504D
Member
- Feb 16, 2013
- 33
- 10
Wilaya ya Magu mkoani Mwanza, hususan Idara ya Elimu Msingi mekuwa ikitajwa sana kwenye uga huu wa JF kutokana na mambo kadha wa kadha kwenda kombo.
Kuna jambo jipya linaloendelea hukohuko Magu linalomhusu Mwl. Mkuu wa Ilungu S/ Msingi Bwn. Mambosasa.
Mwalimu huyu anatuhumiwa kuwadunga mimba wanafunzi wake watatu.
Mabinti hao wamehojiwa na mamlaka na vyombo husika na wametoa maelezo ya kutosha ambayo kwa hakika yanasikitisha!
Maelezo yao ni pamoja na kubainisha kwamba, mwalimu wao huyo alikuwa anawafanyia ufuska wake huo kwenye ofisi yake ya Mwalimu Mkuu; na wakati mwingine alikuwa anawaingiza mabinti wawili kwa mpigo; anamshughulikia mmoja, huku mwenzake akiangalia!
Ni udhalilishaji wa hali ya juu sana ambao umefanywa na mwalimu huyu ambaye ni mlezi; mtumishi wa umma aliyeaminiwa na Jamhuri, tena aliyesomeshwa kuwa mlezi wa watoto wa Taifa hili, akaaminiwa na Mamlaka za Wilaya, Mkurugenzi na Afisa Elimu na mamlaka zingine, anageuka kuwatafuna watoto wasiokuwa na hatia alikoabidhiwa ndani ya ofisi ya umma; badala ya kuwapa elimu, kuwatunza na kuwalinda ili wafikie malengo yao; inaumiza sana.
Mwalimu huyu sasa yuko nguvuni, mamlaka husika zikimhoji kubaini ukweli yakini wa mambo haya ili hatua stahiki zichukuliwe.
Ni matarajio ya waathirika na jamii kwa ujumla kwamba, mamlaka zote zinazohusika katika kushughulikia jambo hili zitatenda yote yapasayo kwa mujibu wa sheria, ili hali itendeke kwa pande zote.
Mwl. Mambosasa asitendewe isivyostahili bila ushahidi madhubuti dhidi yeke, ili tu kuifurahisha jamii inayomtuhumu (Public Interest).
Lakini pia hali ya waathirika lazima ilindwe; kama kuna ushahidi dhahir shahir dhidi ya mtuhumiwa; basi Mambosasa abebe mzigo wake wa mahindi mabichi aliyokula!
Alamsiki.
Kuna jambo jipya linaloendelea hukohuko Magu linalomhusu Mwl. Mkuu wa Ilungu S/ Msingi Bwn. Mambosasa.
Mwalimu huyu anatuhumiwa kuwadunga mimba wanafunzi wake watatu.
Mabinti hao wamehojiwa na mamlaka na vyombo husika na wametoa maelezo ya kutosha ambayo kwa hakika yanasikitisha!
Maelezo yao ni pamoja na kubainisha kwamba, mwalimu wao huyo alikuwa anawafanyia ufuska wake huo kwenye ofisi yake ya Mwalimu Mkuu; na wakati mwingine alikuwa anawaingiza mabinti wawili kwa mpigo; anamshughulikia mmoja, huku mwenzake akiangalia!
Ni udhalilishaji wa hali ya juu sana ambao umefanywa na mwalimu huyu ambaye ni mlezi; mtumishi wa umma aliyeaminiwa na Jamhuri, tena aliyesomeshwa kuwa mlezi wa watoto wa Taifa hili, akaaminiwa na Mamlaka za Wilaya, Mkurugenzi na Afisa Elimu na mamlaka zingine, anageuka kuwatafuna watoto wasiokuwa na hatia alikoabidhiwa ndani ya ofisi ya umma; badala ya kuwapa elimu, kuwatunza na kuwalinda ili wafikie malengo yao; inaumiza sana.
Mwalimu huyu sasa yuko nguvuni, mamlaka husika zikimhoji kubaini ukweli yakini wa mambo haya ili hatua stahiki zichukuliwe.
Ni matarajio ya waathirika na jamii kwa ujumla kwamba, mamlaka zote zinazohusika katika kushughulikia jambo hili zitatenda yote yapasayo kwa mujibu wa sheria, ili hali itendeke kwa pande zote.
Mwl. Mambosasa asitendewe isivyostahili bila ushahidi madhubuti dhidi yeke, ili tu kuifurahisha jamii inayomtuhumu (Public Interest).
Lakini pia hali ya waathirika lazima ilindwe; kama kuna ushahidi dhahir shahir dhidi ya mtuhumiwa; basi Mambosasa abebe mzigo wake wa mahindi mabichi aliyokula!
Alamsiki.