Mwl. Mambosasa S/Msingi Ilungu-Magu, atendewe haki kutokana na tuhuma ya kuwadunga mimba wanafunzi wake watatu

504D

Member
Feb 16, 2013
33
10
Wilaya ya Magu mkoani Mwanza, hususan Idara ya Elimu Msingi mekuwa ikitajwa sana kwenye uga huu wa JF kutokana na mambo kadha wa kadha kwenda kombo.

Kuna jambo jipya linaloendelea hukohuko Magu linalomhusu Mwl. Mkuu wa Ilungu S/ Msingi Bwn. Mambosasa.
Mwalimu huyu anatuhumiwa kuwadunga mimba wanafunzi wake watatu.

Mabinti hao wamehojiwa na mamlaka na vyombo husika na wametoa maelezo ya kutosha ambayo kwa hakika yanasikitisha!

Maelezo yao ni pamoja na kubainisha kwamba, mwalimu wao huyo alikuwa anawafanyia ufuska wake huo kwenye ofisi yake ya Mwalimu Mkuu; na wakati mwingine alikuwa anawaingiza mabinti wawili kwa mpigo; anamshughulikia mmoja, huku mwenzake akiangalia!

Ni udhalilishaji wa hali ya juu sana ambao umefanywa na mwalimu huyu ambaye ni mlezi; mtumishi wa umma aliyeaminiwa na Jamhuri, tena aliyesomeshwa kuwa mlezi wa watoto wa Taifa hili, akaaminiwa na Mamlaka za Wilaya, Mkurugenzi na Afisa Elimu na mamlaka zingine, anageuka kuwatafuna watoto wasiokuwa na hatia alikoabidhiwa ndani ya ofisi ya umma; badala ya kuwapa elimu, kuwatunza na kuwalinda ili wafikie malengo yao; inaumiza sana.

Mwalimu huyu sasa yuko nguvuni, mamlaka husika zikimhoji kubaini ukweli yakini wa mambo haya ili hatua stahiki zichukuliwe.
Ni matarajio ya waathirika na jamii kwa ujumla kwamba, mamlaka zote zinazohusika katika kushughulikia jambo hili zitatenda yote yapasayo kwa mujibu wa sheria, ili hali itendeke kwa pande zote.

Mwl. Mambosasa asitendewe isivyostahili bila ushahidi madhubuti dhidi yeke, ili tu kuifurahisha jamii inayomtuhumu (Public Interest).
Lakini pia hali ya waathirika lazima ilindwe; kama kuna ushahidi dhahir shahir dhidi ya mtuhumiwa; basi Mambosasa abebe mzigo wake wa mahindi mabichi aliyokula!

Alamsiki.
 
Pole mwalimu Mambosasa. Ila walimu hamna huruma hivi huwa hamvifananishi vitoto vya wenzenu na wa kwenu?
 
Kuna jambo jipya linaloendelea hukohuko Magu linalomhusu Mwl. Mkuu wa Ilungu S/ Msingi Bwn. Mambosasa.

Mwalimu huyu anatuhumiwa kuwadunga mimba wanafunzi wake watatu.
Analidhalilisha sana jina hilo la kamanda wa D.S.M.Z
 
Analidhalilisha sana jina hilo la kamanda wa D.S.M.Z
Kwani wana undugu nae au ni majina tu yamefanana?
Kama ni majina tu yamefanana, sina usemi.
Ila kama wana undugu, kuna usemi unasema hivi, DAMU NI NZITO KULIKO MAJI; na nyingine inasema, KILA MCHUMA JANGA HULA NA WA KWAO!! Waswahili bwana!!
 
Yeah...ananiona kila siku D
Huyo mwalimu atakua haelewani na jamii hivyo ni visa vya kutaka kumkomoa huenda hajafanya huo uharifu.Watoto wa shule ya msingi ni wadogo sana na hawezi kuwafanyia unyama wakiwa wawili kwa zamu.Ninachodhani huyo mwalimu atakua na mchezo wa kuchukua wake za watu au mabinti wa hilo eneo bila ridhaa ya wananzengo.Wasukuma hawawezi kumtongoza binti mzuri ambaye ana mahusiano na mwalimu.Mwalimu atakua amewazidi kete kwa wadada ndo mchezo mchafu ukaanzia hapo.
 
Wilaya ya Magu mkoani Mwanza, hususan Idara ya Elimu Msingi mekuwa ikitajwa sana kwenye uga huu wa JF kutokana na mambo kadha wa kadha kwenda kombo.

Kuna jambo jipya linaloendelea hukohuko Magu linalomhusu Mwl. Mkuu wa Ilungu S/ Msingi Bwn. Mambosasa.
Mwalimu huyu anatuhumiwa kuwadunga mimba wanafunzi wake watatu.

Mabinti hao wamehojiwa na mamlaka na vyombo husika na wametoa maelezo ya kutosha ambayo kwa hakika yanasikitisha!

Maelezo yao ni pamoja na kubainisha kwamba, mwalimu wao huyo alikuwa anawafanyia ufuska wake huo kwenye ofisi yake ya Mwalimu Mkuu; na wakati mwingine alikuwa anawaingiza mabinti wawili kwa mpigo; anamshughulikia mmoja, huku mwenzake akiangalia!

Ni udhalilishaji wa hali ya juu sana ambao umefanywa na mwalimu huyu ambaye ni mlezi; mtumishi wa umma aliyeaminiwa na Jamhuri, tena aliyesomeshwa kuwa mlezi wa watoto wa Taifa hili, akaaminiwa na Mamlaka za Wilaya, Mkurugenzi na Afisa Elimu na mamlaka zingine, anageuka kuwatafuna watoto wasiokuwa na hatia alikoabidhiwa ndani ya ofisi ya umma; badala ya kuwapa elimu, kuwatunza na kuwalinda ili wafikie malengo yao; inaumiza sana.

Mwalimu huyu sasa yuko nguvuni, mamlaka husika zikimhoji kubaini ukweli yakini wa mambo haya ili hatua stahiki zichukuliwe.
Ni matarajio ya waathirika na jamii kwa ujumla kwamba, mamlaka zote zinazohusika katika kushughulikia jambo hili zitatenda yote yapasayo kwa mujibu wa sheria, ili hali itendeke kwa pande zote.

Mwl. Mambosasa asitendewe isivyostahili bila ushahidi madhubuti dhidi yeke, ili tu kuifurahisha jamii inayomtuhumu (Public Interest).
Lakini pia hali ya waathirika lazima ilindwe; kama kuna ushahidi dhahir shahir dhidi ya mtuhumiwa; basi Mambosasa abebe mzigo wake wa mahindi mabichi aliyokula!

Alamsiki.
Huyu na yule wa dar mropokaji mtu na ndgu yake
 
Kina babu tale waliachana na ujinga wa vyeti wakawa misheni town tu... sasa wanaenda bungeni kwa cv kubwa kwamba meneja wa wasanii..

Wasomi tunatoa macho tu
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom