Mwongozo juu matumizi ya "Loud Speakers" kwenye Nyumba za Ibada katikati Makazi ya raia

Kiresua

JF-Expert Member
May 13, 2009
1,184
259
Wana JF,

Habari za leo hii,

Kwa muda sasa nimekuwa nikijiuliza juu ya suala hili la matumizi ya loud speakers kwenye nyumba za ibada (Makanisa na Misikiti) yaliyoko katikati ya makazi ya watu. Hivi kuna sheria yoyote au mwongozo unaolekekeza juu ya hili? I beg to remain neutral kwa hili.

Utakuta mtu kajinunulia residentian plot anaweka nguzo nne, turubai juu annazisha kanisa (hapa amebadilisha matumizi), halafu anakesha mwenyewe na familia yake huku akiwa amefungulia spika hadi mwisho usiku kucha! au Msikiti uko katikati ya makazi ya watu asubuhi na mapema baada kuwaamsha watu kwa adhana, wanaendelea kuomba kwenye loud speakers bika kujali kuwa wamezungukwa na waumuni wa imani nyingine ambao hawahitaji kuamshwa kwa sauti za maombi/sala zinazofanyika makanisani au misikitini!

Kwa kweli najiuliza sana hivi hakuna mwongozo juu ya hilli katika nchi yetu yenye utulivu wa kiimani?

Naomba tujadili hili ila kama kuna mwongozo basi tupate mwangaza namna ya kuwasukuma watawala/viongozi wetu kuchukua hatua stahiki, au kama mwongozo hakuna basi tuone namna ya kunzisha machakato wa kurekebisha hili.

Ikizingatiwa kuwa katika katiba ya Nchi
Na. 19.-(1) Kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, imani na uchaguzi katika mambo ya dini, pamoja na uhuru wa mtu kubadilisha dini au imani yake.
(2) Bila ya kuathiri sheria zinazohusika za Jamhuri ya Muungano, kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza
dini itakuwa ni huru na jambo la hiari ya mtu ya binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.

kwa tafsiri yangu katika neno "huru" haimaanishi kiholela, matakwa na uhuru wa mtu mwingine haupaswi kuingiliwa kwa shughuli huru za kidini, ndio maana tunaelekezwa kuwa, kumbi za sherehe ziwe na sound proof, ili unapofurahi usibugudhi wengine kwa nao wanahijaji na wanayo haki ya kupata utulivu.

Karibuni Wana Taifa!
 
Ninavyofahamu katika sheria za Halmashauri na Manispaa zetu ipo sheria inayozuia sauti za namna ambazo zinakoseha utulivu sehemu za makazi na webgine wanaita "sound pollution". Hata madisko yanawekewa taratibu za kupiga miziki yao. Hili ni suala ambalo Halmashauri na Manispaa wanaweza kulishughulikia.
 
binafsi nakereka sana na hizi kelele ,nafikiri pia ni huku mjini sana maana dini hizi zimegeuka biashara ndio wanapiga makelele sana kuit watu,ila tuseme kweli ukikaa karibu na hizi nyumba za ibada ni keroo sana.mjini maisha magumu umelala saa sita ,kumina oja watu wanapiga kengele zao wengine weekend unasema upumzike ndio mikesha imeanza yaani its so purukushani ni kero sana.
 
Ninavyofahamu katika sheria za Halmashauri na Manispaa zetu ipo sheria inayozuia sauti za namna ambazo zinakoseha utulivu sehemu za makazi na webgine wanaita "sound pollution". Hata madisko yanawekewa taratibu za kupiga miziki yao. Hili ni suala ambalo Halmashauri na Manispaa wanaweza kulishughulikia.

mkuu' serikali yenyewe ndo chanzo cha hayo makelele. Manspaa ya Ilala siku hizi inakodisha ukumbi wa Karimjee hall' na pia na makumbusho ya taifa nao wanafanya hivyo, eneo la uwanja kwa nje kwa harusi, sendoff, kitchen p. n.k, makelele mtindo moja mpaka usiku wa manane, hasa siku za mwisho wa juma, na ukumbuke maeneo haya yamezungukwa na taasisi mbalimbali, hospitali ya Ocean road, Chuo cha IFM na cha Utalii, ofisi za bunge, na Ikulu haiko mbali na eneo hili, pia apartments za makazi. Je kama wenyewe wanashindwa kutii sheria, unafikiri wataweza kusimamia ili haki itendeke?
 
