Mwl auwawa.

MotoYaMbongo

JF-Expert Member
Jan 7, 2008
2,146
883
Mwl wa nidhamu wa shule ya sekondari Chemchemi mkoani Singida ameuwawa kwa kuchomwa na kisu kifuani. Mwl huyo amechomwa kisu na wanafunzi wake hao, kwa sababu alikuwa anamfuatilia mmoja wa wanafunzi hao aliekuwa mtoro wa kupindukia. Wanafunzi hao walimvizia mwl huyo alipokuwa anatoka kilabuni na ndipo walipomvamia na kumtendea ukatili huo. Hadi sasa wanafunzi hao wametiwa mbaloni na jeshi la polisi na watafikishwa mahakamani siku yoyote kuanzia kesho.
 
haya sasa ni makubwa watu wataanza kuoogopa fani ya Ualimu, hawa watoto wachukuliwe hatua kali iwe fundisho kwa wengine
 
Hakika kazi ya kuondoa ujinga ni ngumu sana katika mazingira kama haya, just chukulia mtu yupo kwa ajili ya kukusaidia uondokane na ujinga, wewe unakataa mbinu anazkupa mwalimu kisha unaona ni kero sana kwa mwalimu kukufuatafuata unaamua kuua. Je tutafika????
 
Hakika kazi ya kuondoa ujinga ni ngumu sana katika mazingira kama haya, just chukulia mtu yupo kwa ajili ya kukusaidia uondokane na ujinga, wewe unakataa mbinu anazkupa mwalimu kisha unaona ni kero sana kwa mwalimu kukufuatafuata unaamua kuua. Je tutafika????
Sio siri,sasa hivi moja ya watu ambao huenda hawaaminiki na walio katika maisha magumu sana kwa sasa na tunakokwenda ni waalimu. Naposema waalimu simaanishi wa shule za msingi tu la hasha bali wo kuanzia shule za msingi hadi vyuo vikuu japo wao hujiita wahadhiri.Kutokana na mfumo wetu mabaya wa elimu usiorekebishwa mara kwa mara kwa maslahi ya taifa, wanafunzi wamekuwa hawajui wajibu wao,wengi hawajui kwa nini wamo humo mashuleni,hawajui kazi ya mwalimu ni ipi,na hata waalimu wenyewe kutokana na kutokana na mfumo huohuo wa uanafunzi wamekuwa nao hawajui wajibu wao saa nyingine ni upi kwa wanafunzi,matokeo yake kila kitu kimekuwa kikifanya kwa uzoefu na expediency tu.
Sasa hivi mwalimu akisahisha mtihani wa mwanafunzi na kumkosehs ajapo kwa haki kabisa basi mwalimu huyo atachukiwa sana,mwalimu akimuonya mwanafunzi kwa jambo la haki kabisa mf,utoro au ulevi, bangi nk mwalimu huyo atachukiwa kabisa.Kutokana na kuwa walimu nao kama vile hawana mtu wa kuwatetea hasa wanapopata vipigo toka kwa wanafunzi,migomo,na hata kuuawa kama hivyo,Waalimu wetu hao baadhi yao wameishi a kusema nifanye hivi kwa faida ya nani wakati watu wenyewe hawaelewi.

Kutokana na hilo wengi sasa wanafundisha tu,mwanafunzi aelewe asielewe potelea kokote sio wajibu wangu,wengine kuepuka mtatizo wanaamua kustandardise tu maksi kwa kuwafaulisha wanafunzi wote hata kama wajinga basi,wengine wao ni lesser fair tu,na hawa ndio hupendwa sana na wanafunzi.Hii ndio elimu yetu iendako sasa.
 
WANAFUNZI 600 wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu. Augustine cha jijini Mwanza waliofutiwa matokeo ya mitihani wa muhula wa pili kwa mwaka wa masomo 2007/2008, wanajiandaa kwenda mahakamani kupinga uamuzi huo.

Bora hawa wameamua kwenda kwa pilato
 
Sio siri,sasa hivi moja ya watu ambao huenda hawaaminiki na walio katika maisha magumu sana kwa sasa na tunakokwenda ni waalimu. Naposema waalimu simaanishi wa shule za msingi tu la hasha bali wo kuanzia shule za msingi hadi vyuo vikuu japo wao hujiita wahadhiri.

Upo sahihi, kabisa Ukiangalia upande wa vyuo vikuu ndio noma zaidi maana wanafunzi wakifeli wanasema kuwa umewakamata na wengine "wanatishia kwenda Bagamoyo kukushusha mshipa" Kuna Mhadhiri mmoja aliwahi kunilalamikia kuwa mwanafunzi kamwambia akimkata basi ajue kuwa nayeye siku zake zinahesabika anamloga na hamtanii. Kwa wale tusioamini uchawi tunaweza puuzia ila kama mwanafunzi anatamka hivyo ujue yupo tayari kukudhuru kwa namna yoyote. Inatisha sana hii kazi kwa sasa
 
chem chem ni shule iliyopo mkoani SINGIDA, huku wana-IRAMBA waliopo sehemu mbaloimbali wakiunganisha nguvu zao pamoja kwa ajili ya maendeleo yao pamoja kuna wanaorudisha nyuma jitihada hizo.
UKWAMI (wanairamba waishio sehemu tofauti duniani kwa maendeleo ya IRAMBA) hii ni changamoto nyingine kwenu, tokomezeni hali hii...!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom