Mwinyi ajipa ujiko kwa kuweka misingi imara ya mageuzi!

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
Mwinyi: Niliweka misingi bora vyama vingi


Na Ali Suleiman, Zanzibar

RAIS mstaafu wa Awamu ya Pili, Bw. Ali Hassan Mwinyi, amesema katika kipindi cha uongozi wake, alifanya kazi kubwa ya kuweka misingi bora katika mfumo wa vyama vingi kiasi cha kuwapo uvumilivu wa kisiasa nchini.

Alhaji Mwinyi alisema hayo juzi wakati akifungua kongamano la siku mbili la uvumilivu wa kisiasa lililotayarishwa na taasisi ya kibunge ya Amani Forum mjini hapa.

Alisema misingi hiyo aliyoiweka ndiyo inayofanya kazi na kulifanya Taifa hili na vyama siasa kuwa na siasa za kuvumiliana na za kistaarabu.

"Tunaweza kuwa na vyama vingi, si tatizo, lakini cha msingi ni kujenga tabia ya kuwa na siasa za kuvumiliana zitakazoendeshwa kwa njia ya kistaarabu," alisema.

Alisema utaratibu huo umekuwa ukivutia watu wengi wa mataifa jirani, kiasi cha kuonekana Tanzania kama moja ya nchi zilizokomaa katika siasa za vyama vingi.

Rais mstaafu Mwinyi ambaye ndiye aliyeanzisha mchakato wa Tanzania kuingia katika mageuzi ya mfumo wa vyama vingi nchini mwaka 1992, aliwataka Watanzania kuendeleza utamaduni wa kuvumiliana na kuheshimiana.

Alisema siasa si ugomvi wala vurugu, lakini ni utaratibu tu unaokubalika katika kupata viongozi kwa njia ya amani na utulivu.

Kongamano hilo liliwakutanisha viongozi mbali mbali wa kisiasa nchini, wakiwamo wabunge na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kutoka vyama vya CCM na CUF na viongozi wa vyama vya siasa nchini, lilijadili mada mbali mbali zikiwamo siasa za kuvumiliana na njia za kuepuka migogoro.

Miongoni mwa kazi za taasisi ya Amani Forum, ni kujaribu kuipatia ufumbuzi migogoro mbali mbali katika nchi za Maziwa Makuu Afrika na kusimamia uchaguzi mbali mbali nchini.


source majira
 
Mwinyi was simply the best!!!

Pamoja na mapungufu yake yaliyojitokeza chini ya utawala wake bado taa ya mzee Ruksa itaendelea kung'aa kwa hekima zake,busara na uvumilivu wake.

Nadhani watu bado wataendelea kukumbuka pale watawala waliomfuatia kutopata nderemo na vifijo vingi kutoka kwa wananchi ukilinganisha nae, nakumbuka matukio kadhaa likiwemo lile la uwanja wa Taifa zamani watu walipolipuka kwa hamasa na kushangilia ruksa,ruksa huku mkuu wa nchi kwa wakati huo akipata shamra shamra ndogo ukilinganisha na ruksa.

Tukio la kujiuzulu uwaziri ktk miaka ya 80s baada ya watendaje wa chini kuvurunda bado inamuweka ktk chati ya viongozi wachache ambao ni 'responsible & accountable'

Kila la kheri Ruksa tutaendelea kukuenzi......
 
People you must be joking! I would say simply the worst, though JK anaelekea huko huenda atamshinda. Kuna mangi mabaya ya kusema kuhusu utawala wake kuliko hata JK na Mkapa combined, ni kipindi ambacho mkewe alikuwa Rais by proxy, na kuuza tausi wote ikulu, Corruption ilihalalishwa dawa za kulevya mpaka maofisa wa ubalozi wakaanza hata kuhusishwa, balozi zilikuwa kama dili za watu na sio za serikali, infaltion kinoma, kashfa ya vigogo, wahindi kuwanyanyasa watanzania kwa mbwembwe, Mkemia mkuu wa serikali na wenzake waliaga dunia kwenye mazingira ya ajabu ajabu(kisa kutaka kuwalinda watanzania dhidi ya vyakula vibovu), heshima ya TAnzania ilikuwa lowest ever, lowest hata kuliko ya sasa,uswahili(umission town) ulitawala kuwa sekta ya uchumi Tanzania, Zanzibar ndiyo kama ulikuwa mali ya mtu binafsi kila kitu kilikuwa kinaenda ovyo.....mpaka waasi wa Burundi wakaanza hata kujaribu kushambulia Tanzania, and then today you tell me Mwinyi was best? Sikubaliani hata kidogo, Mpaka sasa Mkapa stands best to me(ana mapungufu yake i agree)
 