Sio dini tu pamoja na baa. Baa zinapiga kelele sana kwa muziki hasa siku wana promotion. Ni udhia mtupu. Halmashauri inapaswa kutoa kanuni ya baa zote ziwe soundproof.
 
wana jf,

habari za leo hii,

kwa muda sasa nimekuwa nikijiuliza juu ya suala hili la matumizi ya loud speakers kwenye nyumba za ibada (makanisa na misikiti) yaliyoko katikati ya makazi ya watu. Hivi kuna sheria yoyote au mwongozo unaolekekeza juu ya hili? I beg to remain neutral kwa hili.

Utakuta mtu kajinunulia residentian plot anaweka nguzo nne, turubai juu annazisha kanisa (hapa amebadilisha matumizi), halafu anakesha mwenyewe na familia yake huku akiwa amefungulia spika hadi mwisho usiku kucha! Au msikiti uko katikati ya makazi ya watu asubuhi na mapema baada kuwaamsha watu kwa adhana, wanaendelea kuomba kwenye loud speakers bika kujali kuwa wamezungukwa na waumuni wa imani nyingine ambao hawahitaji kuamshwa kwa sauti za maombi/sala zinazofanyika makanisani au misikitini!

Kwa kweli najiuliza sana hivi hakuna mwongozo juu ya hilli katika nchi yetu yenye utulivu wa kiimani?

Naomba tujadili hili ila kama kuna mwongozo basi tupate mwangaza namna ya kuwasukuma watawala/viongozi wetu kuchukua hatua stahiki, au kama mwongozo hakuna basi tuone namna ya kunzisha machakato wa kurekebisha hili.

Ikizingatiwa kuwa katika katiba ya nchi
na. 19.-(1) kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, imani na uchaguzi katika mambo ya dini, pamoja na uhuru wa mtu kubadilisha dini au imani yake.
(2) bila ya kuathiri sheria zinazohusika za jamhuri ya muungano, kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza
dini itakuwa ni huru na jambo la hiari ya mtu ya binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.

Kwa tafsiri yangu katika neno "huru" haimaanishi kiholela, matakwa na uhuru wa mtu mwingine haupaswi kuingiliwa kwa shughuli huru za kidini, ndio maana tunaelekezwa kuwa, kumbi za sherehe ziwe na sound proof, ili unapofurahi usibugudhi wengine kwa nao wanahijaji na wanayo haki ya kupata utulivu.

Karibuni wana taifa!
nimependa hoja yako lakini niongezee na hili la watu kubadili matumizi na kuweka bar . Makelele usiku mzima kwa wale tunao kaa sinza kila mtaa una bar na wanakesha. Usiku maeneo ya afrika sana sinza watu wanapiga kelele usiku kucha ni makazi ya watu lakini makahaba wamebadili matumizi
 
ni changamoto yetu sote tuifanyie kazi kwa kufuata sheria halali,taratibu na miongozo yetu!
 
Wakati nakaa tabata kimanga kwa kelele hizo tulifankiwa kumuhamisha mchungaji peter nyaga kutoka kenya aliyekuja kuanzisha kanisa lake na njia tulizotumia ni za kisheria
Mkuu Remote , hebu funguka zaidi na sisi tupate tujifunze kutoka kwenu. Mlifanya nini (eg mlitumia sheria gani) mpaka mkafanikiwa?
 
Last edited by a moderator:
Kelele ktk baadhi ya nyumba za Ibada na nyumba za starehe ni kero sana,nadhani itakuja sababisha mapambano! Mimi naona ni kielelezo cha utawala ulioshindwa ambao unaogopa kuwadhibiti wavunja sheria.
 
uko sahihi sana mkuu
mchungaji mwenyewe ana kiburi cha ajabu
bahati nzuri hakimu wa kesi yenu hakukubali rushwa,alimtia hatiani
alihamia tabata changombe kwenye bar moja pale
makelele yale yale, alihonga manispaa ya Ilala na hata mkurugenzi alimkingia kifua
tena Mkenya yule wanasheria wa manispaa wakakubali kumlinda, hana kibali cha kufanya kazi nchini.
cha kushangaza usiku kwenye hilo kanisa lake wanalala humo humo wake kwa waume kinachofanyika ndani Mungu anajua
chunguzeni kuna mwingine nae yuko Tegeta mpare moja hivi zamani alikuwa na kashfa kibao ikiwemo ujambazi
eti sasa ni mchungaji,maajabu

chungezeni wachungaji wote wa vichochoroni ni wa Kenya au waKOngo na lengo lao kuvuna hela na sio mahubiri.
inafaa saa wananchi kuamka wenyewe kuwatimua kwa njia yoyote since rushwa imetawala.
utashangaa hadi usiku wanapiga muziki na makelele
tu umetoka kazini umechoka watoto hawawezi kulala.Mungu gani huyo anaekubali usumbufu??
Wakati nakaa tabata kimanga kwa kelele hizo tulifankiwa kumuhamisha mchungaji peter nyaga kutoka kenya aliyekuja kuanzisha kanisa lake na njia tulizotumia ni za kisheria
 
SMU kila manispaa inasheria zake nendeni manispaa husika mtapata maelezo.
 
