Kiresua
JF-Expert Member
- May 13, 2009
- 1,184
- 259
Wana JF,
Habari za leo hii,
Kwa muda sasa nimekuwa nikijiuliza juu ya suala hili la matumizi ya loud speakers kwenye nyumba za ibada (Makanisa na Misikiti) yaliyoko katikati ya makazi ya watu. Hivi kuna sheria yoyote au mwongozo unaolekekeza juu ya hili? I beg to remain neutral kwa hili.
Utakuta mtu kajinunulia residentian plot anaweka nguzo nne, turubai juu annazisha kanisa (hapa amebadilisha matumizi), halafu anakesha mwenyewe na familia yake huku akiwa amefungulia spika hadi mwisho usiku kucha! au Msikiti uko katikati ya makazi ya watu asubuhi na mapema baada kuwaamsha watu kwa adhana, wanaendelea kuomba kwenye loud speakers bika kujali kuwa wamezungukwa na waumuni wa imani nyingine ambao hawahitaji kuamshwa kwa sauti za maombi/sala zinazofanyika makanisani au misikitini!
Kwa kweli najiuliza sana hivi hakuna mwongozo juu ya hilli katika nchi yetu yenye utulivu wa kiimani?
Naomba tujadili hili ila kama kuna mwongozo basi tupate mwangaza namna ya kuwasukuma watawala/viongozi wetu kuchukua hatua stahiki, au kama mwongozo hakuna basi tuone namna ya kunzisha machakato wa kurekebisha hili.
Ikizingatiwa kuwa katika katiba ya Nchi
Na. 19.-(1) Kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, imani na uchaguzi katika mambo ya dini, pamoja na uhuru wa mtu kubadilisha dini au imani yake.(2) Bila ya kuathiri sheria zinazohusika za Jamhuri ya Muungano, kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza
dini itakuwa ni huru na jambo la hiari ya mtu ya binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.
kwa tafsiri yangu katika neno "huru" haimaanishi kiholela, matakwa na uhuru wa mtu mwingine haupaswi kuingiliwa kwa shughuli huru za kidini, ndio maana tunaelekezwa kuwa, kumbi za sherehe ziwe na sound proof, ili unapofurahi usibugudhi wengine kwa nao wanahijaji na wanayo haki ya kupata utulivu.
Karibuni Wana Taifa!
Habari za leo hii,
Kwa muda sasa nimekuwa nikijiuliza juu ya suala hili la matumizi ya loud speakers kwenye nyumba za ibada (Makanisa na Misikiti) yaliyoko katikati ya makazi ya watu. Hivi kuna sheria yoyote au mwongozo unaolekekeza juu ya hili? I beg to remain neutral kwa hili.
Utakuta mtu kajinunulia residentian plot anaweka nguzo nne, turubai juu annazisha kanisa (hapa amebadilisha matumizi), halafu anakesha mwenyewe na familia yake huku akiwa amefungulia spika hadi mwisho usiku kucha! au Msikiti uko katikati ya makazi ya watu asubuhi na mapema baada kuwaamsha watu kwa adhana, wanaendelea kuomba kwenye loud speakers bika kujali kuwa wamezungukwa na waumuni wa imani nyingine ambao hawahitaji kuamshwa kwa sauti za maombi/sala zinazofanyika makanisani au misikitini!
Kwa kweli najiuliza sana hivi hakuna mwongozo juu ya hilli katika nchi yetu yenye utulivu wa kiimani?
Naomba tujadili hili ila kama kuna mwongozo basi tupate mwangaza namna ya kuwasukuma watawala/viongozi wetu kuchukua hatua stahiki, au kama mwongozo hakuna basi tuone namna ya kunzisha machakato wa kurekebisha hili.
Ikizingatiwa kuwa katika katiba ya Nchi
Na. 19.-(1) Kila mtu anastahili kuwa na uhuru wa mawazo, imani na uchaguzi katika mambo ya dini, pamoja na uhuru wa mtu kubadilisha dini au imani yake.(2) Bila ya kuathiri sheria zinazohusika za Jamhuri ya Muungano, kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza
dini itakuwa ni huru na jambo la hiari ya mtu ya binafsi, na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi.
kwa tafsiri yangu katika neno "huru" haimaanishi kiholela, matakwa na uhuru wa mtu mwingine haupaswi kuingiliwa kwa shughuli huru za kidini, ndio maana tunaelekezwa kuwa, kumbi za sherehe ziwe na sound proof, ili unapofurahi usibugudhi wengine kwa nao wanahijaji na wanayo haki ya kupata utulivu.
Karibuni Wana Taifa!