People you must be joking! I would say simply the worst, though JK anaelekea huko huenda atamshinda. Kuna mangi mabaya ya kusema kuhusu utawala wake kuliko hata JK na Mkapa combined, ni kipindi ambacho mkewe alikuwa Rais by proxy, na kuuza tausi wote ikulu, Corruption ilihalalishwa dawa za kulevya mpaka maofisa wa ubalozi wakaanza hata kuhusishwa, balozi zilikuwa kama dili za watu na sio za serikali, infaltion kinoma, kashfa ya vigogo, wahindi kuwanyanyasa watanzania kwa mbwembwe, Mkemia mkuu wa serikali na wenzake waliaga dunia kwenye mazingira ya ajabu ajabu(kisa kutaka kuwalinda watanzania dhidi ya vyakula vibovu), heshima ya TAnzania ilikuwa lowest ever, lowest hata kuliko ya sasa,uswahili(umission town) ulitawala kuwa sekta ya uchumi Tanzania, Zanzibar ndiyo kama ulikuwa mali ya mtu binafsi kila kitu kilikuwa kinaenda ovyo.....mpaka waasi wa Burundi wakaanza hata kujaribu kushambulia Tanzania, and then today you tell me Mwinyi was best? Sikubaliani hata kidogo, Mpaka sasa Mkapa stands best to me(ana mapungufu yake i agree)

Bongolander mimi naamini kabisa sisi waTZ kama siyo wAfrica ubongo wetu siyo sawa! Tushasahau kuwa this guy was the worst president, a failed president! We have to diffentiate between the worst President (PRESIDENCY) and a good guy! Ni kweli he is a nice guy but the worst president Tanzania had! Mkapa was the best, all his qualities dipped kwa sababu ya uchoyo wake!
 
Mzee Rukhsa, as a person, ni mtu muungwana, mwema sana, nami naamini ndio sababu watu wanampenda. Hakuwa na chembe ya roho mbaya wala kisasi. Na watu waliokuwa wanafanya kazi chini yake waliutumia vibaya uungwana wake, wema wake, huruma aliyokuwa nayo, fairness (kiswahili hapa nisaidieni), waliyatumia haya vibaya kujinufaisha binafsi. Udhaifu wa mzee Rukhsa ulionekana pale alipowaonea haya ama huruma watu hawa, lakini binafsi hakushiriki ufisadi huo. Kwa hiyo kwa uelewa wangu wa yule mzee, watu wengi wanampenda yeye binafsi, kuliko utawala wake, na hili linaonekana hata sasa anapoalikwa kwenye hafla mbalimbali. Ona sasa ni zaidi ya miaka 12 tangu alipostaafu, lakini hakuna hoja yoyote ya ufisadi iliyoibuliwa dhidi yake.

Licha ya yanayosemwa kuhusu uchumi, sijui inflation nk, Mzee Rukhsa alitutoa mahali pagumu sana, nadhani hatua alizochukua wakati ule akiwa madarakani zilikuwa muafaka kabisa kwa ajili ya kutuvusha katika mazingira yaliyokuwapo. Ndiyo yaliyokuwa majibu ya matatizo yetu kwa wakati ule, kwa hiyo hayapaswi kutumika kumtathmini Mzee Rukhsa kwa viwango vya leo hii. Kazi iliyopo kwa walio madarakani LEO ni kutafuta majibu ya matatizo ya watanzania kwa mazingira ya LEO, na si kuanza kujilinganisha na mazingira aliyoyakuta Mzee Rukhsa au Mwalimu Nyerere.
 
Mzee Rukhsa, as a person, ni mtu muungwana, mwema sana, nami naamini ndio sababu watu wanampenda. Hakuwa na chembe ya roho mbaya wala kisasi. Na watu waliokuwa wanafanya kazi chini yake waliutumia vibaya uungwana wake, wema wake, huruma aliyokuwa nayo, fairness (kiswahili hapa nisaidieni), waliyatumia haya vibaya kujinufaisha binafsi. Udhaifu wa mzee Rukhsa ulionekana pale alipowaonea haya ama huruma watu hawa, lakini binafsi hakushiriki ufisadi huo. Kwa hiyo kwa uelewa wangu wa yule mzee, watu wengi wanampenda yeye binafsi, kuliko utawala wake, na hili linaonekana hata sasa anapoalikwa kwenye hafla mbalimbali. Ona sasa ni zaidi ya miaka 12 tangu alipostaafu, lakini hakuna hoja yoyote ya ufisadi iliyoibuliwa dhidi yake.

Licha ya yanayosemwa kuhusu uchumi, sijui inflation nk, Mzee Rukhsa alitutoa mahali pagumu sana, nadhani hatua alizochukua wakati ule akiwa madarakani zilikuwa muafaka kabisa kwa ajili ya kutuvusha katika mazingira yaliyokuwapo. Ndiyo yaliyokuwa majibu ya matatizo yetu kwa wakati ule, kwa hiyo hayapaswi kutumika kumtathmini Mzee Rukhsa kwa viwango vya leo hii. Kazi iliyopo kwa walio madarakani LEO ni kutafuta majibu ya matatizo ya watanzania kwa mazingira ya LEO, na si kuanza kujilinganisha na mazingira aliyoyakuta Mzee Rukhsa au Mwalimu Nyerere.

Mzee Kithuku....'Need I say More!!!'

Umepigilia msumari ktk hoja hii, Mwinyi kwa kiasi kikubwa alifanya yale ambayo yalikuwa ni medicine kwa kipindi chake.

Nashauri pia kwa wenye doubt wapitie kitabu kile cha mchumi maarufu 'Keynes' alipokuwa akielezea 'general caourse of unemployment' ingawa pia walio chini yake waliutumia upole na uungwana wake kumuangusha. lakini lazima tukubali kuna wakati chepeo liitwe chepeo kwa maana ya jina lake.

Mwinyi hakuanzisha kampuni ikulu (kwa kutumia address ya majengo ya mahali pale palipotukuka).

Mwinyi 'hakuwabully' wala kuwadharau wapinzani wake zaidi aliendelea kuwa mstaarabu hata pale palipokuwa na muolekeo wa matusi ya waziwazi.

Mwinyi hakuwa na tamaa ya kutaka kutumia madaraka yake kujinyakulia hisa za makampuni binafsi na kujigawia 'lion shares' yeye na familia yake (Kiwira mining Corporation) prove this differently to leaders followed after him.

Na mengineyo mengi..., ndio maana mzee huyu heshima yake ktk jamii bado itabaki 'intact' na ataendelea kufurahiwa na watz wa rika zote kila aendapo. Kusema was the the worst ni kutukubaliana na 'response' inayoonekana ktk jamii pale wazee hawa waliowahi kupita jengo jeupe wanavyopekelewa kwa watu wa kawaida.

Tanzania itajengwa na watu wake walio na huruma kwa wenzao na wasio na choyo wala uroho wa kujinufaisha kwa kutumia ofisi za umma.
 
Anayemsema vibaya Mzee Mwinyi na kumsifia Mkapa, nadhani ana lake jambo, kama si Mkapa basi ni wanufaika wake, lakini sisi tilio wengi ni waathirika wa Mkapa.. na tunaomba Mungu tusiwe waathirika wa Kikwete maana bado kweupeee, Mkapa alianza makeke 1999 miaka minne baada ya kutawala... Labda tukumbuke toleo la kwanza la RAIA MWEMA waliandika:


Masikini Mzee Ali Hassan Mwinyi!

Ncheme, nchicheme? Oktoba 31, 2007

TUNGEKUWA tumejaaliwa uungwana na Mwenyezi Mungu, nasi tukawa ni watu wa kukiri makosa yetu na kisha tukawa na moyo wa kutaka radhi wale tuliowakosea, basi Watanzania wengi tungekuwa tumekwisha kuunga ujumbe wa watu wasiopungua 500 kwenda kuanguka chini ya miguu ya Mzee Ali Hassan Mwinyi huku tukimwomba atusamehe kwa makosa makubwa tuliyomtendea.

Ujumbe huo ungepaswa uongozwe na wahariri na wasanifu wakuu wa tahariri katika magazeti ya miaka ya mwanzo ya 1990, kwa sababu sisi ndio hasa tulikuwa msitari wa mbele katika kutenda makosa hayo dhidi ya mzee huyo ambaye tulimbatiza jina la "Mzee Ruksa".

Kosa kubwa tulilotenda dhidi ya Rais huyo wa Awamu ya Pili ilikuwa ni kumhusisha na vitendo vya rushwa na ufisadi, hata kuwafanya wasomaji wa magazeti yaliyochapishwa wakati huo, waamini kwamba kilichokuwa kikifanyika Ikulu ulikuwa ni uharamia wa hali ya juu.