SMU kila manispaa inasheria zake nendeni manispaa husika mtapata maelezo.

Hizi maispaa zetu zinazosubiri mpaka wanachi walalamike ni kero tupu!

Lakini Mkuu naona kwa sababu tatizo hili ni la kitaifa, naona kuna umuhimu wa serikali kuu kuja na mwongozo, kuna taarifa kuwa Rwanda walishapiga marufuku makelele usiku!! ibada zinafanyika ndani ya majumba ya ibada bila kuasthiri utendaji wa watu walio nje!
 
ni kweli mkuu
nadhani suala la kuruhusu wapi pajengwe bar au grocery au ukumbi wa disco au kanisa na msikikiti bado liko chini ya serikali za mitaa na sio serikali kuu
sina hakika kama kuna Pullution Act kwani sound ni pollution pia
suala hili kama watoa lesseni limeachiwa manispaa au halmashauri
wananchi sasa kuwasilisha kero huko ili zifanyiwe kazi
tatizo rushwa kwani wanasheria wa manispaa wanashikishwa rushwa hizo na kukaa kimpya
Hizi maispaa zetu zinazosubiri mpaka wanachi walalamike ni kero tupu!

Lakini Mkuu naona kwa sababu tatizo hili ni la kitaifa, naona kuna umuhimu wa serikali kuu kuja na mwongozo, kuna taarifa kuwa Rwanda walishapiga marufuku makelele usiku!! ibada zinafanyika ndani ya majumba ya ibada bila kuasthiri utendaji wa watu walio nje!
 
Kenge nyiee kila mtu anauhuru kama unakaa kimya nyumbani kwako tulia na uboya wako, Wanao kesha baa waache wanywe nchi yetu inaendeshwa na pato la pombe, Waislamu waacheni ndo wanamwabudu Mungu HATA Wakristo muwaacheni wakeshe usiku haijari wanakaaje kanisani. Wekama hukeshi niliboya tuu hunalolote.
 
Kenge nyiee kila mtu anauhuru kama unakaa kimya nyumbani kwako tulia na uboya wako, Wanao kesha baa waache wanywe nchi yetu inaendeshwa na pato la pombe, Waislamu waacheni ndo wanamwabudu Mungu HATA Wakristo muwaacheni wakeshe usiku haijari wanakaaje kanisani. Wekama hukeshi niliboya tuu hunalolote.

Duhh.. Mkuu wee noma!
 
ni kweli mkuu
nadhani suala la kuruhusu wapi pajengwe bar au grocery au ukubi wa disco au kanisa na msikikiti bado liko chini ya serikali za mitaa na sio serikali kuu
sina hakika kama kuna Pullution Act kwani sound ni pollution pia
suala hili kama watoa lesseni limeachiwa manispaa au halmashauri
wananchi sasa kuwasilisha kero huko ili zifanyiwe kazi
tatizo rushwa kwani wanasheria wa manispaa wanashikiswa rushwa hizo na kukaa kimpya

ni shida kubwa sana, Manispaa zetu hazina nguvu kabsa!!
 
mkuu bado una hang over ya jana?
pole sana amka ukachape kazi
Kenge nyiee kila mtu anauhuru kama unakaa kimya nyumbani kwako tulia na uboya wako, Wanao kesha baa waache wanywe nchi yetu inaendeshwa na pato la pombe, Waislamu waacheni ndo wanamwabudu Mungu HATA Wakristo muwaacheni wakeshe usiku haijari wanakaaje kanisani. Wekama hukeshi niliboya tuu hunalolote.
 
ki-ukweli kelele zinakera sana hasa kwa makanisa uchwara, wanakwaruza masauti kama majini, wakianza uwezi kulala kuna cku tutawapopoa na mawe, pale tegeta barabarani ndio usiseme, watu hawana kazi wanashinda wamelala kanisani. Baa za makelele bado ndogo sana hawa tunawamudu lakini ukigusa dini wanakuambia wewe ndio shetani, wanasema usilale kwani ujui cku wala saa utakapochukuliwa, kesheni mkiomba bila mwisho.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom