Mwl. Mambosasa S/Msingi Ilungu-Magu, atendewe haki kutokana na tuhuma ya kuwadunga mimba wanafunzi wake watatu

Marupurupu ya maticha hao
Mambo ya namna hii ni ukatili na udhalilishaji uliokithiri kwa watoto wanaofanyiwa hayo na waalimu wao. Jamii na Taifa pia linaathirika maana watoto hawa ni nguvukazi ya Taifa.
Taarifa zilizopo kuhusu tukio hili ni kwamba, aliyekuwa akiyafanya hayo kwa wanafunzi wale siyo Mwl. Mkuu Mambosasa peke yake; bali Mwl. Mkuu Msaidizi pamoja na Mwalimu wa Nidhamu, nao walikuwa washiriki wa mchezo huo mchafu dhidi ya watoto wale!!
Mwl. Mkuu, Msaidizi wake na Discipline Master, wanahusika kuwanajisi watoto hadi kuwapa mimba!!
Jamani, watoto hawa wako exposed kwenye hatari kiasi gani?
Ni mtu kutukana na kukufuru madaraka aliyopewa na umma; na haikubaliki.
Mwl. Mkuu ni kiongozi mwenye dhamana kubwa sana katika jamii; ndiyo maana Serikali inawalipa mishahara na Posho ya Madaraka, maana inatambua wajibu mkubwa wanaoubeba.
Baadhi ya shule zina watoto zaidi ya elfu moja, majengo, samani, fedha, miundo mbinu mbalimbali, waalimu na watumishi wengine; vyote hivi viko chini ya Mwl. Mkuu, ikiwa ni pamoja na kusimamia utendaji wa waalimu, taaluma ya watoto na mambo mengine mengi yahusuyo kituo husika. Ni wajibu mkubwa, Mwalimu anayekabidhiwa ukuu ni dhamana kubwa, yapaswa kuheshimiwa.
Kama unaona huwezi kumudu Ualimu Ukuu, kwa nini unakubali na kukiri uteuzi? Ni heri kukataa uteuzi, kuliko kuupokea kisha unakwenda kuwabikiri mabinti zetu; wengine tunasikia mpaka mnawafumua marinda ili kukwepa mimba; pumbavu sana, shwain!!
 
Mleta hoja inaonekana si mtanzania make ana busara nyingi kitu ambacho wabongo wengi tunakikosa..
Mi mashaur sheria ichukue mkondo wake kwa kuzingatia haki na usawa

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Mambo ya namna hii ni ukatili na udhalilishaji uliokithiri kwa watoto wanaofanyiwa hayo na waalimu wao. Jamii na Taifa pia linaathirika maana watoto hawa ni nguvukazi ya Taifa.
Taarifa zilizopo kuhusu tukio hili ni kwamba, aliyekuwa akiyafanya hayo kwa wanafunzi wale siyo Mwl. Mkuu Mambosasa peke yake; bali Mwl. Mkuu Msaidizi pamoja na Mwalimu wa Nidhamu, nao walikuwa washiriki wa mchezo huo mchafu dhidi ya watoto wale!!
Mwl. Mkuu, Msaidizi wake na Discipline Master, wanahusika kuwanajisi watoto hadi kuwapa mimba!!
Jamani, watoto hawa wako exposed kwenye hatari kiasi gani?
Ni mtu kutukana na kukufuru madaraka aliyopewa na umma; na haikubaliki.
Mwl. Mkuu ni kiongozi mwenye dhamana kubwa sana katika jamii; ndiyo maana Serikali inawalipa mishahara na Posho ya Madaraka, maana inatambua wajibu mkubwa wanaoubeba.
Baadhi ya shule zina watoto zaidi ya elfu moja, majengo, samani, fedha, miundo mbinu mbalimbali, waalimu na watumishi wengine; vyote hivi viko chini ya Mwl. Mkuu, ikiwa ni pamoja na kusimamia utendaji wa waalimu, taaluma ya watoto na mambo mengine mengi yahusuyo kituo husika. Ni wajibu mkubwa, Mwalimu anayekabidhiwa ukuu ni dhamana kubwa, yapaswa kuheshimiwa.
Kama unaona huwezi kumudu Ualimu Ukuu, kwa nini unakubali na kukiri uteuzi? Ni heri kukataa uteuzi, kuliko kuupokea kisha unakwenda kuwabikiri mabinti zetu; wengine tunasikia mpaka mnawafumua marinda ili kukwepa mimba; pumbavu sana, shwain!!
Yan jamani 😢😢
 
Mambo ya namna hii ni ukatili na udhalilishaji uliokithiri kwa watoto wanaofanyiwa hayo na waalimu wao. Jamii na Taifa pia linaathirika maana watoto hawa ni nguvukazi ya Taifa.
Taarifa zilizopo kuhusu tukio hili ni kwamba, aliyekuwa akiyafanya hayo kwa wanafunzi wale siyo Mwl. Mkuu Mambosasa peke yake; bali Mwl. Mkuu Msaidizi pamoja na Mwalimu wa Nidhamu, nao walikuwa washiriki wa mchezo huo mchafu dhidi ya watoto wale!!
Mwl. Mkuu, Msaidizi wake na Discipline Master, wanahusika kuwanajisi watoto hadi kuwapa mimba!!
Jamani, watoto hawa wako exposed kwenye hatari kiasi gani?
Ni mtu kutukana na kukufuru madaraka aliyopewa na umma; na haikubaliki.
Mwl. Mkuu ni kiongozi mwenye dhamana kubwa sana katika jamii; ndiyo maana Serikali inawalipa mishahara na Posho ya Madaraka, maana inatambua wajibu mkubwa wanaoubeba.
Baadhi ya shule zina watoto zaidi ya elfu moja, majengo, samani, fedha, miundo mbinu mbalimbali, waalimu na watumishi wengine; vyote hivi viko chini ya Mwl. Mkuu, ikiwa ni pamoja na kusimamia utendaji wa waalimu, taaluma ya watoto na mambo mengine mengi yahusuyo kituo husika. Ni wajibu mkubwa, Mwalimu anayekabidhiwa ukuu ni dhamana kubwa, yapaswa kuheshimiwa.
Kama unaona huwezi kumudu Ualimu Ukuu, kwa nini unakubali na kukiri uteuzi? Ni heri kukataa uteuzi, kuliko kuupokea kisha unakwenda kuwabikiri mabinti zetu; wengine tunasikia mpaka mnawafumua marinda ili kukwepa mimba; pumbavu sana, shwain!!
Mamlaka husika zichukue hatua zote kwa umakini ili haki itendeke na ionekane ikitendeka wa wahusika wote.
Mara nyingi, watuhumiwa katika kesi za aina hii wamekuwa wakiachiwa huru na mahakama, kutokana na kukosekana kwa ushahidi ama kwa huo ushahidi kuvurugwa kwa makusudi, au kutokana na makosa ya kiufundi yanayokuwa yamefanywa na upande wa mashtaka kuanzia upatikanaji wa taarifa, ukamataji, upelelezi, mashtaka, ushahidi na uendeshaji wa kesi.
Mtiririko huo wote unapaswa kufanyika kwa kufuata sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai (Criminal Procedure Act). Pakifanyika ukiukwaji wowote wa sheria mahala popote kwenye mtiririko huo; basi mshtakiwa atapata upenyo wa kuachiwa huru na mahakama kwa makosa ya kikanuni yanayokuwa yamefanywa na upande wa mashtaka ambayo yataifanya mahakama iwe na mashaka kuhusu mashtaka dhidi ya mshtakiwa (hata kama ni madogo); mashaka ambayo yanaweza kumnufaisha mshtakiwa mahakamani (benefit of doubt), hatimae mshtakiwa kuachiwa huru.
Kesi ya jinai haianzii mahakamani, bali huanza tangu taarifa ya kosa linalodaiwa kutendeka inapotolewa polisi.
Tunatarajia polisi na waendesha mashtaka wa serikali mtakuwa makini (smart) kuanzia mwanzo (kama hamjafanya makosa tayari) mpaka mwisho ili muweze kushinda kesi hii; vinginevyo mtapigwa chini na Mwl. Mambosasa akiwatumia mawakili wa utetezi; ni haki yake kutetewa na wanasheria.
Tutatarajia kuona mnyukano wa kisheria kati ya waendesha mashaka wa serikali (State Attorneys) na mawakili wa utetezi (Defense Counsels) ambao watawekwa na Chama Cha Waalimu Tanzania (CWT) ili kumtetea mwanachama wao!!
 
Kwa ile sheria ya ubakaji ya kulinda haki za wanafunzi ilivyo,nikiwa mkubwa sitaki kazi ya ualimu katu!
 
Kwani wana undugu nae au ni majina tu yamefanana?
Kama ni majina tu yamefanana, sina usemi.
Ila kama wana undugu, kuna usemi unasema hivi, DAMU NI NZITO KULIKO MAJI; na nyingine inasema, KILA MCHUMA JANGA HULA NA WA KWAO!! Waswahili bwana!!
Ila mti mmoja hauwezi kutoa matunda tofauti
 
Yan jamani 😢😢
Huyu mwalimu angekuwa ameshavuliwa ualimu mkuu kitambo tangu mwaka jana 2019 mapema kutokana na kasoro kadhaa za kiuongozi na kitaaluma zilizokuwa zinaikumba Ilingu S/Msingi chini ya uongozi wake.
DEO Msingi Magu na jopo la maofisa wake walipotaka kuchukua hatua hiyo, Afisa Vifaa na Takwimu (S.L.O.) aliyekuwepo wakati ule alimshauri DEO na maofisa wenzake wamwonye Mwl. Mambosasa na kumwagiza afanye marekebisho yaliyohitajika badala ya kumvua madaraka. DEO na jopo walipokea ushauri wa mwenzao.
Wahenga walisema la kuvunda halina ubani. Poleni watoto!!.
 
Back
Top Bottom