Sasa tunajua kwamba yote haya hayakuwa kweli. Haiwezekani kusema kwamba Mzee Mwinyi hakuwa na dosari, kwani kusema hivyo ni kumwondoa kwenye kundi la binadamu.




Alikuwa na dosari zake na udhaifu wake, na hayo bado anayo hadi leo, kwa ilivyokuwa wakati akiwa Ikulu. Lakini pia ni kweli kwamba sehemu ya udhaifu wake ilitokana na wema na upole wake katika mazingira ya "manyang'au" aliowaamini na ambao hawakusita kuutumia upole wake na jina lake kufanya walivyotaka kwa kumsingizia yeye.

Leo hii sote tunajua kwamba tulimwonea sana Mzee Mwinyi kwa kumbebesha mambo yasiyokuwa yake. Na wala si yeye peke yake aliyekumbwa na uonevu huo bali pia mkewe, Bi Sitti Mwinyi, ambaye naye alihusishwa na kila aina ya maovu kutokana na uvumi ulioenezwa na baadhi ya vyombo vya habari.

Baadhi tutakumbuka pia kwamba Mzee Mwinyi aliwahi kulalamika hadharani kwamba uvumi ulikuwa umeenezwa kuhusu yeye kumwoa kigori mdogo kwa kumfanya aache shule… kila aina ya uvumu na uzushi. Mzee huyu muungwana alivumilia, akavuta subira, akasamehe. Haishangazi kwamba amebaki kuwa kipenzi cha Watanzania kutokana na upole, unyenyekevu na uadilifu wake.

Tunajua sasa kwamba, ingawaje vitendo vya ufisadi vilitendeka chini ya uongozi wake, yeye mwenyewe binafsi hakuhusika moja kwa moja.

Baada ya Mzee Mwinyi kuondoka madarakani ndipo nchi hii imepata bahati mbaya si tu ya kuendelea kuelemewa na vitendo vya ufisadi katika safu za uongozi, bali pia mkosi wa kuwa na ‘kiongozi' mkuu anayesimamia ufisadi huo kwa kushiriki yeye mwenyewe binafsi kuunda kampuni ya biashara na kuisajili rasmi kwa anwani ya ofisi ya umma, na hata kujihaulishia umiliki wa kampuni ya serikali na kuiandikisha kwa jina lake na familia yake na maswahiba zake.

Tumshukuru Mungu tunayo Katiba inayoweka mipaka ya mihula ya uongozi, la sivyo baada ya mihula mitano tungeikuta nchi imehamia bara jingine kwa jinsi tamaa za wakuu zilivyozidi na jinsi matumbo yao yalivyo na nafasi za kujaza.

Kisha tumshukuru Mzee Mwinyi kwa uungwana wake, na mwisho tumwombe radhi kwa jinsi tulivyomdhalilisha.

http://www.raiamwema.co.tz/07/10/31/4.php
 
Obsever naungana na wewe kabisa. Mimi sijasahau hopelessnes ya Mzee Ruksa Presidency, najua kuna watanzania wengi ambao vichwa vyetu sio vya panzi wanaweza kukumbuka hayo. Mzee Ruksa as a person hatuhusu sana watanzania, wanaomhusu ni ndugu zake na rafiki zake. Lakini he almost brought the Country, the Union and the respect of Tanzania to is knees.
Ikulu ilikuwa pango la wanyang'anyi, ilikuwa sehemu ya watu kulia Pilau na ujinga mwingine ambao hauelezeki, how can we forget those things so easily, au ndiyo IQ zetu ni below 70!?
 
Kwanza kabisa nirudie historia. Mwaka 1989-1991 iliundwa tume ya kuuliza watanzania waamue ama tubaki na CCM au tuwe na vyama vingi. Matokeo yake 80% walitaka tubaki na CCM (akiwemo Mwinyi mwenyewe) na 20% walitaka tuwe na mageuzi. Yeye kama Rais alielekea kwa 100% tubaki na CCM (kumbuka pia Waziri Mkuu wake JSM alindwa kuongoza bunge na kuzaliwa kamati ya kuunda serikali tatu). Lakini kwa kusoma alama za nyakati marehemu JKN alipendekeza tukubali mageuzi (maoni ya 20%) hadharani na Mwinyi hakuwa na choice. Mwaka 1992 vyama vingi vilianza rasmi. Mwaka 1995 tulikuwa na uchaguzi wa vyama vingi.

Swali: Ni misingi gani aliyoiweka yeye (Mwinyi) ambayo anajivunia sasa?
 
