Mwita Waitara adai elimu bure maana yake ni wanafunzi kulipiwa ada na Serikali, mzee Mwamakula amshangaa na kusema mawaziri hawana maono

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,616
141,445
Naibu waziri wa Tamisemi anayeshughulikia miundombinu ya elimu ya msingi na sekondari mwalimu Mwita Waitara amesema maana ya Elimu Bure ni wanafunzi kulipiwa ada na serikali.

Waitara amedai kuwa wananchi wengi wanachanganya mambo kwa kudhani kuwa ujenzi wa miundombinu ya elimu yakiwemo madarasa, maabara, madawati, vyoo nk ni sehemu ya mpango wa elimu bure na hivyo hawapaswi kuchangia.

Naye kada wa CCM ambaye ni afisa wa polisi mstaafu mzee Mwamakula amemshangaa waziri Waitara na kusema kwa hakika mawaziri wa awamu ya 5 hawana maoni kabisa.

Mzee Mwamakula amesema anashindwa kuelewa majukumu ya waziri wa Utawala Bora endapo hata swala la ujenzi wa madarasa ya watoti linakuwa na mjadala wa kitaifa wakati linaeleweka kabisa ni jukumu la nani.

Chanzo: Malumbano ya Hoja ITV
 
Saizi kuna waropokaji,sikumbuki lini nimeangalia taarifa ya habari ya bongo maana ni kichefuchefu sana,unaona viongozi wanatoa matamko ya kijinga,hotuba za kitoto,wanatukana watu ovyo.......yaani unajiuliza hivi hawa wana hata abc za kuwa viongozi?
Huyu Waitara katokea Chadema!
 
Naibu waziri wa Tamisemi anayeshughulikia miundombinu ya elimu ya msingi na sekondari mwalimu Mwita Waitara amesema maana ya Elimu Bure ni wanafunzi kulipiwa ada na serikali.

Waitara amedai kuwa wananchi wengi wanachanganya mambo kwa kudhani kuwa ujenzi wa miundombinu ya elimu yakiwemo madarasa, maabara, madawati, vyoo nk ni sehemu ya mpango wa elimu bure na hivyo hawapaswi kuchangia.

Naye kada wa CCM ambaye ni afisa wa polisi mstaafu mzee Mwamakula amemshangaa waziri Waitara na kusema kwa hakika mawaziri wa awamu ya 5 hawana maoni kabisa.
Mzee Mwamakula amesema anashindwa kuelewa majukumu ya waziri wa Utawala Bora endapo hata swala la ujenzi wa madarasa ya watoti linakuwa na mjadala wa kitaifa wakati linaeleweka kabisa ni jukumu la nani.

Source: Malumbano ya Hoja ITV
Tatizo siyo kutokuwa na maono kwa mawaziri. Tatizo ni bosi wao.Alipoingia magogoni alipiga marufuku"michango michango"kwa mbwembwe na tambo na kuonya watakaotenda kinyume! Baada ya kuona "mtiti"ulivyo mzito ka-retreat. Kazi imebaki kusafisha "uharo"huo kitu ambacho kinawatesa wasaidizi wake kwani lugha iliyotumika ilieleweka! Utaipinduaje?
 
Tatizo siyo kutokuwa na maono kwa mawaziri. Tatizo ni bosi wao.Alipoingia magogoni alipiga marufuku"michango michango"kwa mbwembwe na tambo na kuonya watakaotenda kinyume! Baada ya kuona "mtiti"ulivyo mzito ka-retreat. Kazi imebaki kusafisha "uharo"huo kitu ambacho kinawatesa wasaidizi wake kwani lugha iliyotumika ilieleweka! Utaipinduaje?
Wewe elimu bure unaitafsiri vipi?
 
Hata angetokea TLP au NLD,kutokea Chadema hakujustifai kutotumia akili ya nn uongee na wakati gani uongee,then mm huwa simsupport mwanasiasa kwa chama alichotoka ila kwa hoja na namna anavyoweza kusimama mbele ya umma na kutoropoka ropoka kama zuzu.........
Chadema ndio walipigania elimu bure!
 
Wewe elimu bure unaitafsiri vipi?
Kwa mujibu wa tafsiri ya leo "Ni mzazi/mlezi kutotozwa ada!"
Lakini kwa tuliosoma enzi za "Elimu bure" ya kiukweli ilikuwa: Hakuna ada,nauli unalipiwa,chakula ,matibabu,vitabu na vinginevyo muhimu hulipii! Hata hao wanaodanganya wanatoa elimu bure wanajua. (Labda kina Jafo,Kairuki,Waitara,Mavunde) hawajui kwani ni "mawaziri watoto)"
 
Back
Top Bottom