gmosha48
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 2,399
- 1,478
Ndugu yang kinachonisikitisha mimi ni pale Radio Clouds na KIBONDE walivyolishikia kidedea, amesoma gazeti lote la HABARI LEO huku akiwashutumu wanaharakati kwa kukaa kimya!... halafu anaongea huku akionyesha kufurahishwa na hatua iliyochukuliwa na Bakwata pamoja na taasisi nyingine za kiisilam.. napata sana uoga na naoma propaganda zinavyoendeshwa naiona Tanzania yangu ikipoteza umoja kwa jambo ambalo kwangu naona sio kubwa kiivyo... Waislam ni watu wenye busara sana natumaini hawatalichulia swala hili kwa jazba kiasi hicho, Sitaki kuamini kwamba BAKWATA wanatumiwa na CCM maana wamekuja Mbogo kuliko tukio lenyewe.
Mkuu, kwa ujumla kinachofanywa na vyombo vya habari kwa sasa zikiwemo TV na Redio ni aibu kubwa! Wamezidisha mno kushabikia na kuonyesha upendeleo wa wazi kwa Chama Tawala na serikali. Chama na Serikali tayari wana vyombo vyake vya habari, hivyo propaganda za chama tawala na serikali zingeachiwa vyombo husika. Kwa mtazamo wangu, vyombo huru ( binafsi) vingejikita katika kuonyesha habari zenye uwiano.... kwa maana kuwa zipo habari nyingine ambazo hatuwezi kuzisikia kutoka kwenye radio au TV za chama tawala na serikali. Inashangaza sana kuona TV kama ITV wanaripoti kampeni za CCM peke yake, bila kutiupia hata sekunde moja ya kampeni za vyama vingine. Kama hiyo ndo demokrasia tunayojivunia, bado tuna safari ndefu.