Mwinyi is both right and wrong.On one hand (ahh, never the proverbial one armed economist lol) he had the chance to use the Nyalali Report and say 80% of the people do not want multi party and that's that.

But as president he allowed himself to be convinced that the minority deserve to be heard.

On the one hand, his noble stature is reduced by the fact that all careful students of history knew the wind of perestroika and glasnost was blowing our way from the Dachas of suburban Moskva to Eastern Europe.Nyerere and company knew if CCM was not going to take the initiative to implement multi party system, not only was the western aid going to stop and pressure to mount, but with the help of the James Mapalala's (remember CUF before it was hijacked?) and Kassanga Tumbo, a Romanian scenario complete with the Causecuing of the politrubo was not very unreal.

So he has to stop pretending like he did it out of the goodness of his heart, if that was in the 1970's or even before 1985 yes, but after 1989, pleeeeease!
 
Hivi mnakumbuka chini ya mzee Ruksa uwanja wa historia wa mnazi mmoja ulitaka kuuzwa yajengwe maduka . Hivi kweli sehemu ambayo kuna mnara wa mashujaa wa taifa ilitaka kupigwa mnada , you guys must be kidding . Ruksa was the worst president in Tanzania history , wanyonge walikuwa hawana haki ! Rushwa was the language if you had hefty pocket at that time then you were above the law.
 
Mtu wa Pwani

Ha ha ha ha ha ha ha ha ha................................WHAT? Mzee Ruksa naona huelewi maana ya hilo neno. Karibu JF ingawa upo hapa muda mrefu.

Ama kweli mwenye chongo huita kengeza.
 
Kama kweli Mzee Mwinyi alianzisha uhuru wa vyama vingi kwa nini ajipigie debe? Si historia itatukumbusha? Tangu lini Waafrika tumekuwa na hii tabia ya wanasiasa kutukumbushia: "nimewaleteeni maji, nimewajengeeni shule." If you did that don't you think the people know it? The only time you need to remind them, and only in a subtle way, is when you are campaigning for their votes.
 
Jasusi

Long time mzee karibu jukwaaani, ulikuwa umepotea kitambo.
 
Mwinyi is both right and wrong.On one hand (ahh, never the proverbial one armed economist lol) he had the chance to use the Nyalali Report and say 80% of the people do not want multi party and that's that.

Pundit ni lazima ukumbuke kuwa Mapalala alikuwa ni pandikizi la serikali, kulikuwa na maofisa kadhaa wa usalama waliokuwa wameandaliwa kuyumbisha vyama vya upinzani vitakavyoanzishwa, yeye Mapalala, Marando na Jafu walikuwa ni sehemu ya watu hao ambao walitukima kuwafool watanzania na international community, na ni kama wamefanikiwa, only recently watu wameanza kuwang'amua.
Ukweli kuhusu Nyalali report ni more complicated kuliko kusema juu juu kuwa asilimia 80 walisema wanataka chama kimoja. The story ni kuwa asilimia 20 walikuwa clear wanataka vyama vingi, na kati ya hao asilimia 80 waliosema wanataka chama kimoja, asilimia sitini ya hao walisema "LAKINI". hiyo lakini ilitaka kuwepo na mechanism ya kukidhibiti hicho chama kimoja, na ukweli ni kwamba walikuwa wanasema wanataka kuwepo na chama kinaweza kukidhibiti hicho chama kimoja walichotaka. Wenye akili akiwemo Nyerere walipopiga mahesabu waliona kuwa asilimia 80, na sio asilimia 20 ndio walitaka vyama vingi. Kwa hiyo sio kama wachache walipewa, wengi waliamua na uamuzi wa wengi ndio uliofuatwa. Naona kuna baadhi ya watu hawataki kujua ukweli huu.
 
Pundit,
Nadhani kama ulifuatilia ule mjadala ndani ya CCM ile Februari 1992 utaona kuwa wengi wa CCM walimwona Nyerere kama msaliti. Ile mind set ya chama kimoja ilikiuwa imetanda sana. Mimi niliufuatilia kwa kiasi katika redio ila bahati mbaya jioni hiyo nilikuwa naondoka kurudi huku kwa hiyo sikusikiliza hotuba zote za wajumbe wa mikoani. Lakini masuali yalikuwa inawezekanaje mwanajeshi aliyekuwa mtiifu kwa CCM awe neutral, etc, etc.
 
n dio maana naipenda JF! hakuna mtu atakayepambwa hapa. Kila mtu mkong'oto tu mpaka kieleweke.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom