Mwili wa Dkt. Mwele Malecela wawasili Tanzania ukitokea Uswisi

Uzi umechangiwa kweli kweli huu wa marehemu Dr Mwele Ntuli. Angekuwa aliyefariki ni Mwakifyatu hata angekuwa alikuwa na wadhifa wa Katibu Mkuu Umoja wa Mataifa, sidhani kama wachangiaji wangefika hata kumi. Hapa wameshafika zaidi ya 221. Nimekumbuka ule wimbo wa Msondo ngoma!
Alikuwa anapendwa na watu, na alikuwa mioyoni mwao.
 
Alikuwa anasoma UDSM Engineering, anaitwa Senyagwa, alifarili 1984 kwa ajali akiwa anatoka Disco na benz ya baba yake. Alifia karibu na njia panda ya kwenda St. Peters Catholic church, kule Mbuyuni. Baba yake alienda kikazi Uingereza, yeye huku nyuma akamuomba mama yake ampe fungu za benz, akaenda disco la akina Kalikali enzi zile mpaka alfajiri na ndipo njiani akakutana uso kwa uso na lori, nadhani alisinzia shauri ya uchovu.
Nafahamu hiyo ajali, ilitoke hapo unapo sema zamani kulikua na kakilima fulani hivi , kulikua na jirani yetu anaitwa Terrence kwenye hiyo ajali ana aka vunjia mguu., mademu walio kuwepo nime wasahau ila na dhani nilikua nina fahamu mmoja wapo ,
 
Ippy kafa inafika miaka 20 sasa acha uwongo lemutuz alikimbilia marekani huko kaishi zaidi ya miaka 30 karudi bongo alifikia kwa baba yake...
kaja kua mpambe wa watu wenye vyeo
Wapi nimemtaja Ippy kwenye nilicho andika, Fmilia hiyo na ijua tuli kua majirani toka walipo kuwa Oysterbay na mpaka walivyo hama ,Lemutuz sikuwai muona wala kumsikia , hakuishi nao ,nilio wajua ni Huyo Kaka yao, Mwele,Seche na mwendwa. hao wadogo Kina Ntuli , Samuel and mwenzao pia siku wahi wajua labda walikua wadogo zaidi au walikua hawaja zaliwa , Ila watoto wa yule mama aliye fariki niliwajua hao wanne nilio wataja.
 
Wapi nimemtaja Ippy kwenye nilicho andika, Fmilia hiyo na ijua tuli kua majirani toka walipo kuwa Oysterbay na mpaka walivyo hama ,Lemutuz sikuwai muona wala kumsikia , hakuishi nao ,nilio wajua ni Huyo Kaka yao, Mwele,Seche na mwendwa. hao wadogo Kina Ntuli , Samuel and mwenzao pia siku wahi wajua labda walikua wadogo zaidi au walikua hawaja zaliwa , Ila watoto wa yule mama aliye fariki niliwajua hao wanne nilio wataja.
Mzee Malecela kwa kweli kapitia mapito magumu sana kifamilia.
Kufiwa na wanawe watatu, kufiwa na mke, na mtoto mmoja kuugua na kupata ulemavu licha ya kufikia ngazi ya Jaji, kibinadamu ni mapitio mazito sana.
Pale Dodoma kanisani, Askofu alimlinganisha mzee Malecela na Ayubu, lakini alimuasa asije kumuacha Mungu.
 
Mwili wa marehemu Dr. Mwele Ntuli Malecela umewasili Dar es salaam mnamo saa sita usiku na ndege ya KLM.

Mwili umepokelewa na baba yake mzee Samwel Malecela pamoja na waombolezaji wengi waliogubikwa na huzuni, na waliosubiri uwanjani toka jioni.

Msafara uliekekea moja kwa moja nyumbani kwa mzee Samwel Malecela ambapo sala fupi zilifanyika.

Mzee Abdulrahman Kinana aliyekuwa Katibu Mkuu CCM na Mama Kate Kamba Mwenyekiti wa CCM DSM, walishiriki misa hiyo fupi ya kuupokea mwili nyumbani kwa mzee Malecela.
MAZISHI
Kama scribe, nimehudhuria sehemu kubwa na mazishi ya Dr Mwele Ntuli Makecela.
Mombolezo na mazishi hayakufikia kuwa ya kitaifa lakini mahudhurio yake ni karibia kuwa ya kitaifa.
Viongozi wengi hasa waliohudumu pamoja na mzee Malecela walikuwepo.

Mzee Jakaya Kikwete
Fredrick Sumaye
Rais wa Zanzibar Hussein Mwinyi
Waziri Mkuu Majaliwa
Jaji Warioba
Mzee Mkuchika
Abdurahman Kinana
Kate Kamba
Phillip Mangula
William Lukuvi
Mama Makinda
Emmanuel Nchimbi( ingawaje kufika kwake kidogo kulikuwa na ukakasiwa siku nyingi, haswa matukio baada ya masiba wa Ippy Malecela)

Na mawaziri na viongozi vijana na viongizi wa Karibuni:

Spika Tuli Ackson
Nape Nnauye
Jauary Makamba
Harrison Mwakyembe
Stella Manyanya
Prof Mkenda
Palamagamba Kabudi

Nitendelea kujaza majina kadri ya kumbukumbu na wadau tukumbushane.

A notable absence ni Wizara ya Afya, Ummy Mwalimu.
Na waombolezaji hasa wa ngazi za juu waliunganisha ukweli wa kisyansi na experience ya Dr Mwele na kuondolewa kwake NIMR.
Mzee Fredrick Sumaye alienda mbali na kusema yule aliiyeshindwa kuukubali ukweli wa kisayansi wa Dr Mwele basi ana matatizo binafsi na ni shauri lake.

Sehemu zote waombolezaji walikuwa wengi sana.
 
Back
Top Bottom