Ilikuwa mida ya saa 9:30 alasiri pale maeneo ya Musoma alliance,wakati huo nikiwa natoka ktk kiwanda cha Mara Oil (nilipokuwa nafanya kibarua ingawaje ilikuwa child labour kwani wakati huo nilikuwa na miaka 16).
Mwalimu alipita na gari yake aina ya Land rover akiwa na dereva wake akamuona mama mmoja pembeni mwa barabara akiwa na ameshikwa na uchungu na hatua za mwisho za kujifungua, mume wake akiwa amesimama pembeni kwani alikuwa akimsindikiza hospitalini kwa baiskeli,hali ilipokuwa mbaya akamshusha ili ijifungue.
Mwalimu akamwamuru dereva kusimamisha gari,akasogea kwa karibu na kumwamuru dereva kumpakia yule mama na kumkimbiza hospitali mara moja. Akampa dereva pesa anunue unga wa ulezi ili utumike kumpikia uji yule mama atakapojifungua.
Mwl yeye akabaki pale barabarani kwenye kona ya Musoma alliance.Magari yakaendelea kupita,yale ya serikali walipokuwa wakimwona mwalimu wanasimama na kutaka kujua kulikoni ikiwezekana aingie kwenye gari.Wote walipewa jibu hili" Nenda,kwani mama aliyekuwa anajifungua hapa hamkumwona?"
Katika siku hii ya leo ya kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha mwl.Nyerere,nimeamua kuwaletea ushuhuda huo juu ya moyo wa utu aliokuwa nao mwalimu.Lakini pia hali ya maisha aliyoishi mwl.
Nani leo hii rais mstaafu anaweza kutumia LandRover Pick up?
Mwalimu alipita na gari yake aina ya Land rover akiwa na dereva wake akamuona mama mmoja pembeni mwa barabara akiwa na ameshikwa na uchungu na hatua za mwisho za kujifungua, mume wake akiwa amesimama pembeni kwani alikuwa akimsindikiza hospitalini kwa baiskeli,hali ilipokuwa mbaya akamshusha ili ijifungue.
Mwalimu akamwamuru dereva kusimamisha gari,akasogea kwa karibu na kumwamuru dereva kumpakia yule mama na kumkimbiza hospitali mara moja. Akampa dereva pesa anunue unga wa ulezi ili utumike kumpikia uji yule mama atakapojifungua.
Mwl yeye akabaki pale barabarani kwenye kona ya Musoma alliance.Magari yakaendelea kupita,yale ya serikali walipokuwa wakimwona mwalimu wanasimama na kutaka kujua kulikoni ikiwezekana aingie kwenye gari.Wote walipewa jibu hili" Nenda,kwani mama aliyekuwa anajifungua hapa hamkumwona?"
Katika siku hii ya leo ya kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha mwl.Nyerere,nimeamua kuwaletea ushuhuda huo juu ya moyo wa utu aliokuwa nao mwalimu.Lakini pia hali ya maisha aliyoishi mwl.
Nani leo hii rais mstaafu anaweza kutumia LandRover Pick up?