Katika ibada ya jumapili iliyokuwa inafanyika kwenye kanisa la EFATA Nabii na mtume mwingira aliporomosha matusi ya nguvu kwenye ibada hiyo kwa watu wote wanaokwenda Loliondo na waandishi wa habari wanaojifanya kumuandika kwenye vyombo vya habari baaadhi ya maneno yenye lugha iliyopitiliza sitaweka ila mojawapo ni haya " Nasema wale wanaokwenda Loliondo ni wajinga!! nasema niwajinga!! waandishi wa habari ambao wanatabia ya kuniandikaandika kwenye vyombo ya habari ni wajinga'' nasema niwajinga, mawaziri wanaokwenda Loliondo ni wajinga!!! wanaonisema kuwa ninalaaana ya Kanisa la Moja ni wajingaaaa!!! baada ya kuporomosha maneno ambayo sio rahisi kwa mtu yeyote wa mungu kuyatamka alimalizia kwa kuwataka wamumini waitikie kwa kusema ameeen. Hata hivyo alibainisha wazi kuwa anajua kuna waandishi wa habari wapo ibadani hapo hivyo waandike wanavyoweza maana ni wajinga.
Kwenye Ibada ya jumapili ya tarehe 13/03/2011 mwingira alitoa amri mafundi waliokuwa wanarusha ibada ya jumapili kwa njia ya TV wazime ili wanachi wanofuatilia ibada hiyo wasione kashfa aliyoitoa kumkashifu babu wa loliondo hata hivyo bila kujua kuwa JF member alikuwa mmoja wa watu waliokuwa wametinga ndani ya ibada hiyo. Hata hivyo inaonesha kuwa mwingira anashida kubwa kiroho hivyo kwani taharuki na ghadhabu aliyoionyesha ibadani juu ya kuanikwa na vyombo vya habari mimi binafsi sijui nitafanyiwa maombi gani ili niamini kuwa mwingira ni nabii. Baada ya ibada baadhi ya waumini wake walisikika wakimlaumu kwa lugha alizotumia kuwasilisha hisia zake!! nimeona niwajuze wenzangu ili mjue msimamo wa nabii huyu!!!!
Kwenye Ibada ya jumapili ya tarehe 13/03/2011 mwingira alitoa amri mafundi waliokuwa wanarusha ibada ya jumapili kwa njia ya TV wazime ili wanachi wanofuatilia ibada hiyo wasione kashfa aliyoitoa kumkashifu babu wa loliondo hata hivyo bila kujua kuwa JF member alikuwa mmoja wa watu waliokuwa wametinga ndani ya ibada hiyo. Hata hivyo inaonesha kuwa mwingira anashida kubwa kiroho hivyo kwani taharuki na ghadhabu aliyoionyesha ibadani juu ya kuanikwa na vyombo vya habari mimi binafsi sijui nitafanyiwa maombi gani ili niamini kuwa mwingira ni nabii. Baada ya ibada baadhi ya waumini wake walisikika wakimlaumu kwa lugha alizotumia kuwasilisha hisia zake!! nimeona niwajuze wenzangu ili mjue msimamo wa nabii huyu!!!!