nguruka wa kig0ma
JF-Expert Member
- Jan 16, 2020
- 2,946
- 2,929
Saalam wanabodi,
Napata taabu ninapoona mambo yanayotendwa na viongozi na vyombo vya dola vya nchi yetu.
Najiuliza, ivi baba wa taifa Mwl Nyerere ametujenga katika misingi gani?
1. Kizalendo halisi?
2. Nidhabu ya woga?
3. Au machafuko na vita vya majirani zetu vimetupumbaza?
Viongozi wanatuburuta watakavyo, lakini tumekaa kimyaaaa! Na hata tukisema, basi kwa sauti ya unyongeee, kiasi kwamba wanaotuburuta wanajua kuwa hawa tumeshawalegeza.
1. Tunatungiwa sheria za hovyo, za kutuziba midomo na kutukandamiza lakini tupo tu. Shame on us!
2. Pesa zetu zinatumika bila utaratibu, lakini tupo tu!
3. Democracy inabinywa, lakini tupo tu!
4. Watu wanajiwekea kinga za kisheria wasishitakiwe wakitoka madarakani kwakuwa wanajua wanayotenda ni maovu,
lakini sisi tupo tu. PUMBAVU SISI!
5. Tulitaka katiba mpya, pesa nyingi zimetumika, leo hii ukiuliza sababu za kutopata katiba mpya ni nini, majibu yatakuwa haikuwa sera wala kipaumbele changu. Sisi tupo tu!
6. Watu wanatekwa, wanapotezwa na kuuawa, sisi tupo tu. Nk, nk, nk
Hao wanaofanya haya wakitaka tuwachague wanakuja na maneno, kuwa msiwachague wapinzani, isijekuwa kama Burundi, Rwanda au Congo.
Watanzania tunakubali tu!
MWALIMU NYERERE, UMETUJENGAJE? KWENYE UMOJA ULIFANIKIWA, KWENYE KUDAI HAKI ZETU UMETUJENGA KWENYE MSINGI UPI?
INAUMA SANA, TUMEKUWA KAMA SAMAKI KWENYE JARIFE, WANAVUTWA TU, AKIRUKARUKA KUJITETEA ANAPIGWA RUNGU. DAAAAH!
Napata taabu ninapoona mambo yanayotendwa na viongozi na vyombo vya dola vya nchi yetu.
Najiuliza, ivi baba wa taifa Mwl Nyerere ametujenga katika misingi gani?
1. Kizalendo halisi?
2. Nidhabu ya woga?
3. Au machafuko na vita vya majirani zetu vimetupumbaza?
Viongozi wanatuburuta watakavyo, lakini tumekaa kimyaaaa! Na hata tukisema, basi kwa sauti ya unyongeee, kiasi kwamba wanaotuburuta wanajua kuwa hawa tumeshawalegeza.
1. Tunatungiwa sheria za hovyo, za kutuziba midomo na kutukandamiza lakini tupo tu. Shame on us!
2. Pesa zetu zinatumika bila utaratibu, lakini tupo tu!
3. Democracy inabinywa, lakini tupo tu!
4. Watu wanajiwekea kinga za kisheria wasishitakiwe wakitoka madarakani kwakuwa wanajua wanayotenda ni maovu,
lakini sisi tupo tu. PUMBAVU SISI!
5. Tulitaka katiba mpya, pesa nyingi zimetumika, leo hii ukiuliza sababu za kutopata katiba mpya ni nini, majibu yatakuwa haikuwa sera wala kipaumbele changu. Sisi tupo tu!
6. Watu wanatekwa, wanapotezwa na kuuawa, sisi tupo tu. Nk, nk, nk
Hao wanaofanya haya wakitaka tuwachague wanakuja na maneno, kuwa msiwachague wapinzani, isijekuwa kama Burundi, Rwanda au Congo.
Watanzania tunakubali tu!
MWALIMU NYERERE, UMETUJENGAJE? KWENYE UMOJA ULIFANIKIWA, KWENYE KUDAI HAKI ZETU UMETUJENGA KWENYE MSINGI UPI?
INAUMA SANA, TUMEKUWA KAMA SAMAKI KWENYE JARIFE, WANAVUTWA TU, AKIRUKARUKA KUJITETEA ANAPIGWA RUNGU. DAAAAH!