kwa hiyo "wapiga risasi watu na waweka watu kwenye viroba" wataenda peponi? Sawa bhana, naona hata Mungu mnadhani mnaweza kumtisha kama mnavyotutisha sisi raia wa Tanganyika. Mtamtisha tu kuwa na yeye akileta fyokovyoko mtamzima then atawaachia lango la peponi muingie kama mnavyoingia na masanduku kwenye vituo vya kupigia kura hahahahaha.
 
pia wang'oe siti za kwenye magari, daladala na mabasi maana hazijazingatia mita 1 na zaidi. isiruhusiwe daladala wala basi la abiria kubeba watu maana siti zimewekwa umbali wa chini ya robo mita
 
Back
Top Bottom