Mwinjilist Aliyeshambuliwa kwa Kukashifu uislam Afariki!

Malafyale

JF-Expert Member
Aug 11, 2008
13,813
11,126
MWINJILISTI wa Kanisa la Pentekoste la Mto wa Mbu, Jackson John ambaye alikuwa mmoja kati ya waliojeruhiwa kwenye mapigano baina ya
waumini wa madhehebu ya kiislamu na kikristo yaliyotokea Februari 24 wilayani Monduli amefariki dunia.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na ndugu wa mwinjilisti huyo zinadai kuwa alifariki jana alfajiri katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC.

Mapigano hayo yalitokea baada ya waumini wa kiislamu kuwashutumu Kiongozi wa Kanisa la Full Salvation Church, Mchungaji John Chenge (29) aliyekuwa akihubiri injili eneo la Comix kwa kukashifu dini ya kiislamu.

"Ndugu yetu kafariki, unajua alipigwa sana alitobolewa na misumari kwenye kifua hata kwenye macho. Amekufa kutokana na majeraha ya misumari aliyoyapata kwenye kifua ambako baadhi ya misumari iliichelewa kutolewa; alisema mmoja wa ndugu wa marehemu ambaye
hakupenda kutaja jina lake.

Hata hivyo, Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha, Akili Mpwapwa alikana kusikia taarifa hizo.

Kwanza nyinyi nani kawaambia mimi sina hizo taarifa, sijaletewa. Ndio nazisikia kutoka kwenu," alisema Kamanda Mpwapwa.

Katika mpigano hayo vitu mbalimbali viliharibiwa yakiwamo makanisa ya Angilikana na Pentekoste, shule ya Mama Anna na nyumba za wakazi wa Mto wa Mbu kwa kuchomwa moto.

Kutokana na vurugu hizo Jeshi la polisi linawashikilia watu kadhaa, akiwamo Bwanga Musa (54), Shaban Hassan (58), Gabriel Kamunya (45), Ana Sospeter (40), Rashid Mziray (29), Frank Mwenda (42) pamoja na Bakari Twalib (18).


Source:Gazeti la Majira March 04
 
...unajua alipigwa sana alitobolewa na misumari kwenye kifua hata kwenye macho. Amekufa kutokana na majeraha ya misumari aliyoyapata kwenye kifua ambako baadhi ya misumari iliichelewa kutolewa.

Hizi dini! Hawa wanaopigana na hata kujeruhi wenzao wanazijua vizuri?
 
...unajua alipigwa sana alitobolewa na misumari kwenye kifua hata kwenye macho. Amekufa kutokana na majeraha ya misumari aliyoyapata kwenye kifua ambako baadhi ya misumari iliichelewa kutolewa;..
Hizi dini! Hawa wanaopigana na hata kujeruhi wenzao wanazijua vizuri?
Mkuu.

kwa haya yaliyotokea basi kama kuna somo moja kuu ambalo kila mtanzania mweye dini yampasa aliweke akilini mwake ni kutokukejeli dini ya mwenzake.

Tusibughudhi wengine, tusikashifu wala kukejeli dini za wengine au matokea yake tutajikuta matukio kama haya yatakuwa ni ya kawaida na mbaya zaidi chuki itajengeka katika misingi ya kidini na machafuko yatatokea katika nchi yetu.

Kunyoosheana vidole bila ya kutibu mzizi wa tatizo ni kuongeza tatizo. Tuheshimu dini za watu wasio na imani kama zetu.

Na wote watakaopatikana na hatia ya kufanya uhalifu katika tukio hili basi sheria uchukue mkondo wake.
 
Ajabu ni kwamba huko zilikoanzia hizi dini wenyewe wanaishi kwa maelewano na kuvumiliana. Ujinga uko huku kwetu ambako dini ilisafirishwa baadae tu.
 
inahuzunisha sana-ila mi nashangaa mana sehemu ukikuta mahubiri ya kiislamu-mengi utasikia wanaponda ukistro,na wanafanya hivyo kujaribu kuonyesha kuwa wao ndo wafia dini wazuri-naamini watapata malipo yao hapahapa duniani
 
RIP Mchungaji John Chenge

Mimi ninakumbuka wakati wa Mzee Rukhsa hii mihadhara iliwahi kupigwa marufuku kwasababu ilikuwa chanzo
cha uvunjifu wa amani. Lakini alipoingia mzee Mkapa kwa kuogopa akaicha tena ikaendelea. Watu masikini
and ignorance kama watanzania it is easier to brainwaish them under the guise of religion. Religion is a mental disease
(I'm sorry but I've to say it).

Hapo Manzese kuna mihadhara ya waislamu inaendeshwa kila siku, kazi yao kubwa ni kukashifu ukiristo. Lakini
serikali haichukui hatua. Siku Wakiristo wakiamua kujibu mapigo. Mnafahamu nini kitatokea "be the judge yourself".

Lakini kwakuwa serikali yetu siku hizi imepata "excuse" utamsikia JK na Wassira wake wakisema hiyo ni kazi ya CDM (SIC).

Tafadhari serikali pingeni marufuku hii mihadhara yote inayokashifu dini za watu wengine. Dini ya mwenzako kuwa mbaya
hakuifanyi dini yako kuwa nzuri. Hubirini dini zenu sio kukashifu dini za watu wengine.
 
ongopa sana tena sana vita vya kidini - hivi vinaweza kutupukutisha zaidi ya ukimwi. yale yaliyotokea Rwanda miaka hiyo yatakuja kwetu. eehh mwenyezi mungu tunusuru - liondoe shetani hili ndani ya vichwa vya watu wote wenye kutaka kupandiliza vita hii.

Kwa wakristo waliofanyikwa haya wasamehe - kwani ukipigwa shavu la kulia geuza na la kushoto - mwachieni mwenyezi mungu muweza wa yote.
 
Ile mbegu ya udini iliyopandwa na CCM wakati wa uchaguzi mwaka 2010 sasa imezaa matunda.

Hongera CCM kwa ubunifu wenu wa kuwagawa watz kwa misingi ya dini ili muwatawale daima.

Hapo hakuna atakaye patikana na hatia kwa vile walikuwa wanatekeleza sera ya chama tawala ya WAGAWE UWATAWALE.Hivi kuna sababu ya wakristo kuwa wanachama na washabiki wa CCM chama chenye agenda ya siri dhidi ya Ukristo?
 
Mkuu.

kwa haya yaliyotokea basi kama kuna somo moja kuu ambalo kila mtanzania mweye dini yampasa aliweke akilini mwake ni kutokukejeli dini ya mwenzake.

Tusibughudhi wengine, tusikashifu wala kukejeli dini za wengine au matokea yake tutajikuta matukio kama haya yatakuwa ni ya kawaida na mbaya zaidi chuki itajengeka katika misingi ya kidini na machafuko yatatokea katika nchi yetu.

Kunyoosheana vidole bila ya kutibu mzizi wa tatizo ni kuongeza tatizo. Tuheshimu dini za watu wasio na imani kama zetu.

Na wote watakaopatikana na hatia ya kufanya uhalifu katika tukio hili basi sheria uchukue mkondo wake.

Nakubaliana na wewe 100%
Ila huu ni upande mmoja wa shilingi
Pia Watanzania tujifunze kuwa wavumilivu wa kukosolewa, (ngozi ngumu kama Sam Six anavyosema)

Ukosoaji ni changamoto ya kutafuta ukweli na huleta kujengeka na kuimarika zaidi.
 
Nakubaliana na wewe 100%
Ila huu ni upande mmoja wa shilingi
Pia Watanzania tujifunze kuwa wavumilivu wa kukosolewa, (ngozi ngumu kama Sam Six anavyosema)
Ukosoaji ni changamoto ya kutafuta ukweli na huleta kujengeka na kuimarika zaidi.
Mkuu
Kukosoana ni jambo jema ila kukosoana sio kukejeliana au kukashifiana.
Katika mambo ya kawaida nafikiri uko juu ya msitari na nakubaliana na wewe lakini katika mambo ya imani za dini kuna nafasi ndogo ya kukosoa kama wewe si mwenye imani hiyo. Hata pale unapokuwa wa imani hiyo hiyo utapata vikwazo sana.

Halafu kuna na lugha utakayoitumia kufikisha ujumbe wako au namna vile utakavyokosoa. Sio kwa matusi au kukejeli au kukashifu.
Tuko pamoja mkuu.
 
RIP Mchungaji John Chenge

Mimi ninakumbuka wakati wa Mzee Rukhsa hii mihadhara iliwahi kupigwa marufuku kwasababu ilikuwa chanzo
cha uvunjifu wa amani. Lakini alipoingia mzee Mkapa kwa kuogopa akaicha tena ikaendelea. Watu masikini
and ignorance kama watanzania it is easier to brainwaish them under the guise of religion. Religion is a mental disease
(I'm sorry but I've to say it).

Hapo Manzese kuna mihadhara ya waislamu inaendeshwa kila siku, kazi yao kubwa ni kukashifu ukiristo. Lakini
serikali haichukui hatua. Siku Wakiristo wakiamua kujibu mapigo. Mnafahamu nini kitatokea "be the judge yourself".

Lakini kwakuwa serikali yetu siku hizi imepata "excuse" utamsikia JK na Wassira wake wakisema hiyo ni kazi ya CDM (SIC).

Tafadhari serikali pingeni marufuku hii mihadhara yote inayokashifu dini za watu wengine. Dini ya mwenzako kuwa mbaya
hakuifanyi dini yako kuwa nzuri. Hubirini dini zenu sio kukashifu dini za watu wengine.

nakubaliana nawe bro. hapa Manzese inaudhi saaaaaaaaaana. Hata hivyo wakristo huwa nawasifu, ni wavumilivu sana. Ipo siku ya mto wa umbu kwa serikali kufumbia macho hali hiyo.
 
Marehemu Mtume Muham-mad na Allah wamesha anza kuuwa watu Tanzania?

Waislam wapi upendo mnao dai upo kwa allah?
 
..kuna huyo aliyepoteza maisha, na waliomshambulia nao wanafuatia.

..hapo hati ya mashtaka inabadilishwa.

..labda ilikuwa kesi ya uharibifu wa mali, lakini sasa itakuwa kesi ya MAUAJI.
 
MWINJILISTI wa Kanisa la Pentekoste la Mto wa Mbu, Jackson John ambaye alikuwa mmoja kati ya waliojeruhiwa kwenye mapigano baina ya
waumini wa madhehebu ya kiislamu na kikristo yaliyotokea Februari 24 wilayani Monduli amefariki dunia.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na ndugu wa mwinjilisti huyo zinadai kuwa alifariki jana alfajiri katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC.

Mapigano hayo yalitokea baada ya waumini wa kiislamu kuwashutumu Kiongozi wa Kanisa la Full Salvation Church, Mchungaji John Chenge (29) aliyekuwa akihubiri injili eneo la Comix kwa kukashifu dini ya kiislamu.

"Ndugu yetu kafariki, unajua alipigwa sana alitobolewa na misumari kwenye kifua hata kwenye macho. Amekufa kutokana na majeraha ya misumari aliyoyapata kwenye kifua ambako baadhi ya misumari iliichelewa kutolewa; alisema mmoja wa ndugu wa marehemu ambaye
hakupenda kutaja jina lake.

Hata hivyo, Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha, Akili Mpwapwa alikana kusikia taarifa hizo.

Kwanza nyinyi nani kawaambia mimi sina hizo taarifa, sijaletewa. Ndio nazisikia kutoka kwenu," alisema Kamanda Mpwapwa.

Katika mpigano hayo vitu mbalimbali viliharibiwa yakiwamo makanisa ya Angilikana na Pentekoste, shule ya Mama Anna na nyumba za wakazi wa Mto wa Mbu kwa kuchomwa moto.

Kutokana na vurugu hizo Jeshi la polisi linawashikilia watu kadhaa, akiwamo Bwanga Musa (54), Shaban Hassan (58), Gabriel Kamunya (45), Ana Sospeter (40), Rashid Mziray (29), Frank Mwenda (42) pamoja na Bakari Twalib (18).


Source:Gazeti la Majira March 04

NI mapigano au kipigo? Waandishi wenye mrengo hawaeleweki!
 
Hivi yule jamaa aliye kashifu utatu mtakatifu kule mpanda alichuliwa hatua gani?? Afterall hii mihadhara ya kidini inapaswa ifanyike makanisani na misikitini.

Mbona sijasikia wakatoliki, anglican, aic na warutheri wakiendesha mihadhara ya mara kwa mara?? Tatizo madhehebu nayo yamekua mengi sana na mengine yanatafuta wafuasi kwa kila namna ikiwa ni pamoja na kukashifu dini na madhehebu mengine. Hii haikubaliki hata kidogo.

Watu sasa wamegeuza dini biashara.
 
NI mapigano au kipigo? Waandishi wenye mrengo hawaeleweki!
hicho kilikuwa ni kipigo kitakatifu, lol hadi misumari kama wanajenga nyumba..mmh
I can feel the sympathy and pain of the deceased.
 
RIP Mchungaji John Chenge

Mimi ninakumbuka wakati wa Mzee Rukhsa hii mihadhara iliwahi kupigwa marufuku kwasababu ilikuwa chanzo
cha uvunjifu wa amani. Lakini alipoingia mzee Mkapa kwa kuogopa akaicha tena ikaendelea. Watu masikini
and ignorance kama watanzania it is easier to brainwaish them under the guise of religion. Religion is a mental disease
(I'm sorry but I've to say it).

Hapo Manzese kuna mihadhara ya waislamu inaendeshwa kila siku, kazi yao kubwa ni kukashifu ukiristo. Lakini
serikali haichukui hatua.

MWINYI alipiga marufuku pale tu mihadhara wakati wakristo walipoanza kuwajibu waislamu kwa kuanzisha na wao mihadhara eg Kundi la BIBLIA NI JIBU, tatizo la Waislamu ni TOLERANCE hawana, wao ndiyo wana haki ya kuua na kutukana dini za wenzao, dini yao ukiijadili kidogo tu kosa! Na mauaji ya MWEMBE CHAI yalitokea baada ya Mihadhara yote kupigwa marufuku, waislamu wao hawataki Wakristo wajibu ila wao waruhusiwe kushambulia ukristo, IF YOU ARE LIVING IN A GLASS DONT THROW STONES AND IF YOU CANT TAKE BLOWS DONT THROW BLOWS! Wanataka ubondia then wanalalamika ngumi za uso!
 
Back
Top Bottom