Mwisho wa kizazi na nguvu ya Mungu

Na mimi sikumaanisha tunda la kati huko Eden, Mimi nilimaanisha kitendo cha kufanya ngono/mapenzi na baadaye mimba kutungwa kwa mwanamke na mtoto binadamu kuzaliwa duniani, hiki kitendo ndo kinaleta tafrani na shida kwa watu hao hao, bora kuacha tendo hilo ili namna nyingine ya dunia ije !
Shida watu huwa mnadhani tunda walilokula Adam na Eva ni ngono;

Tunda walilokula ni tunda halisi la mti uliokuwepo kwenye bustani ya Edeni.

Mungu aliwaagiza kuzaana mara tu ya kukamilisha uumbaji wa wote wawili, ina maana aliwaruhusu kufanya tendo la ndoa mara tu baada ya kukamilisha uumbaji wao na SI KWAMBA walianza kufanya tendo la ndoa baada ya uasi wa sheria (kula tunda walilokatazwa na Mungu)

Msiwe hivyo jamani, tunda hilo katika maandiko siyo fumbo bali ni lugha Moja kwa moja na dhahiri kabisa.
 
Adam alifanya uzinzi kabla ya kuruhusiwa na hii laana inaendelea kutuandama🤗🤗🤗
Mungu alijipangia muda wa kuwaruhusu kwa baraka zote wao wakafanya ile tunaita kujiongeza😂😂
Lazima utest mitambo
Nalog off
 
Kama hivo basi tuachwe huru, mambo ya kuambiwa shida za duniani ni sababu ya mambo ya dhambi mara shetani mara sijui Mungu anapanga yeye yaachwe ! Yaani maisha yetu yawe huru kama anavyosema
Ww upo huru. Unabanwa na sheria za nchi tu.
 
haya yote umeyafahamu kupitia wapi!?

je unaweza kunipa maana ya mungu!? na kumuelezea pia!? kwa nia ya kufundishana kama hautojali!
Lugha ni mfumo wa sauti za nasibu zilizokuwa katika mpangalio maalumu zilizokubaliwa kwenye jamii husika. Mfano neno barabara. Kiuhakika si barabara bali jamii imeipa hilo jina na kulibariki ndiyo liwe rasmi ya kuwa ikisemwa barabara basi ifahamike kama tunavyofahamu nini maana ya barabara.

Kama ilivyokuwa kwa waundaji wa zana au bidhaa anuwai wana majina yao husika na yanayofahamika ndani ya jamii nazungumzia wafanyabiashara. Halikadhalika kwa neno Mungu. Jamii imelikubali na kulifanya liwe rasmi ya kwamba inapotamkwa neno Mungu inamaanisha aliyeumba ulimwengu na vilivyomo ndani yake wakiwemo binadamu.

Hivyo, ikitamkwa Mungu inamaanisha aliyetuumba sisi na vinginevyo kama mwisho wa aya ya juu inavyofafanua.

Haya yote umeyafahamu wapi?
Nimeyafahamu kupitia vyanzo tofauti mchanganyiko ambazo ni haya tunayofundishwa darasani kwenye elimu za mashuleni. Mengine nimeyapatia kupitia elimu za dini. Hivyo, kwa mjumuisho wa elimu hizo mbili zikanifanya kukubali kuwa yupo aliyeyafanya haya ambaye ni Mungu.
 
I see.... nimeipenda na urefu wake, hoja nzuri katika lugha/kiswahili kisicho rahisi!

Kwa maneno mengine ambayo ni generally; katika hali ya kawaida SISI BINADAMU NI VIUMBE WADOGO KUJUA HATA NGUVU NA UWEZO WA MUNGU, JINSI ALIVYOUMBA BINADAMU WAKE NA MAKUSUSUDI YAKE.....
Mantiki ya kusema vile hapo juu ni kwa nini shida na mateso duniani yamezidi na hakuna msaada toka kwa Mungu; hivyo basi tuachane na uzazi na kuzaliana ili shida zikome, na huyo muumba aanze upya!

Screenshot_20210126-174552.png

Huu mchoro una jawabu la swali lako Mkuu.
 
Katika hali ya tafakuri ya kawaida, Mungu ndiye Muumba wa vitu vyote akiwemo kiumbe binadamu!

Kizazi cha binadamu hufanya watu kuongezeka kila kukicha. Ongezeko la watu na kizazi kuendelea kuwepo duniani ni kwa sababu ya tendo la ndoa/ngono. Yaani kiumbe hai binadamu na yote yanayomkuta ni sababu ya kufanya tendo hilo. Kitendo cha mwanamke kukutana na mwanaume ndo kinafanya binadamu na matatizo yaliyopo yaendelee kuwepo. Vitu vyote unavyoona binadamu anafanya, binadamu yule ni kwa vile alizaliwa, naye atazaa tena binadamu mwenye tabia na matendo yake, yawe mazuri au mabaya.

Ninachotaka kusema ni kuwa jeuri ya Mungu au nguvu za Mungu kufanya yote haya yanayomkuta binadamu ni kumuumba binadamu na hali au namna ya kuweza kufanya mapenzi au tendo la ndoa ngono. Tendo lile ndo maana aliliweka kwa namna ambayo kiumbe binadamu linamfurahisha akili na mwili. Kwa maneno mengine, tendo lile lisingekuwa linasisimua mwili na akili za binadamu, naamini watu wasingezaliana na kuongezeka. Hiyo ndo jeuri ya Mungu na hapo ndo mtego wa Mungu kwa binadamu.

Siku binadamu duniani wakiligundua na kupata upeo na uwezo wa kuliacha tendo lile miaka na miaka, dunia ingekuwa na history nyingine na mabadiliko ya nguvu Mungu yangejitokeza. Mthalani, binadamu duniani wakikubaliana kuacha kuzaa na kuzaliana miaka almost Mia au Mia mbili ili waliopo waishe naamini Mungu angejipanga upya. Lazima angetokea na kuumba ulimwengu mpya. Binadamu duniani nzima nikubaliane, na viumbe wengine ikitokea nao wakajikuta wanafanya hivo nadhani Mungu angepata akili nyingine. Bahati mbaya au nzuri ni kama tendo lile ni kama sehemu ya akili au roho au utu wa mtu, ni kama ndo maisha yenyewe. Lkn ingewezekana tungeacha kuzaa na kuzaliana miaka na miaka tuone kutatokea nini- duniani.

Ndo maana nikasema, jeuri ya Mungu kwa binadamu ni kufanya tendo la ndoa au ngono kuwa na hali ya burudani and it's like uncontrollable urge.
Kwa maneno mengine ni kuwa ngono ni tendo la maana kubwa sana katika concept ya uumbaji. Janja ya Mungu ni hapo...... Ebu tujaribu kama miaka 150, Mungu aumbe upya !
Mkuu ulichokisema kina ukweli ndani yake!
 
Back
Top Bottom