Mwonekano wa Rais Samia Suluhu likiongezwa hili utakuwa babu kubwa

El Roi

JF-Expert Member
May 29, 2020
263
502
Kuna clip niliwahi kuisikia ya mh Rais wakati akiwa makamu wa Rais akieleza jinsi alivyopitia hatua mbalimbali mpaka kufika alipokuwa.

Moja ya Jambo ktk maongezi yake alilosema ni kuwa kabla ya kwenda kugombea jimbo la Makunduchi, Zanzibar kama mbunge wa jimbo uvaazi wake (dressing code) ulikuwa ni wa kizungu. Nakumbuka anatania kwenye ile clip kwamba ilikuwa ni masuruali, na manywele mpaka huko.

Anasema ni wananchi ndo walimshauri avae kiutamaduni (Kizanzibar hasa) nadhani mantiki ikiwa ni kumfanya akubalike kwenye ile jamii yake.

Na kweli kwa kuvaa vile anaonekana yuko vizuri sana.

Ushauri wangu ni nyongeza tu kwamba kama alivyoshauriwa huko nyuma, hata Sasa naona bado mantiki ipo kwamba, wakati anavaa kizungukizungu pia wakati huu itapendeza Sana. Hivyo basi dressing code ya mheshimiwa ikiwa versatile (mchanganyiko) itakuwa nzuri zaidi (Kwa maoni yangu).

Kwa wataalamu wa mwonekano(presentableness) tayari Rais naturally ni presentable, hivyo akiongeza mwonekano tofautitofauti wa uvaaji, siyo tu kwamba ataonekana anavutia bali ushawishi (influence) itaongezeka kwa makundi tofauti tofauti ya kijamii.
Vinginevyo nampongeza Rais wangu. She is quite composed and humane looking.

I can't wait to seeing my president, if this can happen, being versatile in dressing code.

Wasalaam.
 
hata Sasa naona bado mantic ipo kwamba, wakati anavaa kizungukizungu pia wakati huu itapendeza Sana. Hivyo basi dressing code ya mheshimiwa ikiwa versatile ( mchanganyiko) itakuwa nzuri zaidi.( Kwa maoni yangu).
Safi sana Mkuu kwa ushauri na ni ushauri mzuri.
 
Mimi ningelikuwa Model nyuzi kama hizi za kujinga Ningekupiga Lifeban!
Yani Watu wanawaza namna bora ya kuijenga Tanzania wewe unaweza maisha yake Binafsi?

Unadhani Maisha bora yanajengwa na Mavazi?
Yani Mwafrika unamuazia avae Kizungu?
Yani ungenyoosha tu maelezo kuwa hutaki Avae kiislamu manake tayari munajipanga na Ajenda ya kumwita ana Udini.

Time Will Tell
[/QUOTE
Naona unapotosha makusudi. Urgue and don't shout.
 
Taarabu za khanga moko na mitindo ya Mwambao zirudishwe Ikulu, vinywaji laini mchana na vikali usiku, Ikulu irejeshewe hadhi yake ya sehemu yenye kupendwa na Watanzania na si sehemu ya kupigwa vibao na mateso mengine
 
Sasa Mkuu kuvaa kizunguzungu si ni hayo masuruali na manguo ya ajabu ajabu? Avae hivyo I'll kumpendezesha Nani? Mabeberu? Mh.Rais aendelee na mavazi yake yaleyale ya heshma na anapendeza Sana.
Jamani dunia ya leo hakuna mabeberu.hili neno limefutika,hata cuba,korea kaskazini,china,urusi n.k hawatumii tena neno hilo.kwa sasa dunia ni kijiji.ndio maana mie na wewe tumeweza kuandika hapa.
 
Mwisho wa siku mtasema tena mbona haambatani na mume wake kila sehemu anako kwenda?

Wabongo bhana!! Sisi tunataka atuletee maendeleo ya watu na vitu, nyinyi mnataka kumuona akitokelezea kizungu! Ili iweje sasa! 🤔
 
Kwaiyo unataka kusema raisi wa jamuhuri ajui kuvaa

SUBIRI KIDOGO
Anavaa vizuri Sana. Na ndivyo nilivyomueleza hapo juu. Ukifuatilia maelezo yangu utagundua haya ni maoni yangu na mantic ni kuongeza vionjo positively kwa mkuu wetu. Umeelewa ndugu?
 
Mimi ningelikuwa Model nyuzi kama hizi za kujinga Ningekupiga Lifeban!
Yani Watu wanawaza namna bora ya kuijenga Tanzania wewe unaweza maisha yake Binafsi?

Unadhani Maisha bora yanajengwa na Mavazi?
Yani Mwafrika unamuazia avae Kizungu?
Yani ungenyoosha tu maelezo kuwa hutaki Avae kiislamu manake tayari munajipanga na Ajenda ya kumwita ana Udini.

Time Will Tell
Model?
 
Back
Top Bottom