Mwizi wa kura ni sawa tu na mwizi wa kuku. Amri ya saba inasema USIIBE. Haijasema usiibe kuku lakini kura iba tu!
Mwizi anashughulikiwa kwa staili yake. Binadamu tuna staili yetu na kuku wana staili yao.
Kuna mwizi wa kuku anaitwa kunguru. Huyu huiba vifaranga vya kuku. Lakini kufanikiwa kwake inategemea mama mwenye vifaranga anafanyaje. Kuna kuku mwenye vifaranga ambaye akiona kunguru anaiba vifaranga vyake analia tu na kulalamika. Hii haimzuii kunguru kupora vifaranga na ataviiba kimoja kimoja hadi vyote vimeisha.
Lakini kuna kuku mwingine mwenye vifaranga ambaye kunguru akitaka kuiba watoto wake anamrukia juu kwa juu na kujibu mashambulizi hadi kunguru anakimbia. Kunguru anaogopa sana kumwibia kuku huyu na anaacha watoto wake salama.
Ukitangaza mapema kuwa kunguru akitaka kuiba kuku wako hutachukua hatua za kumzuia si utakuwa umemwambia aibe kwa muda wake?
Mwizi anashughulikiwa kwa staili yake. Binadamu tuna staili yetu na kuku wana staili yao.
Kuna mwizi wa kuku anaitwa kunguru. Huyu huiba vifaranga vya kuku. Lakini kufanikiwa kwake inategemea mama mwenye vifaranga anafanyaje. Kuna kuku mwenye vifaranga ambaye akiona kunguru anaiba vifaranga vyake analia tu na kulalamika. Hii haimzuii kunguru kupora vifaranga na ataviiba kimoja kimoja hadi vyote vimeisha.
Lakini kuna kuku mwingine mwenye vifaranga ambaye kunguru akitaka kuiba watoto wake anamrukia juu kwa juu na kujibu mashambulizi hadi kunguru anakimbia. Kunguru anaogopa sana kumwibia kuku huyu na anaacha watoto wake salama.
Ukitangaza mapema kuwa kunguru akitaka kuiba kuku wako hutachukua hatua za kumzuia si utakuwa umemwambia aibe kwa muda wake?