MWISHO wa UKAWA

Old Member (Retired)

JF-Expert Member
Sep 29, 2012
3,401
1,604
Ukawa itasambaratishwa kwa kutumia pesa tu.

Ukitoa ngono, hakuna kitu tunacho kiabudu watanzania kama pesa haijalishi pesa ni halali au haramu.
Kwa kutambua hilo, CCM itatumia pesa kulitawanya genge hili la vijana na wazee. Kwa bahati mbaya
si vijana wote au wazee wote watapata hizo pesa bali ni wale wachache wenye nguvu kubwa ndani
ya genge hilo.

TUWAOMBEE UKAWA, washinde jaribu la pesa ili waokoe kizazi cha sasa na kijacho.
 
UKAWA mbona imeshasambaratika siku nyingi baada ya mbowe na slaa kula pesa ya wafadhili
 
Maalim Seif bado anazo nguvu za maamuzi kwa upande wa CUF Taifa? Mtu mwenye ushawishi na rahisi kurubuniwa kwa vipande vya fedha ni Mh Seif S. Hamad.Prof Lipumba hana tamaa,ila ana ushawishi mdogo CUF. Kwa CHADEMA alikuwa Mh ZZK,kwa sasa hana ubavu.
 
Hakuna pesa itakayotumika kusambaratisha UKAWA. Hawa watasambaratishwa na tamaa zao za kugombea madaraka.
 
Ndoto za mchana kama wameshindwa kuisambaratisha cdm na cuf wataweza vipi baada ya kuunganisha nguvu?
Waje na hizo pesa kama hawajafilisika na ukawa ikazidi kuimarika
 
Ukawa itasambaratishwa kwa kutumia pesa tu.

Ukitoa ngono, hakuna kitu tunacho kiabudu watanzania kama pesa haijalishi pesa ni halali au haramu.
Kwa kutambua hilo, CCM itatumia pesa kulitawanya genge hili la vijana na wazee. Kwa bahati mbaya
si vijana wote au wazee wote watapata hizo pesa bali ni wale wachache wenye nguvu kubwa ndani
ya genge hilo.

TUWAOMBEE UKAWA, washinde jaribu la pesa ili waokoe kizazi cha sasa na kijacho.
Unakula ugali kwa mboga ya serikali saa tano usiku, kwanini usiote ndoto kama hizo. Halafu ukishaota ndoto unajiita nabii; kisha unatabiri nakuamini utabiri huu na kujaribu kutuaminisha. Yaani umeshasahau kuwa msingi ni ndoto iliyotokana na kula ugali kwa mboga ya serikali saa tano usiku. Kuwa makini ndugu!

Any way kukusaidia tu (maana najua umetuwa na Kinana na Nape) UKAWA ndo mambo yote kwa sasa, hata ufanyeje!
 
Back
Top Bottom